EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 3, 2014

PREMIER LEAGUE YASHIKA USUKUKANI WA FEDHA NA BOLI

REKODI zilizopatikana kutokana na usajili wa ligi mbalimbali za Ulaya umekuwa ukipishana lakini kwa idadi ndogo sana na hii inatokana na vyombo vya habari au wale wanaozitoa kwao wanavyowahabarisha.
Lakini haziondoi suala la kuonyesha hali halisi, mfano BBC inaamini England kwa usajili wametumia kitita cha pauni milioni 835 na Dailymail wanaamini ni pauni milioni 857.7, hii inaonyesha hakuna tofauti kubwa sana.
Kikubwa cha kujadili ni namna ambavyo England imeingia kwenye njia nyingine kabisa kutokana na timu zake kutumia idadi kubwa ya fedha katika usajili hadi kufikia kuzitupa mbali ligi za Hispania ‘La Liga’ na Italia ‘Serie A’ ambazo zimekuwa ziking’ara kutokana na kutumia fedha nyingi katika usajili.
 Katika kipindi cha misimu miwili, klabu za England, Tottenham Hotspur na Liverpool ziliwauza Gareth Bale na Luiz Suarez kwa vigogo wa Hispania, Real Madrid na Barcelona.
Hadi sasa biashara ya Bale ndiyo uhamisho ghali zaidi kwa kuwa aliuzwa kwa pauni milioni 85, Suarez naye ni kati ya uhamisho ghali kwa kuwa ni pauni milioni 75.
Msimu uliopita wa 2013-14, klabu za England zilitumia pauni milioni 760, lakini msimu huu gharama zimepanda maradufu hadi kufikia pauni milioni 857 ambayo imevunja rekodi ya misimu yote tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo.
Misimu miwili sasa, Premier League imebadilika, badala ya kuuza wachezaji tu Hispania imekuwa ikinunua tena kutoka La Liga na kwa bei ghali.
Arsenal imefanya hivyo misimu miwili mfululizo ikianza kumnunua Mesut Ozil kutoka Real Madrid na msimu huu ikamnunua Alexis Sanchez kutoka Barcelona wakati Man United ilimtwaa Ander Herrera kutoka Athletic Bilbao, kisha ikamnasa Angel Di Maria kutoka Real.
Lakini hiyo haitoshi, Premier League sasa ndiyo ligi ghali zaidi kutokana na kutumia fedha nyingi za usajili mara mbili ya La Liga ambayo inashika nafasi ya pili.
Usajili wa La Liga ambayo inawajumuisha vigogo Real Madrid na Barcelona, umegharimu zaidi ya pauni milioni 434 wakati Serie A ina pauni milioni 272 zilizotumika kwa ajili ya manunuzi ya uhamisho wa wachezaji.
 Bundesliga yenyewe imetumia pauni milioni 261 wakati Ufaransa kupitia klabu zao mbili kubwa, angalau walijisukuma na kufikia hadi pauni milioni 112.
Hii utaona kiasi gani Premier League imegeuka kuwa ligi maarufu lakini pia inayotumia fedha nyingi na zaidi klabu tano za juu ndizo zimetumia fedha nyingi.
Manchester United ndiyo imeongoza kwa kumwaga pauni milioni 153.1, Liverpool inafuatia kwa kutumia pauni milioni 116.8, Chelsea (pauni milioni 87.7), Arsenal (pauni milioni 78.2), Southampton (pauni milioni 57.9) na Man City (pauni milioni 54.5).
Mara chache sana usajili kushuka, lakini kutokana na fedha hizo za kiwango cha juu zinazotumika, Premier League itazidi kuwa ligi maarufu zaidi duniani kwa asilimia 63 badala ya 58 ilizokuwanazo awali.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate