BONDIA
Floyd Mayweather ametuhumiwa kumtesa, kutishia kumuua na kumuibia
mpenzi wake wa zamani, Shantel Jackson kwa mujibu wa kesi iliyofunguliwa
mahakamani.
Bondia
huyo bingwa wa uzito wa madaraja matano tofauti ambaye hajawahi
kupoteza pambano, anatarajiwa kupanda ulingoni wikiendi hii kuzipiga
na Marcos Maidana akiwa anakabiliwa na hatari ya kutupwa jela baada ya
mashitaka yaliyowasilishwa na mpenzi wake huyo wa zamani.
Mwanamitindo
huyo mwenye umri wa miaka 29 alikuwa akizungumza huku akilia na kutaja
jina Mayweather wiki iliyopita katika Mkutano na Waandishi wa Habari,
akilalamika kupigwa na bondia huyo, na kubandika picha zake za faragha
za vipimo vya ultrasound kwenye mitandao ya kijamii na kutangaza kwamba
wameachana kwa sababu ametoa mimba ya watoto wao wawili pacha.
Lakini
katika jalada lililofunguliwa mahakamani kilichosheheni katika uhusiano
wa bondia huyo na mlimbwende huyo kwa miaka minane ni machungu tu.
Shantel anasema aliteseka mno mikononi mwa Mayweather, mwenye umri wa miaka 37, aliyekuwa akimpiga, hadi akamtegua bega, na wakati fulani alimtishia kumpiga bastola.
Pia
alimuweka ‘jela’ nyumbani wake Las Vegas, na kutishia kuchapisha picha
za uchi alizompiga mlimbwende huyo kwa siri wakiwa wamelala pamoja
kitandani na kumuibia maelfu ya dola alizopokea kwa ajili yake.
No comments:
Post a Comment