EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 6, 2014

AMA KWELI MCHEPUKO SIYO DILI


Dustan Shekidele, Morogoro
MH! ‘Haga gangi’ (haya mengine)!  Simon Manase (22) ambaye ni dereva wa bodaboda, mkazi wa Kijiji cha Nguyami, wilayani Gairo mkoani hapa amecharangwa mapanga mwilini na kukatwa mkono wa kulia na mtu aliyetajwa kwa jina la Frank akidai kumfumania na mkewe vichakani.
Kijana Simon Manase (22) aliyecharangwa mapanga baada ya kufumaniwa na mke wa mtu vichakani.
Ishu hiyo inadaiwa kujiri usiku mnene wa Oktoba 31, mwaka huu kwenye Kijiji cha Nembo mpakani mwa Gairo na Kilosa katika muziki wa mitaani maarufu kwa jina la ‘kigodoro’.Mwandishi wetu alipiga gia hadi kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kuzungumza na mashuhuda, viongozi wa kata, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Berega na Mkuu wa Kituo cha Polisi Dumila.

“Siku ya tukio tulikuwa kwenye shereha ya mwenzetu, mwanae amevunja ungo hivyo nyumbani kwake aliweka muziki wa kigodoro, cha ajabu ilipofika saa sita usiku DJ wa muziki, Alex Munga alitutangazia kwamba kuna watu wanapigana mapanga baada ya kufumaniana kwenye kichaka.
Simon Manase akiuguza majeraha katika Hospitalini ya Berega mkoani Morogoro.
“Tulikimbilia kule. Kufika tukamkuta Frank akimcharanga mapanga Simon akidai amemfumania na mkewe ,”alisema shuhuda aliyejitambulisha kwa jina la Elizabeth Joseph.Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Nembo, Musa Bruno alikiri kutokea kwa tukio hilo kwenye kijiji chake.
“Ni kweli, siku hiyo, mimi na msaidizi wangu, Daudi Kisonela na mgambo wa kijiji tulifika eneo la tukio na kushuhudia Simon akivuja damu mwilini huku mkono wake wa kulia ukining’inia nusu hadi mfupa wa ndani ukionekana baada ya kupigwa mapanga na Frank akidai kamfumania na mkewe,” alisema mtendaji huyo.
Akaendelea: “Tuliwaweka kikao, tulimhoji mke akasema mumewe alikurupuka kumcharanga mapanga mtuhumiwa kwani si kweli.
Majeraha ya usoni ya panga alilopigwa Simon Manase.
“Kwa kauli ya mama huyo tulimtia hatiani Frank, tukamkamata na kumfikisha Kituo cha Polisi Dumila, cha ajabu wakati sisi tukitafuta usafiri, huku nyuma mtendaji wa kata alimuachia huru Frank huku akitukabidhi panga lenye damu kama ushahidi.”Akizungumza kwa tabu na mwandishi wetu katika wodi ya wanaume Hospital ya Misheni ya Berega, Gairo, Simon alisema:
”Siku ya tukio nilifika kwenye kigodoro kwa lengo la kusaka abiria, mtu mmoja aliniambia nimkodishe pikipiki aendeshe mwenyewe, kuna watu anataka kwenda kuwafuata baada ya makubaliano ya bei nikamkabidhi pikipiki yangu na mimi nikamsubiri palepale.
Majeraha ya kichwani na begani aliyopata Simon Manase.
“Ilipotimu saa 6 nikaona jamaa harudi, nikaamua kuondoka nikiamini nitakutana naye njiani. Nilipofika mbali kidogo nikamuona Frank akiwa na panga mkononi huku akinishutumu kwamba natembea na mkewe, nilijaribu kubisha, akarusha panga la kichwa katika hatua ya kujihami nililipanchi na mkono ambapo alinikata mkono.
“Mkewe naye alikuwepo, alipojibu si kweli alimpiga,”alisema kijana huyo.
Juhui za mwandishi wetu kutaka kuzungumza na Frank zilikwama kufuatia mtuhumiwa huyo kutimua mbio akiogopa chombo cha habari.
Mganga mkuu wa hospitali aliyolazwa Simon, Alfred Chiponda alithibitisha kumpokea mgongwa huyo.
Mkuu wa kituo cha polisi, afande James Charles alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema vijana wake wanamsaka  Frank.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate