WIKI iliyopita vyombo vya habari likiwemo gazeti la hili viliandika
habari ya Jiji la Dar es Salaam kutikiswa na wimbi la utekaji watoto
ambao wamekuwa wakichukuliwa katika mazingira ya kutatanisha huku
wengine wakiuawa na kunyofolewa sehemu zao nyeti.
Msingi wa habari hiyo ulikuwa ni kutoa tahadhari kwa wazazi na vyombo vya dola kuchukua hatua ya kujilinda na uhalifu huo mpya.
Lakini pamoja na wema wa habari hizo, Jeshi la Polisi Mkoa wa
Kipolisi wa Kinondoni kupitia kwa kamanda wake Camilius Wambura,
waliziita habari hizo kuwa ni za kizushi huku wakionya kuwachukulia
hatua wanaoeneza uzushi huo.
Tafakuri ya kawaida kuhusu onyo la uzushi huo iliwahusu waandishi wa
habari wakiwemo wa gazeti la hili. Kusudio la polisi kwenye tamko hilo
linaweza kuwa na tafsiri nyingi lakini moja kati ya hizo ni kuwaambia
wananchi wawapuuze waandishi.
Wakati sura ya jeshi la polisi hasa Kinondoni ikiwa na picha hiyo ya
uzushi wa waandishi, tukio la mwanafunzi wa darasa la kwanza Shule ya
Msingi Msingwa iliyopo Kimara-Temboni, wilayani Kinondoni jijini Dar
eneo la kazi la Kamanda Wambura, alitekwa mwishoni mwa wiki iliyopita,
akauawa kisha kunyofolewa sehemu zake za siri.
Katika mazingira hayo swali la mzushi ni nani kati ya waandishi wa
habari na polisi limepata jibu. Hata hivyo, haliwezi kuwa jambo la
kufurahia kupata ushindi wa uzushi bila kujiuliza kasumba ya polisi
kuwaita waandishi wazushi kaianzisha nani na kwa manufaa gani.
Vita ya kugombea fito kwenye ujenzi wa nyumba moja kaibuni nani?
Maana ushirikiano kati ya jeshi la polisi na waandishi unazidi kuzorota
kila siku, hakuna anayeona hatari inayolikabili taifa siku za usoni kama
hali hii itaendelea kuota mizizi.
Ni juzi tu waandishi wa habari wamepigwa na polisi wakati
wakitekeleza majukumu yao, mzozo umepoa kimtindo lakini moshi ungali
ukifuka.Hata kama jeshi la polisi halitaki kushaurika kwa dalili
zinavyojionesha hivi sasa kwa waandishi kuhojiwa, kutishwa na
kusukwasukwa kwa baadhi ya habari kutafsiriwa vibaya na jeshi hili;
bado wanahabari wana jukumu la kuitumia jamii bila hofu.
Ushauri wangu kwa jeshi la polisi lenye sura hii ni kwamba, haliwezi
kupata mafanikio ya kweli ya kuwalinda raia na mali zao bila kuwa na
ushirikiano wa kutosha na vyombo vya habari. Hilo naweza kuliapia!
Taarifa za matukio zimekuwa zikiripotiwa kwa wingi zaidi kwenye vyombo
vya habari kuliko polisi ambako kumejaa lawama za “ukipiga simu
hawapokei” na woga wa watoa habari kugeukwa pindi wafikishapo ripoti zao
polisi. Anayebisha katika hili shauri yake.
Wahariri ni mashahidi wa hiki nisemacho, wao wamekuwa watu wa kwanza
kupewa taarifa za ajali licha ya kuwa siyo trafiki, huambiwa habari za
wauza madawa ya kulevya ingawa wao siyo polisi, watu kujihusisha na
ujambazi hata kama wao siyo askari kanzu! Yote hii ni ushahidi wa
kuaminika kwao.
Sasa ukiona jeshi la polisi halitaki ushirika na waandishi wenye
wingi wa taarifa za matukio kama nilivyosema ni dhahiri kwamba hawataki
pia kupata ripoti zitakazowasaidia kufanikisha ulinzi wao kwa jamii.
Mwenye hasara ni nani, ni waandishi au polisi wenye jukumu la
ulinzi? Vyombo vya habari viliandika utekaji watoto vikamaliza kazi
yake, Wambura alipokuja na kauli ya uzushi leo yeye ndiye anayenyooshewa
vidole, siyo waandishi. Ningekuwa kijana ningesema Wambura anatakiwa
kujiongeza.
Nachochea tu!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe
No comments:
Post a Comment