EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, October 11, 2014

NDOA, HAIPO: GARDNER AMSALITI JIDE?

Stori: Waandishi Wetu
LICHA ya kutothibitishwa juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa ndoa yake na mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Jide’, mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash ‘Kepteini’ amenaswa na kabinti akiwa kwenye pozi tata za kimahaba hivyo baadhi ya watu kuhoji anasaliti ndoa? Risasi Jumamosi lilifuatilia hatua kwa hatua.
Mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash ‘Kepteini’ akiwa katika pozi la kimahaba na binti huyo.

OFM KAZINI, TUJIUNGE COCO
Tukio hilo lililojaa viulizo kibao bila majibu, lilifuatiliwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers hatua kwa hatua ambapo lilijiri Jumatano iliyopita kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay jijini Dar kulipokuwa tamasha la wazi la kuibua vipaji vya wasaniii mbalimbali.
Awali, vijana mbalimbali walipanda katika onesho hilo na kuonesha vipaji huku binti huyo jina halikupatikana mara moja, alionekana na rafiki yake ambapo wote walikuwa ni washiriki katika onesho hilo.
GARDNER AMUIBUKIA
Wakati mtangazaji huyo akiwa katika mizunguko yake ufukweni hapo, ghafla jicho lake lilitua kwa binti huyo na kumfuata kisha kumnong’oneza kitu (haikujulikana alimwambia nini).
Gardner na mrembo wakiwa pamoja.
Huku wapenda ‘ubuyu’ wakimfuatilia kwa ukaribu, ndani ya muda mfupi, binti huyo alionekana kuelewa mazungumzo ya Gardner kwa kutingisha kichwa kuashiria ujumbe umemfika vizuri.
WACHEPUKA
Baada ya Gardner na mrembo huyo kusikilizana, wanahabari wetu waliwashuhudia wawili hao wakishikana mikono na kuondoka eneo hilo kwenda kununua vinywaji kisha wakajitenga sehemu wakinywa vinyaji huku Gadner akiwa amemkubatia kwa nyumba mtoto huyo mzuri na mwembamba kama Jide.
WAHAMA PAMOJA
Mashushushu wetu waliwashuhudia wawili hao wakipiga misele pamoja katika maeneo mbalimbali ya ufukwe huo huku mtoto wa kike akiachia tabasamu zito huku jamaa akiwa amemzungushia mkono kiunoni, wakizungumza maneno yalioonesha kuwa wapo kwenye urafiki mzuri.
Akimnong'oneza jambo.
WAPENDA UBUYU SASA!
Wakati Gardner akiwa bize akifanya yake huku akiwa ameongeza umakini, baadhi ya watu ambao ni wepesi kufuatilia mambo ya watu (wapenda ubuyu/umbeya), walianza kuibua minong’ono kwamba kulikoni mtangazaji huyo ambaye amekuwa mzito kutamka kwamba hawako pamoja na Jide, ajiachie kiasi hicho na mrembo huyo.
“Jamani huyu si ni Gardner? Vipi tena mbona anaambatanaambatana na huyu mtoto? Kwa vyovyote ni wazi kabisa kuna kitu kinaendelea kati yao, maana muda wote wapo beneti.“Duh! Sijui Jide akiwaona katika pozi kama hizi atajisikiaje kama kweli hawajaachana,” alisikika mmoja wa wapenda ubuyu.
Baada ya wanahabari wetu kupata walakini na kutaka kuthibitisha hilo, walianza kumfuatilia hatua kwa hatua mpaka waone mwisho wa mchezo utakavyokuwa baada ya kuona dalili hizo, kwa kuwa kadiri muda ulivyozidi kwenda ndivyo mambo yalipozidi kujianika hadharani huku wakijitahidi kukwepa kamera lakini waligonga mwamba.
WABADILISHANA VINYWAJI
Kuonesha kwamba urafiki wao si wakubahatisha, kuna wakati Gardner na mrembo huyo walibadilishana vinywaji jambo ambalo lilifanyika chini ya wapambe wa Gardner ambao walikuwa wakimzingira ili mapaparazi wasiweze kupata picha kwa urahisi.
Akizidi kuwanaye bega kwa bega.
Hata hivyo, mapaparazi wetu walifanikiwa kuzipata picha hizo kwa kutumia mbinu za kiintelijensia kama zinavyoonekana katika ukurasa wa mbele.
WATOWEKA
Wakati mapaparazi wetu wakiendelea kuwafuatilia, ghafla Gardner alitoweka eneo hilo lililokuwa na watu wengi kisha baada ya muda mfupi binti naye akatokomea kusikojulikana.
JIDE AAMBIWA AJIONGEZE!
Kwa mujibu wa mashuhuda wa mpango huo, mke wa Gardner, Jide anapaswa kujiongeza ili kulinda mali yake la sivyo wasichana wa mjini watamzidi kete.
BOFYA HAPA KUMSIKIA GARDNER
Alipotafutwa Gander kupitia simu ya mkononi juzi, Alhamisi ili kuulizwa kuhusu mrembo huyo, mtangazaji huyo alikiri kuwepo Coco kwenye shoo hiyo lakini hakumbuki ni binti gani amuone vizuri kwenye picha.
“Ebwana ni kweli nilialikwa kwenye hiyo shoo so nilikuwepo lakini kuhusu kabinti siwezi kukumbuka labda nione picha.
“Kweli nilipiga picha na mabinti wengi so sijui ni yupi, unajua nature (asili) ya kazi yangu (utangazaji) nakutana na watu wengi na wanapenda kupiga picha na mimi,” alisema Gardner.
Waandishi: Mayasa Mariwata, Denis Mtima na Shani Ramadhani
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate