EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 6, 2014

Mjumbe Ukawa atinga bungeni

Dodoma.
Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.
Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi).

CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.
Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.

Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni.
Baadaye alipoulizwa imekuwaje akajiandikisha ilhali uongozi wa chama chake umesema hawatashiriki, Mwatuka alijibu: “Kwa hapo ni mapema sana kuzungumzia suala hilo, nitazungumza kesho (leo) kule bungeni ukinitafuta.”


Hata hivyo, baada ya dakika kama 30 kupita, Mwatuka alimpigia simu mwandishi na kumwambia: “Sasa kuhusu mimi kuja Dodoma, ni kweli kwamba niko hapa maana nasomesha na nilipofika nimeamua kwenda pale bungeni kuripoti.”

Aliogeza: “Ila mimi pamoja na kujiandikisha, sitashiriki vikao vya Bunge mpaka hapo tutakapokuwa tumepewa mwongozo, maana tuliambiwa kwamba majadiliano yanaendelea kwa hiyo tukiruhusiwa nitakwenda, vinginevyo sitashiriki kabisa, ndiyo hivyo.”
Bwanausi kwa upande wake alisema alimpa lifti Mwatuka kutoka Dar es Salaam baada ya mbunge huyo wa CUF kuomba msaada wa usafiri kwenda Dodoma.

“Ni jambo la kawaida, tulionana Dar es Salaam na akaniuliza iwapo ninakwenda Dodoma na mimi kweli nafasi ilikuwapo kwenye gari, kwa hiyo tumekuja naye hadi hapa, sasa zaidi ya hapo mimi sifahamu,” alisema.

Wajumbe kutoka Zanzibar na wale wa kundi la 201 ndiyo waliokuwa wengi katika usajili wa jana na wajumbe ambao wanatokana na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hasa kutoka Tanzania Bara wakionekana wachache.

Milango yote ya kuingia katika eneo la Bunge ilikuwa imefungwa na kuacha lango moja tu la Magharibi, hali iliyosababisha baadhi ya wajumbe kuhangaika hadi pale walipopata msaada wa polisi waliokuwa wakilinda.

Mkutano wa Bunge Maalumu ambao unafanyika kwa mara ya pili, unatarajia kuchukua miezi miwili ambayo wajumbe wake wanapaswa kuitumia kukamilisha kazi ya kupitia sura 15 za Rasimu ya Katiba zilizosalia na kupiga kura kuamua kuhusu sura mbili zinazohusu Muungano.
Katika mkutano uliomalizika Aprili mwaka huu, wabunge walikuwa wametumia zaidi ya siku 70 na walifanikiwa kupitia sura ya kwanza na sita ambazo hata hivyo, hazikupigiwa kura.
Hadi jana jioni Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta alikuwa akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi, lakini hakukuwa na taarifa rasmi kuhusu ratiba wala ajenda za mkutano unaotarajiwa kuanza leo.

Wabunge wapata ajali
Katika tukio jingine, Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage na Mbunge wa Viti Maalumu, Munde Tambwe wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria wakati wakitokea Tabora kwenda Dodoma kupata ajali.

Wabunge hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na hali zao zilikuwa zinaendelea vizuri.
Akizungumza akiwa katika Wodi Namba 18, Rage alisema amepata majeraha katika bega la kushoto na eneo la nyuma ya mgongo baada ya dereva wa gari walilokuwa wakisafiria kujaribu kulipita lori lililokuwa mbele yao, lakini ghafla lori hilo likaingia katikati ya barabara.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Ezekiel Mpuya aliwataja majeruhi wengine wa ajali hiyo iliyotokea katika eneo la Chigongwe, Dodoma kuwa ni Issa Chimwaga (31), Mwanahamisi Ramadhani (34) na dereva John Hoya (32) ambaye hakuuumia.
Alisema vipimo vimeonyesha kuwa mbali na kupata majeraha usoni na kichwani, Munde pia amevunjika mkono wakati Rage ameteguka bega la kushoto.VIA MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate