EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 16, 2014

WASTARA AOLEWA NA MWANAUME ASIYEMJUA


HiSTORIA KWA UFUPI
Wastara alizaliwa mwaka 1983 katika Hospitali ya Turiani iliyopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro akiwa ni mtoto wa tano kati ya saba waliozaliwa katika familia yao.

Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Wastara Juma.
Alisoma Shule ya Msingi Mvomero na baada ya kuhitimu darasa la saba alijiunga na masomo ya sekondari katika Shule ya Sekondari Kibamba Agriculture ambapo alipofika kidato cha pili aliacha shule.

MATUKIO YA UTOTONI
Mwandishi: Unakumbuka utotoni mwako ni matukio gani ya hatari ambayo ulikuwa ukiyafanya?
“Nilikuwa naparamia miti ya miembe, mikorosho kama sina akili nzuri huko nilikuwa nafuata pia ngedere kwani nilikuwa nawapenda sana, nakumbuka nilishawahi kuvunjika miguu yote pia kuvunjika mkono wa kulia kwa kuparamia miti.”
SABABU ZA KUACHA SHULE
Mwandishi: Umesema uliacha shule ukiwa kidato cha pili, nini sababu?
“Niliacha shule baada ya rafiki yangu kuiba hela nyumbani kwao ambapo alikuwa anakuja nazo shuleni tunakula wote chips,
wazazi wake walipogundua wakaja kushtaki shuleni nikawa natafutwa ili nisimamishwe mbele ya wanafunzi wote nieleze na kuchapwa, nilipogundua hivyo sikwenda tena shuleni maana nilikuwa nina aibu sana.”
AUZA MADUKA
Mwandishi: Je, baada ya kuacha shule ulienda wapi?
“Mama yangu alikuwa mfanyabiashara, alikuwa na duka la nguo na lingine la kuuza madini hivyo nilienda kumsaidia kwenye maduka hayo.”
Mwandishi: Ulifanya hizo biashara kwa muda gani?
APATA MCHUMBA
“Nilifanya kwa muda wa miezi mitatu nikapatiwa mchumba nikaolewa japokuwa nilikuwa simpendi.’’
Mwandishi: Sasa ilikuwaje ukaolewa na mwanaume usiyempenda?
“Nakumbuka nilikuwa na miaka kumi na sita na sikuwahi hata kumuona wala kuzungumza na huyo mwanaume kabla ya ndoa,
alienda moja kwa moja kwa mama yangu wakakubaliana na wakati huo wazazi wakishaamua huwezi kupinga ,hivyo nililazimika kuolewa hivyohivyo kwani mama yangu alikuwa akiogopa aibu ya kuzalia nyumbani kwa vile kwa mila zetu sisi Waarabu ukiwa na miaka hiyo msichana unaonekana ni mkubwa na unastahili kuolewa.”(Wastara baba yake alikuwa Mwaarabu.)
MUME AMZIDI UMRI
Mwandishi: Huyo mwanaume wako mlikuwa mnalingana naye umri au alikuzidi?
“Mwanaume alikuwa mkubwa sana kwangu hivyo kutokana na udogo niliokuwa nao sikuwa najua nini maana ya ndoa kitu nilichokuwa najua kufanya ni usafi tu, suala la mapenzi ndiyo lilikuwa ni shughuli haswa kwani nilikuwa sijui.”
TENDO LA NDOA
Mwandishi: Sasa mumeo alipokuwa akitaka haki ya ndoa ulikuwa unafanyaje?
“Ilikuwa ni kama tunapigana wakati huo ukifika na nilipopata ujauzito sikutaka hata aniguse hivyo mpaka mtoto anazaliwa sikushiriki tena tendo la ndoa na huyo mwanaume kwani nilikuwa namwambia kwamba naumia.”
MAISHA MAGUMU
Mwandishi: Vipi sasa maisha ya ndoa yalikuwaje?
“Maisha yalikuwa magumu sana kwani mwanaume aliyenioa hakuwa na kazi ya aina yoyote na mama hakuligundua hilo, baada ya kunioa alikuwa anaenda kushinda nyumbani kwao ndiyo ndugu zake wakawa wanatupatia chakula na kutulipia kodi.
“Baada ya kuwa na ujauzito wazazi wake walinichukua, nikaenda kukaa nao Zanzibar lakini nikawa nateseka sana ambapo mama yangu aligundua na kusema nije Dar kwani anataka kuniona na kipindi hicho alikuwa anaumwa, nilikuja kwa mama aliponiona alihuzunika sana kwani nilikuwa nimedhoofika. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate