EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, October 7, 2014

WAZUIA MAZISHI YA BIBI YAO


Stori: Victor Bariety, Sengerema WAJUKUU wa marehemu Sabina Ngalu (77) wameibua kutuko makaburini kufuatia kuzama ndani ya kaburi la marehemu huyo na kugoma kutoka wakidai kwamba mpaka walipwe shilingi laki moja (100,000), Uwazi lina mkanda mzima.
Wajukuu wa bibi huyo wakiwa kaburini.
Tukio hilo la aina yake lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita katika Kitongoji cha Nyamwanza Kata ya Sima wilayani Sengerema mkoani Mwanza muda mfupi baada ya mwili wa marehemu kuwasili eneo la mazishi kwenye shamba lake ukitokea Kanisa la Roman Katoliki Parokia ya Yesu Kristo Mfalme la mjini Sengerema.

Sababu za wajukuu hao kung’ang’ania ndani ya kaburi hilo walitaka wapewe ng’ombe mmoja au pesa hizo taslimu kwa mjibu wa mila na desturi za kabila la Kisukuma jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya wanandugu waliodai mila hizo zilipitwa na wakati.
Kufuatia wajukuu hao kuendelea kugomea ndani ya kaburi, kaka wa marehemu, Enosi Ngalu alikwenda  kukata fimbo na kuwashukia kisha kuwacharaza viboko wote huku nao wakisisitiza hawatoki mpamka ‘kieleweke’.
Padri na wananchi wakiwa makaburini.
Baadhi ya wajukuu walioonja joto la jiwe ya kuchapwa viboko ni Andrea Mabula, Sabina Bukuru, Johari Bukuru, Asha Bukuru, Faida Bukuru, Yuves Petro, Semeni na kiongozi wao, Enos Ntilaga.
Kitendo cha wajukuu hao  kuendelea kugoma kutoka kaburini kilimchefua Padri Nicodemus Mayalla ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Yesu Kristo Mfalme, Sengerema ambaye aliamua kuondoka eneo la maziko huku akiwataarifu polisi kuhusiana na vurugu hizo.
Kufuatia hali hiyo, mmoja wa waombolezaji alizama mfukoni na kutoa kiasi hicho cha pesa na kuwapa ndipo walipokubali kutoka dani ya kaburi hilo ili mazishi yaendelee.
Ili kuonesha alikerwa na kitendo hicho, Padri Mayalla ambaye kwa wakati huo alikuwa amewekwa chini na baadhi ya ndugu wakimsihi kutosusia mazishi hayo, aligoma kurejea kaburini kuongoza ibada ya mazishi.
Jeneza lenye mwili wa bibi huyo likishushwa kaburini.
Baada ya vuta nikuvute, hatimaye Padri Mayalla alikubali kuendelea na ibada lakini aliwataka wajukuu hao kurudisha pesa waliyochukua na kuwaomba radhi wana mtaa huo na ndipo yeye aweze kurudi kaburini.
Wajukuu hao waliitwa mbele ya padri huyo  na mbele ya wana mtaa, wakaomba samahani ikiwa ni pamoja na kurudisha kitita hicho cha pesa paroko huyo naye akarejea kaburini na kuongoza ibada ya mazishi.
Hata hivyo, wakati ibada ikiendelea  polisi zaidi ya wanne kutoka Kituo cha Polisi Sengerema wakiwa na bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) na mabomu ya machozi walifika eneo la tukio  ili kuhakikisha amani na utulivu vinatawala.
Polisi akiwa eneo la tukio.
Cha kushangaza, saa baada ya kutoka makaburini, wajukuu hao waliwahi nyumbani kwa marehemu, Mtaa wa Mlimani, Kata ya Nyatukala wilayani Sengerema na kuanzisha timbwili jingine kwa kuficha chakula na vyombo vya kupakulia wakidai warudishiwe pesa yao waliyoirejesha makaburini kwa shinikizo la baba paroko.
Baada ya timbwili hilo kukolea, mmoja wa wafiwa alizama mfukoni na kutoa shilingi laki moja na kuwakabidhi wajukuu hao ambao walirudisha chakula jikoni na taratibu za waombolezaji kupata chakula ziliendelea.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate