EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 1, 2014

DIAMOND: SITAOA KAMWE, WEMA ANA CHAKE

CHANZO NI GLOBAL PUBLISHERS
Kutoka moyoni? Wakati bimkubwa Wema Isaac Sepetu akijiaminisha na kuhisi kuwa amepata mume ambaye ni baba bora, mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amefunguka kuwa kamwe hafikirii kuoa, Ijumaa lina cha kukuhabarisha.
Wema Isaac Sepetu akiwa kwenye pozi la kimahaba na mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’
Kauli hiyo ya Diamond inakuja wiki kadhaa baada ya Wema kuonekana na pete ya ndoa kidoleni kisha kukiri kuvishwa na ‘kichaa’ huyo wa Bongo Fleva ambaye amerejea kutoka Marekani alikotwaa Tuzo ya Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki zilizokwenda kwa jina la African Muzik Magazine (AFRIMMA) 2014.

Hofu ya kuoa
Akizungumza na gazeti hili kwenye mahojiano maalum, Diamond alisema kuwa anahofia kuoa kwa madai kwamba akifanya hivyo anaweza kuanguka kimuziki kitu ambacho hataki kimtokee maishani mwake.
Kumbe!
Jamaa huyo ambaye siku hizi anajiita Dangote (jina la tajiri wa Nigeria, Aliko Dangote) alitiririka kuwa zamani alikuwa na wazo hilo la kuoa lakini akiwatazama wanamuziki wenzake waliooa mwisho wa siku, makali yao hupungua na wengine kupotea kabisa kwenye ramani ya muziki.
Bofya hapa kumsikia Diamond
“Unajua unaweza kuona kama vile nazungumza kitu cha utani lakini ndiyo ukweli wenyewe.
“Kuna wanamuziki wengi walikuwa kwenye peak (kileleni) lakini walipooa tu ‘kiki’ yao ilishuka ghafla katika muziki na wengine wamepotea kabisa.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Mtangazaji wa Radio E-FM, Penniel Mungilwa ‘Penny’.
“Ukifuatilia kwa umakini wapo mastaa wengi duniani ambao umri umekwenda sana lakini hawajaoa. Hata hapa nyumbani kuna mifano hai. Nadhani hofu yao ni kuona kuwa wakifanya hivyo watashuka kimuziki,” alisema Diamond.
Ni kweli kamvisha pete Wema?
Alipoulizwa kama ni kweli amemvisha pete ya uchumba Wema, msanii huyo hakuwa tayari kufafanua kwa kigezo kwamba pete ni urembo kama urembo mwingine kwa mwanamke.
Nje ya boksi
Baada ya kusikia msimamo wa Diamond, gazeti hili lilijiongeza na kutoka nje ya boksi ambapo lilizungumza na baadhi ya wasanii waliooa na wasiooa ambapo walieleza mambo mazito.
Jacqueline Wolper
Siri yafichuka
Katika mazungumzo yao kwa sharti la kutochorwa gazetini, wasanii hao walidai kwamba Diamond anahofia kupoteza kiki kwa warembo ambao wengi ndiyo mashabiki wake wanaoamini nao wanaweza kupata zali la kuolewa naye ndiyo maana humzingira na kumuomba namba ya simu kila anakokwenda.
Msururu wa mademu
Ilielezwa kwamba kwa kuwa jamaa huyo hupenda kuwa juu ndiyo maana alisharipotiwa kutoka na msururu wa wanawake mastaa ambao huchangia jina lake kuendelea kuwa juu.
Ilidaiwa kwamba wakati anatafuta namna ya kuchomoka kimuziki alidaiwa kutoka kimapenzi na warembo waliokuwa na majina madogo kama Rehema Fabian aliyepata umaarufu kupitia Shindano la Miss Kiswahili.
Jokate Mwegelo.
Ilisemekana kwamba baada ya hapo alidaiwa kuwa na msururu wa wanawake mastaa kama waigizaji Jacqueline Wolper Massawe na Aunt Ezekiel Grayson na Jokate Mwegelo.
Baadaye jamaa huyo alidaiwa kuruka na wasichana ambao hawakuwa na kiki hivyo aliwamwaga ndani ya muda mfupi kama Najma na Natasha.
Baadaye Diamond alitua kwa Wema hadi akafikia hatua ya kumvisha pete ya uchumba mwaka 2012 ndani ya Ukumbi wa New Maisha uliopo Masaki jijini Dar.
Kumbukumbu zinaonesha kwamba muda mfupi baada ya kumvisha Wema pete ya uchumba walimwagana ambapo Diamond alitua kwa Mtangazaji wa Radio E-FM, Penniel Mungilwa ‘Penny’.

Irine Uwoya
Diamond hakudumu na Penny kwa madai kwamba mrembo huyo hakuwa na kiki kama ilivyokuwa kwa Wema ambaye jina lake halijawahi kushuka tangu alipovaa Krauni ya Miss Tanzania 2006/07.
Ilisemekana kwamba hata tuzo zilipungua ndipo akampiga Penny chini na kurudi kwa Wema ambaye inasemekana ndiye anayemng’arisha.
Hawa wameoa, je, wameshuka?
Baadhi ya mastaa waliooa ni pamoja na Mohamed Ahmed ‘Z-Anto’, Nurdin Bilal ‘Shetta’, Amini Mwinyimkuu, Lawrence Marima ‘Marlaw’, Amani Temba ‘Mheshimiwa Temba’ na wengineo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate