EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 27, 2014

URAIS 2015 WAIBOMOA BONGO MUVI

KUMEKUCHA! Baada ya kuwepo kwa misuguano ya chini kwa chini kati ya viongozi na wanachama wa kundi la waigizaji wa filamu la Bongo Movie Unity, sasa siri imefichuka kuwa baadhi ya watu wanaotajwa kuwania kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ili wagombee urais mwakani, ndiyo wanaolibomoa kundi hilo kutokana na fedha wanazodaiwa kuzitoa.
Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Baadhi ya waigizaji wenye ushawishi katika kundi hilo waliliambia gazeti hili juzi kwamba, dhambi kubwa inayolitafuna kundi hilo ni kambi za kisiasa zinazoratibiwa na makada wawili wanaoonekana kuwa na ushawishi ndani ya CCM ambao wanatajwa kutaka kumrithi Rais Jakaya Kikwete.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Effects, William J. Mtitu.

“Unajua hapa Bongo Muvi kuna watu wamejikita moja kwa moja katika hizi kambi ambazo kuna waheshimiwa hawa wawili (majina tunayo) ndiyo sababu kuu ya watu wengine kufikia kujiuzulu kwa hoja kuwa wanatumika kwa manufaa ya mtu,” alisema mmoja wao aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Inadaiwa kuwa waheshimiwa hao wawili wamekuwa wakitoa fedha ili kufadhili hafla mbalimbali zinazowahusu waigizaji hao kwa lengo la kutaka kuwatumia muda rasmi wa kampeni utakapowadia.
“Hata hizi hafla zinabuniwa na kuratibiwa na wakubwa hao ambao hutoa fedha za kutosha kwa ajili ya kuzifanikisha. Mfano, kujiuzulu kwa Katibu wa Bongo Muvi, Mtitu (William) kulitokana na kuyeyuka kwa fungu lililotoka kwa… (anataja jina).
“Sasa Mtitu akaona huu ubabaishaji, watu wengine wanufaike wao watumike tu,” alisema mtoa habari huyo.Akizungumzia hitima ya kuwaombea wasanii wa filamu waliotangulia mbele ya haki iliyofanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambako Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa (CCM) Abdallah Bulembo alikuwa mgeni rasmi, mtoa habari hii alisema kuna ‘fungu’ lilitoka.
Katibu wa Bongo Muvi aliyejiuzulu,  Mtitu aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli amechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa wanatumika kisiasa kwa faida ya watu wengine.
“Nimechoka kutumiwa kisiasa bila ridhaa yangu, kisingizio Bongo Muvi, kama kuna mtu au chama kinataka kututumia wasanii au kuitumia Bongo Muvi basi kuwe na uwazi na siyo kumtumia mtu mmoja kwa manufaa yake mwenyewe,” alisema.
Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ alipoulizwa kuhusu ishu hiyo, alikiri kuzisikia siku nyingi, tokea alipoandaa chakula cha usiku kwa wadau wake katika Hoteli ya Great Wall iliyopo Masaki jijini Dar.
“Unajua si kila kitu ni siasa na yote haya yanasemwa kwa kuwa mimi niko kambi ya huyo mheshimiwa. Kwa vile likitokea jambo lolote Bongo Muvi mi huwa naenda kwake kuomba msaada.
“Halafu hakuna mwana Bongo Muvi asiyejua kuwa akaunti yetu ipo tupu, sasa nikienda kuomba fedha naambiwa niko kambi yake, hilo halina ukweli wowote,” alisema Steve anayehisiwa kuwa kambi hiyo.
Akikanusha madai ya kutafuna shilingi milioni 22 kati ya hizo, saba zikiwa ni malipo waliyochukua kwa ushiriki wao katika tamasha moja na zilizobaki zikiwa ni michango kutoka kwa matajiri mbalimbali, Steve alisema:
“Ilitoka shilingi milioni saba kwa ajili ya tamasha, huyo Mtitu ni mmoja wa watu waliokula zile fedha lakini hazungumzi chochote.
Kuhusu kupewa milioni kumi na tano na huyo mheshimiwa ili nifanye dua pale Karimjee Hall si kweli, kuna watu kibao wametoa misaada yao na uzuri zaidi hakuna aliyetoa fedha taslimu zaidi ya kusema mimi nitafanya kitu fulani na wamefanya, mimi namsihi Mtitu awe mkweli tu katika hili asituchonganishe.”
Makada wa CCM wanaotajwa kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho 2015 ni Edward Ngoyai Lowassa, Frederick Tuluway Sumaye, Steven Masatu Wassira, January Yusuf Makamba, Bernard Camillius  Membe, Wiliam Mganga Ngeleja, Samuel John Sitta na hivi karibuni Mizengo Peter Pinda.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate