EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 9, 2014

NI UGAIDI ASILIMIA MIA MOJA

Stori: Mwandishi Wetu Dar na Jaed Kimaro, Bukombe TUKIO la kutisha la kushambuliwa kwa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, ambapo askari wawili walipoteza maisha na silaha kadhaa kuporwa, limeelezwa kuwa kwa kiwango cha asilimia mia moja, jambo hilo ni ugaidi wa dhahiri.

Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, kilichoshambuliwa kwa mabomu.
Jumamosi iliyopita, majira ya saa sita  usiku, watu wasiojulikana, walikivamia kituo hicho kwa mabomu na silaha zingine nzito zinazosadikika kuwa ni za kivita, wakafanya mauaji na kujeruhi watu wengine kadhaa kabla ya kupora bunduki na silaha zilizohifadhiwa kituoni hapo.
Damu ya maaskari iliyomwagika kwenye shambulia hilo la kigaidi.
“Huu siyo ujambazi wa kawaida uliozoeleka, ni kweli kuna wakati matukio yanatokea kuwa ya kutisha sana, lakini aina hii ya mashambulio siyo kawaida, tena kituo cha polisi? Hawa watu ni dhahiri walihitaji kupata silaha tu, sasa sijui zinakwenda kutumika wapi na tuna shaka kama hawa si Watanzania,” alisema Zebareta Shayo, mkazi wa Sinza, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, (IGP) Ernest Mangu (mwenye suti nyeupe) akiwa eneo la Tukio.
Waziri Salum, mwanasheria na wakili wa kujitegemea  alisema tukio hilo ni vizuri kama lingeifanya serikali kutazama upya mipaka yetu kwani kuna kila dalili kuna baadhi ya wageni wanaingia kirahisi na kufanya unyama huo bila kujulikana.
Mfano wa silaha zilizoibwa na majambazi.
Askari waliopoteza maisha katika shambulio hilo wametajwa kuwa ni Uria Mwandiga mwenye namba WP 7106 na Dustan Kimati mwenye namba G 615 PC. Majeruhi ni David Ngupama Mwalugelwa (44) namba E 5831 APL na Mohamed Hassan Kilomo (25) namba H 627 PC.
Mkurugenzi wa Mashtaka (DCI) Isaya Mngulu.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, (IGP) Ernest Mangu na Mkurugenzi wa Mashtaka (DCI) Isaya Mngulu kuwasili tangu juzi mkoani hapa, askari zaidi kutoka Mikoa ya Tabora, Shinganya na Mwanza wanaendelea kuwasili.
Msako mkali unaendeshwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kuweza kuwabaini wahalifu hao huku Kamanda wa Mkoa wa Geita, Joseph Konyo akiwataka wananchi kutoa taarifa mara moja watakapotilia shaka nyendo za mtu yeyote ili kurahisisha zoezi hilo alilodai lazima lifanikiwe.
Juni 10, mwaka huu, tukio kama hilo likihusisha majambazi waliokisiwa kuwa sita, wakiwa na pikipiki tatu walivamia Kituo Kidogo cha Polisi Mkamba kilichopo Kimanzichana, Wilaya ya Mkuranga, Pwani na kuua askari mmoja na mgambo na kujeruhi mgambo mwingine kisha kupora bunduki tano na risasi 60.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate