EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 26, 2014

DENTI AMUUA MWANAYE, AMFICHA UVUNGUNI

MWANAFUNZI wa Chuo cha Uuguzi Chimala wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya,  Vena Mtati (27) (pichani) anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa kwa madai mazito ya kumuua mtoto wake kwa kumnyonga, kumtumbukiza kwenye mfuko wa rambo na kuutia ndani ya mfuko wa salfeti kisha kuuficha chini ya kitanda, Uwazi lina habari ya motomoto!
Vena Mtati akitahayari baada ya kutiwa mbaloni na polisi.
Tukio hilo la kikatili ambalo limewashangaza wengi, hasa ikizingatiwa kuwa mtuhumiwa huyo anajua sheria kwa sababu anajifunza uuguzi, lilijiri Agosti 21, mwaka huu ndani ya nyumba moja iliyopo Kijiweni, Kata ya Mvinjeni mjini hapa.

SHUHUDA
Kwa mujibu wa shuhuda ambaye anaishi jirani na nyumba inayodaiwa kufanyika mauaji hayo (jina lipo), wiki mbili zilizopita, mtuhumiwa huyo alifika kwenye nyumba hiyo akitokea chuoni akiwa na ujauzito.
“Wiki mbili zilizopita, Vena alifikia kwa rafiki yake anayeitwa Joyce ambaye alikuwa amepangisha katika hiyo nyumba. Vena alikuwa na mimba kubwa, baada ya siku tano tu akajifungua,” kilisema chanzo hicho.
Kikaongeza: “Siku ya tukio, Joyce yeye ambaye ni mwenyeji alitoka kwenda katika shughuli zake, akamuacha Vena akiwa chumbani. Nadhani ndipo aliposhikwa na uchungu, akajifugua mtoto wa kike.
“Ilikuwa asubuhi, sisi tukasikia kelele kutoka kwenye chumba hicho. Zile kelele zilikuwa si za kawaida! Ilikuwa kama vile kuna mtu anakabwa.
Akiwa chini ya ulinzi.
“Tuliposikiliza kwa makini, mara sauti ya redio ikaongezwa ili kufanya kelele hizo zisisikike kwa nje. Lakini kwa vile sisi majirani  tulijua kwamba ndani ya chumba kile kuna mjamzito na kelele alizopiga mtoto si za kawaida ndipo tulipomtafuta mwandishi wa habari (hizi),” kilisema chanzo hicho.
HATUA ZA HARAKA
Mwandishi wetu alipopatikana na kunyetishiwa kuhusu kuwepo kwa uwezekano wa mama ambaye ni nesi kumuua mtoto wake aliyejifungua, aliwasiliana na Polisi wa Dawati la Jinsia.
Polisi hao, awali walimtafuta mwenyeji wa mtuhumiwa huyo, yaani Joyce ambaye alikuwa kwenye  mihangaiko yake. Alipopatikana alipokonywa simu yake ya mkononi ili asiweze kuwasiliana na mtuhumiwa.
Aliulizwa kama ana mgeni nyumbani kwake, akakiri. Akaulizwa kama mgeni huyo amejifungua, akakataa ndipo wakamchukua kwenda naye nyumbani kwake kumfuata mtuhumiwa huyo.
ASKARI WAFIKA ENEO LA TUKIO
Paparazi wetu akiwa ameongozana na askari hao walifika kwenye chumba hicho na kumkuta Vena akiwa amesimama mlangoni.
Alipoulizwa kama amejifungua, awali alikataa katakata lakini baada ya  kubanwa na kutishiwa kuswekwa ndani, alikiri kujifungua na kusema kwamba mtoto huyo amemficha uvunguni mwa kitanda.
Denti (aliyeshika kiroba chenye mwili) akiwa chini ya ulinzi wa polisi (Kulia) ni mwenyeji wake, Joyce.
DAMU SAKAFUNI
Ndani ya chumba hicho, sakafuni kulikuwa na damu  zilizodaiwa kumtoka mtuhumiwa huyo wakati akijifungua mwenyewe!
POLISI WAPEKUA UVUNGUNI
Polisi walizama chumbani, wakainama kuchungulia chini ya kitanda. Walichoanza kukiona ni mfuko wa salfeti, wakauvuta  kuutoa. Walipofungua ndani, wakakuta mfuko wa rambo, wakaingiza mkono na kutoa kifurushi kikiwa kimeviringishwa nguo nyingi na ndiye mtoto huyo alimohifadhiwa.
HEBU SOMA HII, INAUMA ZAIDI
Mbali na mwili wa mtoto huyo kuviringishwa nguo hizo, pia ulimwagiwa chumvi na vumbi la mkaa ambapo ilidaiwa mtuhumiwa alifanya hivyo ili mwili huo usitoe harufu utakapotupwa porini.
Majirani walisema maarifa hayo, mtuhumiwa aliyapata kwa sababu tayari anajua namna ya kuhifadhi mwili wa mwanadamu, kwa mwanamke asiye na ujuzi asingeweza kufanya hivyo.
Vena Mtati akiwa na kiroba hicho.
SABABU YA MTOTO KUUAWA
Kuna madai kwamba, mtuhumiwa huyo aliwaambia polisi kuwa alifikia uamuzi wa kumuua mtoto huyo kufuatia mwanaume aliyempa ujauzito aishiye jijini Dar es Salaam kumuahidi ndoa lakini akaingia mitini.
ORODHA YA WALIOKAMATWA
Baada ya polisi kusikiliza maelezo ya mtuhumiwa huyo, walimkamata yeye, mwenyeji wake Joyce na mmiliki wa nyumba hiyo ambaye jina halikupatikana mara moja.
Polisi walisema mmiliki wa nyumba hiyo alikamatwa kwa sababu alikiuka sheria za mji ambapo alitakiwa kutoa taarifa za kumpokea mgeni huyo kwenye serikali za mitaa lakini hakufanya hivyo huku Joyce akidaiwa kutambua kuwa mgeni wake alijifungua lakini akawaambia hakujifungua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate