EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 24, 2014

MAMA SALMA KIKWETE AHUTUBIA MKUTANO WA ELIMU NA AFYA KWA VIJANA DUNIANI ULIOANDALIWA NA TAASISI YA MAMA SARAH BROWN

Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mama Sarah Brown, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza na Mwenyekiti Mtendaji wa Global Business Coalition for Education muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa ‘Getting Serious About Results: The Grand Convergence of Education and Health” ulioandaliwa na Taasisi ya Mama Sarah Brown kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa. Mkutano huo umefanyika huko New York tarehe 23.9.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza Bwana Gordon Brown kabla ya kuanza mkutano uliozungumzia mambo ya elimu na afya kwa vijana duniani tarehe 23.9.2014.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akibadilishana mawazo na Dkt. Sarah Maongezi, Mkurugenzi wa Idara ya Afya katika Taasisi ya WAMA muda mfupi kabla kuanza mkutano huo.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa :’Getting serious about Results: The Grand Convergence of Education and Health’ ambao ulizungumzia mambo ya elimu na afya kwa vijana hapa duniani. Mkutano huo ilifanyika huko New York tarehe 23.9.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza wakati wa mkutano uliojadili masuala ya elimu na afya kwa vijana duniani huku viongozi wengine mashuhuri wakisubiri kuzungumza. Kushoto kwa Mama Salma ni Dkt. Rajiv Shah, Afisa Mtendaji kutoka USAID, akifuatiwa na Bwana Mark Dybul, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Fund to fight AIDS na wa mwisho ni Bwana V. Shanker, Afisa Mtendaji Mkuu wa Afrika, Mashariki ya Kati, Ulaya na Marekani kutoka Standard Chartered.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Dkt. Andy Shih, Makamu wa Rais Mwandamizi anayeshughulikia masuala ya sayansi kutoka katika Shirika la ‘Autism Speaks” (masuala ya usonji) wakati mgeni huyo alipomtembelea Mama Salma kwenye hotelin aliyofikia huko New York, nchini Marekani tarehe 23.9.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifanya mazungumzo na Dkt. Andy Shih.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akimkabidhi Dkt. Andy Shih jarida la WAMA mara baada ya kufanya mazungumzo ya ushirikiano baina ya Taasisi zao.

Baadhi ya Washirika wakiwa kwenye Mkutano huo.PICHA NA JOHN LUKUWI

Na Anna Nkinda – Maelezo, New York

Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika ikiwemo Tanzania zinakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa fursa za elimu kwa watoto wenye umri wa kwenda shule, ubora na usahihi wa elimu, masuala mtambuka kama Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ugonjwa wa Ukimwi.

Changamoto nyingine ni upatikanaji wa huduma rafiki za afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana na udahili mchache wa wasichana katika masomo ya sayansi.

Hayo yamesemwa leo na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea katika majadiliano ya elimu na afya kwa vijana yaliyoandaliwa na Umoja wa kimataifa wa Taasisi za Biashara kwa ajili ya Elimu na kufanyika katika Hoteli ya Reed Smith mjini New York.

Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kwa upande wa sekta ya afya ina changamoto ambazo zina uhusiano mkubwa na elimu na kutoa mfano wa vifo vya akina mama vinavyotokana na matatizo ya uzazi, vifo vya watoto, ndoa za utotoni, mimba katika umri mdogo, utapiamlo na upungufu wa nguvu kazi.

Alisema Serikali na wananchi wa Tanzania walitambua mapema umuhimu wa kuwekeza kikamilifu katika elimu kama msingi wa kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia hususan lengo la pili linalohusu Elimu kwa wote.

“Serikali yetu ilianzisha  Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi  na mpango wa maendeleo ya Elimu ya Sekondari. Mipango yote hii miwili ina malengo ya kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa watoto wote walio katika umri wa kwenda shule, kuongeza ubora na usahihi wa elimu.

Kuboresha urari wa kijinsi na walimu na ufundishaji, kuongeza tija katika uongozi na utawala bora, kurasimisha masuala mtambuka kama vile UKIMWI, Elimu ya Stadi za Maisha,  elimu ya mazingira na jinsia”, alisema Mama Kikwete.

Alisema mpango wa  matokeo makubwa sasa katika elimu unalenga kujenga uwezo wa walimu kwa kutoa mafunzo ya pahala pa kazi, kusaidia watoto wasiofanya vizuri kwa kuandaa vitendea kazi mahususi vinavyozingatia umri na mahitaji, kuboresha miundo mbinu, kwa kujenga madarasa, maabara na nyumba za walimu.

Kuboresha vifaa vya ufundishaji kama vile madawati, vifaa vya maabara, kemikali na  kutoa vitu vya kuongeza motisha kwa walimu.

Mwenyekiti huyo wa WAMA alimalizia kwa kusema elimu bora itapatikana ikiwa afya za vijana zitaboreshwa na kuwa na mikakati ambayo inatambua uhusiano mkubwa wa masuala hayo kwani bila ya elimu timilifu ni vigumu kufikia malengo yaliyopo.

Kwa upande wake Mke wa waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Mama Sara Brown ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa Umoja wa kimataifa wa Taasisi za Biashara alimpongeza Mama Kikwete kwa kazi anayoifanya ya kutoa elimu kwa watoto wa kike ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi na kuboresha afya ya mama na mtoto.

“Nilitembelea nchini Tanzania mwaka 2007 na kujionea kazi anayoifanya Mama Kikwete nampongeza kwa hili. Ni jukumu letu kuhakikisha kuwa watoto wanapata elimu na afya bora ili waweze kuwa na maisha bora hapo baadaye”, alisema Mama Brown.

Nao wachangia mada katika mjadala huo walisema ni muhimu watoto wa kike wakapata elimu sawa na watoto wa kiume kwani wakipata elimu unyanyasaji wa kijinsia ambao unazidi kuongezeka dhidi yao utapungua na kutakuwa na usawa katika mambo mengi.

Walisema, “Wafadhili mbalimbali wamekuwa wakiwekeza katika afya na elimu hasa kwa watoto wa kike ili kuwajengea mazingira mazuri ya kusoma ikiwa ni pamoja na kuwajengea madarasa na vyoo. Ni vyema vijana wakapata elimu na afya bora ili waweze kujihusisha na shughuli za maendeleo”.


Mkutano huo ni moja ya maandalizi ya Mkutano wa  69 wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa (UN) unaotarajiwa kufunguliwa tarehe 24/9/2014    mjini humo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate