EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 10, 2014

DIAMOND AMLIZA MAMA’KE


CHANZO: NI GPL
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amefanya tukio la kihistoria kiasi cha kumliza mama yake mzazi, Sanura Kassim ambaye alimwaga machozi kama mtoto mbele za watu.
...Mama Diamond akilia kwa furaha.
Tukio la mama Diamond kumwaga machozi lilishuhudiwa na kamera za Amani, juzi Jumatatu, mishale ya saa mbili usiku nyumbani kwake, Sinza jijini Dar es Salaam ambako kulikuwa na ‘bethidei’ ya mama huyo.

SAPRAIZI YA NGUVU
Waalikwa na mama huyo, wote walijua kuwa shughuli ilikuwa ni futari lakini kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na tukio la kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mama huyo ambayo inadaiwa alikuwa hakumbuki.
Mmoja wa rafiki wa karibu na familia hiyo, kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini, alisema kuwa hadi jioni, mama Diamond hakuwa akifahamu kuwa aliandaliwa sherehe ya siku yake ya kuzaliwa.
Kilio kikiendelea.
“Mipango yote ilifanywa kwa siri mama Diamond hakujua kilichoendelea. Diamond akiwa Marekani alitoa maelekezo mama yake afanyiwe shughuli hiyo hata kama hayupo kwa sababu siku ya kuzaliwa haijirudii,” alisema rafiki huyo.
Wema na mama mkwe wake.
KILICHOMLIZA
Muda mfupi baada ya shughuli ya kufuturu kukamilika, mama Diamond alishangaa kusikia kwamba kulikuwa na jambo jingine la ziada katika siku hiyo. Alitolewa nje huku akiimbiwa ‘happy birthday’ ndipo alipogundua kilichokuwa kikiendelea.
Mara baada ya shampeni isiyo na kilevi kufunguliwa na waalikwa kupewa, meneja wa Diamond, Babu Tale na wapambe wengine walimuongoza mama huyo hadi kwenye gari aina ya Toyota Lexus Harrier na kuelezwa kuwa ni mali yake kuanzia muda huo tamko lililomshtua na kuanza kulia akiwa haamini alichosikia!
Mama Diamond akilia huku kichwa kikiwa juu ya gari aliyopewa zawadi na mwanaye.
“Siamini macho yangu, siamini... asante sana mwanangu (Diamond), nakuombea kila kukicha mwanangu uwe na afya njema, unilee kwa upendo, asante Mungu,” alisikika mama Diamond akitamka kwa sauti iliyoambatana na kilio cha nguvu.
Muda huohuo akafunguliwa mlango na kuingia ndani ya gari hilo lililopambwa ndani kwa vitu kibao vya thamani.
Mama Diamond akiwa ndani ya gari aliyopewa zawadi.
WEMA, AUNT WAMBEMBELEZA
Machozi ya mama Diamond hayakukoma hata baada ya kushuka ndani ya gari, alionekana kuchanganyikiwa kama siyo kutoamini sapraizi ya mwanaye, ndipo Miss Tanzania 2006, aliye pia mchumba wa mwanaye,  Wema Sepetu na staa wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel walipovaa jukumu la kumtuliza.
Mastaa hao ambao ni mtu na shogaye, walimchukua mwanamke huyo na kwenda naye pembeni ambako walimsihi atulie na akubaliane na alichokiona kwani ndiyo ukweli wenyewe.
Juhudi zao zilizaa matunda, kwani muda mfupi baadaye mama Diamond alifuta machozi na kurudi katika hali yake ya kawaida ingawa alishindwa kuficha furaha yake.
Gari yenyewe ikionekana kwa mbele.
DIAMOND, WEMA NDOA LAZIMA!
Katika kuonesha kuwa sasa amekubali kwa dhati Wema awe mkwewe, mama Diamond aliapa lazima ahakikishe mwanaye anafunga ndoa na mlimbwende huyo.
“Hilo nataka mlijue kabisa. Nitafanya juu chini Diamond amuoe Wema maana ana roho nzuri sana. Niseme ukweli kuwa huyu msichana ndiye chaguo langu na wanaendana sana na mwanangu.
“Angalia wakiwa pamoja, mwanangu anapata mafanikio makubwa sana, nadhani nyota zao zinaendana hivyo sina pingamizi lolote. Ninachotaka ni kuhakikisha wanaoana,” alisema mama Diamond.
Keki iliyotolewa oda na Diamond iliyoandikwa ujumbe wake maalum.
THAMANI YA GARI
Akizungumzia thamani ya gari hilo, Babu Tale alisema ni shilingi 34,000,000 (milioni 34) ikiwa ni pamoja na mazagazaga mengine baada ya gari hilo kununuliwa.
“Hiyo milioni 34 ni pamoja na muziki unaouona ndani ya gari, hizi skrini tatu na mazagazaga mengine kama mnavyoona,” alisema Babu Tale huku akiwaonesha waandishi wetu.
Mama Diamond akikata keki maalum.
DIAMOND BONGO
Hadi tunakwenda mitamboni, Jumanne usiku, ilielezwa kuwa, Diamond alitarajiwa kutua jana Jumatano katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akitokea Marekani alipokuwa kwenye kinyang’anyiro cha Tuzo za BET.
Habari kutoka ndani ya familia zilieleza kuwa, nyota huyo naye ameandaliwa sapraizi ya nguvu kutoka kwa kampani yake wakishirikiana na familia. “Wamejiandaa vya kutosha kumfanyia saprazi ya nguvu na yeye mara tu atakapotua Bongo. Wanafanya siri sana, haijajulikana atafanyiwa nini,” kilipasha chanzo chetu.
Mama Diamond, Bi. Sanura akimlisha keki 'mkwewe' Wema Sepetu katika sherehe yake ya kuzaliwa.
DIAMOND ANATISHA
Nyota ya Diamond imeonekana ikiwaka sana siku za hivi karibuni ambapo amekuwa akipiga shoo za mara kwa mara katika nchi mbalimbali huku akishirikishwa kwenye tuzo za ndani na za kimataifa.
Si jambo la ajabu kusema kuwa, Diamond kwa sasa ndiye Mwanabongo Fleva anayefanya vizuri zaidi pengine kuliko wote katika muziki huo – MHARIRI.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate