EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, August 31, 2014

Freeman Mbowe apata ‘mbabe’ mwenzake

 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Tabora, Kansa Mbarouk (aliyevaa gwanda) akirudisha fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti Taifa wa chama hicho. Waliomzunguka ni walinzi wake. Na Mpigapicha Wetu 

Dar es Salaam. 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Tabora, Kansa Mbarouk amejitokeza ‘kupimana kifua’ na Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe katika uchaguzi wa ndani unaotarajiwa kufanyika Septemba 14.

Mbarouk alirejesha fomu hizo makao makuu ya Chadema jana mchana huku akikumbana na kizingiti cha kuzuiwa na walinzi kuingia ndani kurejesha fomu akiwa pamoja na waandishi wa habari na hata alipotoka nje hakutakiwa kuzungumza na waandishi hao karibu na jengo hilo.

Ili kuepusha vurugu, Mbarouk alitoka eneo hilo na kuanza kuzungumza na waandishi wa habari kwa kusema, “Hili ambalo limenipata kwa kuzuiwa nisipigwe picha wakati nikirejesha fomu nikiingia madarakani nitahakikisha narejesha usawa ndani ya chama hiki na katiba inazingatiwa.”

Aliongeza, “Jambo la pili kulifanya nitahakikisha wanachama wote ndani ya Chadema wanakuwa na haki sawa, hakuna atakayeonewa na atakayevunja katiba kwa njia zozote zile atachukuliwa hatua kali, hakuna atakayekuwa juu ya katiba ya Chadema.”
Juzi, Mbowe alikabidhiwa fomu na makada wa chama hicho na kumtaka awanie tena kiti hicho, ombi ambalo alilikubali na kufungua milango kwa wanachama wengine ‘kupimana naye kifua’.

“Nafasi bado ipo, anayetaka kupima kifua na mimi ajitokeze. Tena nawaomba viongozi wangu msizuie fomu kwa anayetaka,” alisema Mbowe ambaye ameongoza chama hicho kwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano.

Mbarouk alisema, kulingana na katiba ya chama Mbowe amemaliza muda wake wa uongozi na anatakiwa kukiachia kiti hicho kiongozwe na mtu mwingine.
“Mimi nimekuwa mwenyekiti wa mkoa (Tabora) kwa kipindi cha miaka 10 nikaamua kuachia ili wengine waendeleze vivyo hivyo na Mbowe ameongoza kwa miaka kumi anatakiwa kuachia ngazi, na hii ni nafasi yangu imewadia kuiongoza Chadema kufika Ikulu 2015,” alisema Mbarouk.

Huku akisisitiza alisema, “Kauli aliyoitoa Mbowe ya kusema anayetaka kujipima kifua naye ajitokeze ni ya kuwatisha wanachama wasijitokeze, lakini mimi siwezi kutishika na ndiyo maana nimejitokeza kupimana naye kifua na ninajua nitamshinda kwani katiba ikizingatiwa tu hawezi kunishinda.” Uchaguzi huo utatanguliwa na wa Baraza la Vijana Taifa la Chadema, (Bavicha) utakaofanyika Septemba 10 huku Septemba 11 ukifanyika wa Baraza la Wanawake (Bawacha).

Hadi dirisha la urejeshaji fomu linafungwa jana saa 10.30 makada mbalimbali walikuwa wamejitokeza kuwania nafasi hiyo miongoni ni Daniel Madiba anayewania Mratibu Mhamasishaji taifa wa Bavicha na wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Lutiger Haule nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu kupitia Vijana. Haule alisema anataka kuwatumikia vijana katika kupata haki zao na atatumia nafasi hiyo kuwapigania kwa nguvu zote katika harakati za kusaka ukombozi wa pili unaominywa na CCM.

Ushindani ndani ya Bawacha unatarajiwa kuwa kati ya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge Viti Maalum, Chiku Abwao na makada wengine, Lilian Wasira na Sophia Mwakagenda kwa nafasi ya mwenyekiti.

Katika hatua nyingine, nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Baraza la Wanawake ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), imeendelea kupata wagombea baada ya Aisha Yusuf kuchukua fomu na kuirejesha kuwania nafasi hiyo.

Akizungumza katika ofisi za chama hicho zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, Aisha alisema kuwa amelazimika kuwania wadhifa huo kutokana na kuwa na uwezo wa kutosha. “Hivi sasa ukiangalia wanawake wengi bado wapo nyuma hivyo ni wakati wa kuondokana na dhana hiyo ndiyo maana nami nimelazimika kuomba nafasi hiyo,” alisema Aisha.

Alisema kuwa tangu alipojiunga na chama hicho mwaka 2007 amepata uzoefu ikiwamo kuwa Mwekahazina wa Bawacha Kata ya Saranga hivyo ameomba ngazi ya juu zaidi ili aweze kuwatumikia wananchi kwa ukaribu.

Aisha alisema kuwa ni vyema wanawake wakatambua wao ni jeshi kubwa linaloweza kuleta mabadiliko ndani ya Tanzania akieleza kwamba sasa taifa lina matatizo makubwa hivyo wanawake wanapaswa kujitokeza kwa wingi na kuchukua fomu ili kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

“Wanawake ni lazima tuwe jasiri ni lazima tuondokane na mifumo dume inayotukandamiza hiyo itatusaidia tupate nafasi za juu za uongozi katika uchaguzi mkuu ujao,” alisema.

Aisha alisema kuwa anaamini kuwa taifa hili litaweza kupata maendeleo zaidi ikiwa wanawake wengi watapata nafasi nyingi za uongozi.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate