EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 13, 2014

MZUNGU AINGILIA PENZI LA WEMA


Stori: Erick Evarist/Global Publishers
MALOVEE? Mzungu aliyekuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba, Zdravko Logarusic ‘Loga’ anadaiwa kuingilia penzi la mwigizaji Wema Sepetu.
Ishu hiyo imebumburuka ikiwa ni siku chache tangu Diamond atangaze kuwa hayupo tayari kuoa akidai atashuka kimuziki.

Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba, Zdravko Logarusic ‘Loga' akipata ukodaki na Wema Sepetu ndani ya ofisi za Global.
KUMBE ALIMZIMIA KITAMBO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Mcroatia huyo alimzimia Wema mara tu baada ya kutua nchini Desemba, mwaka jana na kumuona mlimbwende huyo ‘akishaini’ kupitia vyombo vya habari, akajiwekea nadhiri kwamba lazima ampate.


CHANZO CHATIRIRIKA
“Loga alimzimia kinoma Wema baada ya kumuona kwenye vyombo vya habari na kuanza kufuatilia baadhi ya filamu zake ambazo zilikuwa zilimkonga moyo kila alipozitazama.
“Baada ya kuvutiwa naye, mtu mzima (Loga) akaanza kutafuta mbinu za kumuimbisha Wema,” kilidai chanzo.

Chanzo hicho kilidai kwamba baada ya kocha huyo kupata wazo la kumtongoza Wema, alianza kumsaka katika viwanja ambavyo aliamini mrembo huyo anatembelea ili aweze kufanikisha azma yake ya kuonja penzi la Beautiful Onyinye.
Zdravko Logarusic ‘Loga'akiwa kazini.
AMSAKA NYUMBANI KWAKE
Ilisemekana kuwa mara kadhaa alishafanya jitihada za kumfuata Wema nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar lakini kila alipotia mguu, hakufanikiwa kuonana na mrembo huyo.
Hata hivyo, ilisemekana kwamba Loga hakukata tamaa kwani alionekana kudata kadiri siku zilivyozidi kuyoyoma.

“Jamaa alipiga sana misele pale Kijitonyama lakini bahati mbaya, misele yake haikuzaa matunda lakini kwa kuwa alikuwa na nia, hakukata tamaa, aliendelea kumsaka katika viunga mbalimbali ambavyo aliamini Wema yupo,” kilidai chanzo hicho.
ZALI LA MENTALI
Kikizidi kumwaga taarifa, chanzo hicho kilibainisha kuwa jitihada za Loga kukutana na Wema zilizaa matunda Aprili 22, mwaka huu maeneo ya Mwenge ambapo bila kutegemea, wawili hao walikutana kila mmoja alipokuwa katika mizunguko yake ya kikazi.

“Ilikuwa kama zali tu siku hiyo, Wema alikuwa katika ofisi moja hivi ambayo alikuwa akifanya shughuli zake za kikazi lakini wakati huohuo Loga naye alitia timu katika ofisi hiyo kwa shughuli zake za kikazi ndipo ilipokuwa golden chance,” kilizidi kudai chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa Wema.
Mkali wa Bongo Fleva na Mpenzi wa Wema Sepetu, Abdul Naseeb, 'Diamond'.
NDOTO ZAANZA KUTIMIA
Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, mara baada ya wawili hao kukutana, pointi ya kwanza muhimu kwa Loga ilikuwa ni kubadilishana namba na mrembo huyo kisha kufanya naye mazungumzo ya kawaida kwa dakika kadhaa.

Ilisemekana kwamba, siku hiyo Loga alionekana mwenye furaha kwani licha ya kubadilishana namba za simu, ilielezwa kuwa walipata fursa ya kupiga picha za pamoja na kutumiana kupitia simu zao hivyo ukaribu wao kuanza kushamiri kuanzia hapo.
AANZA KUIMBISHA
Ilidaiwa kuwa kitendo cha kocha huyo kupata namba ya Wema ilikuwa bahati kama kuokota madafu kwenye miti ya miembe, haraka alianza kutuma maombi ya penzi pasipo kufunguka moja kwa moja kisha badaaye alifunguka kabisa.

“Alianza kwa salamu, akawa anachombezachombeza na maneno ya mitego ambayo mtu mzima ukitumiwa meseji kama hizo unajua kabisa kuna kitu mtu anakitaka kutoka kwako.
“Alipoona Wema haelekei mtegoni, akaamua bora kufunguka laivu, akamtumia meseji zinazoeleza hisia kali ya mapenzi,” kilidai chanzo hicho.

USHAHIDI HADHARANI
Ili kuupata ukweli wa madai hayo, paparazi wa Risasi Jumatano alianza kuchimba undani wa sakata hilo ambapo kwa kutumia njia za ‘kiintelejensia’, alifanikiwa kunasa meseji (SMS) zilizotoka kwa Loga kwenda kwa Wema ambazo zilionesha dhahiri kwamba kocha huyo amedatishwa na staa huyo wa filamu na kuomba hifadhi ya kimalovee.

Meseji hizo zilikuwa zikisisitiza kwamba Loga anamhitaji Wema lakini mtoto wa kike alikuwa mzito kumkubalia mzungu huyo ambaye sasa amesitishiwa ajira yake na uongozi wa Msimbazi, mwishoni mwa wiki iliyopita kutokana na makosa mbalimbali.
WEMA ANASEMAJE
Ili kujiridhisha zaidi, paparazi wetu alimvutia waya Wema na kumuuliza kuhusiana na uhusiano wake na kocha huyo.

Paparazi: Tumesikia Loga anakuimbisha, vipi umemkubalia au vipi?
Wema: Mh! Nani kakwambia?
Paparazi: Nijibu swali langu maana hata ushahidi wa meseji alizokutumia akionesha anakuhitaji, tumeziona na tunazo.

Wema: Kwani kuna tatizo akinihitaji? Si mwanaume, ana haki ya kupenda kama walivyo wengine lakini ishu ni kumkubalia.
Paparazi: Kwa hiyo wewe umemkubalia?
Wema: Aaaa wapi, sipo interested na wazungu hata kidogo by the way mimi nina baby wangu Diamond.

MADAI MENGINE
Wakati huohuo, mtu wa karibu na kocha huyo amepenyeza madai kuwa Loga alipanga kumhamisha Wema na kwenda kuishi naye nje ya nchi lakini haikujulikana mara moja kwamba ni nchi gani achilia mbali kama ilikuwa ni ‘gia’ ya kumpata mwigizaji huyo.

Alipotafutwa Loga ili kuzungumzia madai hayo, hakupatikana mara moja hivyo jitihada zinaendelea, tega sikio kwenye magazeti ya Global.
Kama hiyo haitoshi, pia Loga anadaiwa kutoka na mwigizaji Yvonne-Cherry Ngatwika ‘Monalisa’, madai ambayo mwigizaji huyo ameyakanusha vikali. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate