EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 10, 2014

JOHN BOCCO NJE MECHI YA NGAO NA YANGA JUMAPILI, AZAM FC WAINGIA KAMBINI LEO CHAMAZI

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
MSHAMBULIAJI wa Azam FC, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ anatakiwa kuwa nje kwa wiki mbili au tatu kuanzia leo kutokana na matatizo ya misuli- maana yake hatacheza mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Meneja wa Azam FC, Jemadari Said Kazumari ameiambia BIN ZUBEIRY leo asubuhi kwamba, Bocco aliyeumia kwenye michuano ya Kombe la Kagame mwezi uliopita mjini Kigali, Rwanda baada ya kufanyiwa vipimo, ametakiwa kupumzika ili kupona vizuri.
Atakosekana: John Bocco 'Adebayor' kushoto atakosekana katika mchezo wa Ngao ya Jamii Jumapili 

MABINGWA WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:

Mwaka  Mshindi Matokeo     
2001: Yanga SC  2-1 Simba SC
2009: Mtibwa Sugar  1-0 Yanga SC
2010: Yanga SC  0-0 Simba (3-1penalti)
2011: Simba SC   2-0 Yanga SC
2012: Simba SC  3-2 Azam FC
2013: Yanga SC 1-0 Azam FC

“Tuna majeruhi wawili ambao hawatakuwepo kwenye programu ya mchezo wa Ngao ya Jamii, ambao ni beki Waziri Salum na Nahodha wetu, John Bocco,”amesema mshambuliaji huyo wa zamani wa Kariakoo United ya Lindi.
Bocco aliuamia katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la Kagame dhidi ya El Merreikh ya Sudan ambao Azam FC ilitolewa kwa penalti baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 90.
Jemadari amesema kwamba, Azam FC itaingia kambini jioni ya leo katika hosteli za Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam kuelekea mchezo huo wa Ngao ya Jamii.
Wachezaji wengine wote wapo fiti na wamekuwa wakiendelea na mazoezi Uwanja wa Azam Complex na wanatarajiwa kuingia kambini leo.     
Mabingwa hao wa Tanzania Bara wanaonolewa na kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog watamenyana na washindi wa pili, Yanga SC walio chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo Jumapili Uwanja wa Taifa. 
Yanga SC nayo inatarajiwa kuingia kambini leo kwa ajili ya mchezo huo, ambao unatarajiwa kuwa marudio ya mchezo wa Ngao ya Jamii mwaka jana timu zilipokutana tena Uwanja wa Taifa.
Hii itakuwa mara ya tatu mfululizo, Azam FC kucheza mechi ya Ngao ya Jamii na mara zote ikifungwa kwanza na Simba SC na baadaye na Yanga SC- lakini safari hii kocha Omog anataka kupindua matokeo hayo. 
Yanga SC ndio washindi mara nyingi zaidi wa Ngao, mara ya kwanza wakitwaa mwaka 2001 walipoifunga mabao 2-1 Simba SC, enzi hizo Ligi Kuu inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager. 
Baada ya hapo, haikuchezwa tena mechi ya Ngao hadi mwaka 2009 wakati Mtibwa Sugar ilipoilaza 1-0 Yanga SC.
Mwaka 2010 Yanga walirejesha Ngao kwenye himaya yao, baada ya kuwachapa tena wapinzani wao wa jadi, Simba kwa penalti 3-1 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90.
Simba SC walitwaa mara mbili mfululizo Ngao na kufikia rekodi ya watani, kwanza 2011 walipoifunga 2-0 Yanga na 2012 walipotoka nyuma kwa 2-0 na kuilaza Azam 3-2.
Mwaka jana, Yanga SC ikaweka rekodi ya kuwa timu iliyotwaa mara nyingi zaidi Ngao ya Jamii, baada ya kuilaza 1-0 Azam FC, bao pekee la kiungo Salum Abdul Telela ‘Master’.
Na mwaka huu, tena Azam FC na Yanga SC zinarudia mechi ya Ngao ya msimu uliopita, zitakapokutana tena Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Jumapili patachimbika: Yanga SC nayo inatarajiwa kuingia kambini leo

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate