EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 17, 2014

Shule 10 bora 2013 zaporomoka

Arumeru. Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kisirimi wilayani Arumeru, Arusha, Emmanuel Kisongo amesema kufanya vizuri kwa shule yake ni kuthibitisha shule za kata zinaweza kuwa bora nchini.

Kismiri (pichani) imeshika nafasi ya tatu kati ya shule 10 bora nchini mwaka huu, kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa jana na Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwalimu Kisongo alisema mwaka huu wanafunzi wa shule yake wamefanya mtihani wa kidato cha sita kwa mara ya saba na shule imefanikiwa kushika nafasi ya tatu kitaifa kwa mara ya kwanza.

“Nimefurahi tumeingia kwenye shule 10 bora nchini mara tano na safari hii tumeshika nafasi ya tatu. Ni wazi shule za kata zinaweza, tofauti na fikra za wengi kuwa shule zipo chini kielimu,” alisema.
Kisongo alisema mwaka jana walishika nafasi ya tano, kitaifa na mwaka juzi, walishika nafasi ya tatu kama mwaka huu.

“Siri ya mafanikio yetu ni ufundishaji mzuri na ushirikiano mzuri wa walimu, wanafunzi na wazazi kwa lengo kubwa la kuthibitisha kuwa walioanzisha shule ya kata hawakufanya makosa,” alisema.
Alisema shule yake, ambayo ina jumla ya walimu 32 kati yao 12 wanafundisha kidato cha tano na sita, inafuata michepuo ya sayansi na sanaa (art) na mwaka huu wanafunzi 52 walifanya mtihani.
“Tunajivunia mafanikio haya na malengo yetu kuifanya shule hii kuwa bora nchini kwani ipo katika mazingira tulivu na wanafunzi wa dini zote tunawajenga kuwa na hofu ya Mungu,” alisema.
Alisema kwa sasa wanafunzi wa shule hiyo, wanajitambua na wanaheshimu masomo yao. Hawana muda wa migogoro na shule, jambo ambalo linawapa muda mzuri kusoma.

Shule 10 bora 2013 zaporomoka
Ibrahim Yamola, Mwananchi
Dar es Salaam. Shule za sekondari zilizokuwa kwenye orodha ya Kumi Bora ya matokeo ya kidato cha sita mwaka jana zimeporomoka, huku shule isiyo maarufu ya Igowole, mkoa wa Iringa ikichomoza kutoka nafasi ya nane hadi ya kwanza mwaka huu.

Mazingira ya Shule ya Sekondari ya Igowole iliyopo Wilaya ya Mufindi ni ya kawaida sana, huku kwa muda mwingi wa msimu wanafunzi wakipigwa na baridi kali katika eneo lilipo shule hiyo iliyozungukwa na miti mikubwa.
Katika matokeo ya kidato cha sita mwaka jana, Necta ilipanga shule 10 bora kulingana na idadi ya watahiniwa juu ya 30 na chini ya 30, lakini mwaka huu imeziweka kundi moja, kwa mujibu wa kaimu katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles E. Msonde.

Mwaka jana, kati ya shule 10 zilizokuwa na watahiniwa zaidi ya 30, ni shule nne pekee zimeendelea kuwamo katika kundi la shule 10 bora kitaifa mwaka huu licha ya mabadiliko hayo. Shule hizo ni Marian Girls (Pwani) imekuwa ya sita mwaka huu wakati ilishika nafasi ya kwanza 2013. Shule ya Feza Boys (Dar es Salaam) imeshika nafasi ya pili mwaka huu wakati mwaka jana ilikuwa ya tatu.
Shule ya Sekondari ya Kibaha (Pwani) imeshika nafasi ya tano wakati mwaka jana ilishika nafasi ya tisa. Kisimiri (Arusha) imekuwa ya tatu ilhali mwaka jana ilikuwa ya tano kitaifa.
Shule zilizokuwa 10 bora mwaka jana lakini mwaka huu hazimo katika nafasi hiyo ni; Mzumbe (Morogoro) iliyokuwa ya pili, Ilboru Arusha (4) na Mtakatifu Mary Mazinde Juu ya Tanga (6).
Nyingine ni Tabora Girls (7) na Kifungilo Girls ya Tanga iliyoshika nafasi ya 10.

Katika kinyang’anyiro hicho, shule zilizochukua nafasi ya shule zilizong’olewa katika kumi bora na nyingine kupanda kutoka nafasi moja hadi nyingine ni Igowole (Iringa) iliyoshika nafasi ya kwanza mwaka huu na mwaka jana ilikuwa ya nane. Iwawa (Njombe) imeshika nafasi ya nne. Nyingine ni Nangwa (Manyara) nafasi ya saba, Uwata (Mbeya-8), Kibondo (Kigoma-9) na Kawawa (Iringa) imefunga ukurasa kwa kuwa ya kumi.
Shule zilizokuwa za mwisho mwaka jana katika kundi la wanafunzi chini ya 30 na zaidi ya 30 mwaka huu licha ya mabadiliko hayo ni shule tatu ziliyobaki na nyingine maarufu zikiingia kwa mara ya kwanza.
Baadhi ya shule zilizoshika mkia ni Fidel Castro (Pemba), Tambaza (Dar es Salaam), Muheza (Tanga), Mtwara Technical (Mtwara) na Iyunga Technical ya Mbeya. Al-Falaah Muslim (Unguja) na Osward Mang’ombe (Mara) zikiingia kwa mwaka wa pili mfululizo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate