EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 19, 2014

TAMASHA LA MATUMAINI 2014: WABUNGE KUTWANGANA ‘LIVE’


AGOSTI 8, mwaka huu Uwanja wa Taifa patakuwa hapatoshi kwani Watanzania watashuhudia matukio makubwa ya burudani kupitia Tamasha la Usiku wa Matumaini.
Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba.
Miongoni mwa matukio hayo ni ndondi za waheshimiwa wabunge ambapo mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kigwangala atakazichapa ‘kavukavu’ na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba.

Akizungumza na Mikito Nusunusu, Mratibu wa tamasha hilo lenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya sekondari nchini, Luqman Maloto alitaja burudani kibao zitakazolipamba tamasha hilo ikiwemo mechi ya wabunge mashabiki wa Simba na wenzao wa Yanga, Bongo Fleva dhidi ya Bongo Movie.
Mbunge wa Nzega, Dkt. Hamis Kigwangala akiongea na wanahabari wa Global Publishers (hawapo pichani).
“Wabunge wa Yanga sasa hivi wanatamba na usajili mpya wa Ridhiwani Kikwete wakati wenzao wa Simba wakiwa na Geodfrey Mgimwa sasa sijui mwaka huu nani ataibuka bingwa kwani mwaka jana Yanga walishinda kwa ushindi mdogo wa 1-0,” alisema Maloto.
Yemi alade wa Nigeria kulitikisa jukwaa
Maloto alisema kwa upande wa burudani ya muziki, atadondoka mkali kutoka Nigeria anayetamba na wimbo wa Johnny, Yemi Alade ambaye ameahidi kumtafuta Johnny wake katikati ya maelfu ya mashabiki watakaojitokeza uwanjani siku hiyo.
Hapatoshi kwenye soka
Kama hiyo haitoshi, Maloto alisema katika upande wa mpira wa miguu, mwaka jana kwenye tamasha hilo mechi kati ya Bongo Movie na Bongo Fleva, Bongo Fleva waliibuka kwa ushindi wa bao 1-0 safari hii mambo yatakuwaje?
“Tayari Bongo Movie wameshataja kikosi kamili kitakachoongozwa na kipa wao mahiri Mzee Majuto ‘King’ huku wakiwa kambini chini ya kamati ya ufundi inayoongozwa na Fatuma Makongoro ‘Bi Mwenda’ wakiahidi kuwateketeza kabisa Bongo Fleva,” alisema Maloto.
Kwenye kipengele cha ndondi, Maloto alisema pia kutakuwa na kipute kikali kati ya bondia anayeshikilia mkanda wa UBO (Universal Boxing Organization), Thomas Mashali ‘Simba Asiyefugika’ atakayezipiga na mpinzani wake wa siku nyingi, Mada Maugo ‘Mbunge Mtarajiwa’ huku mwanamuziki Khalid Chokoraa akipimana ubavu na Said Memba, Jacob Steven ‘JB’ atamaliza ubishi unaoendelea kwa sasa kwa kuchapana na Cloud 112 pambano hilo likiwa na raundi nne tu.
Maloto alisema, burudani haitaishia hapo, anga la muziki litashambuliwa na Ally Saleh ‘Ali Kiba’ ambapo atapanda jukwaani na kupiga nyimbo zake zote kali sambamba na kutoa sapraizi ya ukimya wake kwa mara ya kwanza.
Mastaa wengine watakaopokezana kipaza sauti ni pamoja na Meninah, R.O.M.A Mkatoliki, Madee, Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, Wema Sepetu ambaye ataimba nyimbo za bebi wake ‘Diamond’ pamoja na wengine kibao.
“Listi ya waburudishaji ni ndefu, wasomaji waendelee kufuatilia magazeti ya Global Publishers watajuzwa kadri siku zinavyosogea,” alisema Maloto.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate