EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, November 8, 2014

BABA DIAMOND AMSAKA WEMA


Stori: Musa Mateja na Gladness Mallya
Baada ya Wema Isaac Sepetu ‘Beautful Onyinye’ kummwaga mwanaye, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, baba mzazi wa jamaa huyo, Abdul Jumaa ‘Baba Diamond’, amenaswa akimsaka mrembo huyo ili kujua mbichi na mbivu.
Baba mzazi wa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’akigonga getini kwa Wema.
‘UBUYU’ KUTOKA KWA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, baada ya kusikia habari za mwanaye kumwagwa na Wema aliumia roho kwani anamkubali Wema kuliko warembo wengine wote ambao walishatembea na mwanaye huyo.

“Hakuna habari mbaya kwa baba Diamond katika kipindi hiki kama ishu ya Wema kumwaga.
MAUMIVU
“Unaambiwa ‘mdingi’ aliumia sana kwani huwa anampenda mkwe wake Wema.
“Baba Diamond anaamini kabisa kwamba Wema ana nyota ndiyo maana Diamond akiwa naye huwa anang’ara sana,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
...Akiwasili nyumbani kwa Wema.
TATIZO NI NINI?
“Amekuwa akimsaka Wema ili ajue tatizo ni nini na kama kuna uwezekano wakae wayamalize.”
Habari zilieleza kwamba, kwa wiki nzima, baba Diamond amekuwa akimfuata Wema nyumbani kwake, Mtaa wa Bwawani-Kijitonyama jijini Dar lakini amekuwa akimkosa.
RISASI JUMAMOSI MZIGONI
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti hili (Risasi Jumamosi) lilipiga kambi kwa siku kadhaa getini kwa Wema huku likiweka mtego ambao juzikati ulimnasa mzee huyo.Baba Diamond alishuhudiwa akigonga geti kwenye nyumba hiyo anayoishi mkwe wake na kuzungumza na mlinzi ambaye alimwambia kuwa mwanadada huyo hayupo.
Akiondoka kwa Wema kumfuata Diamond.
Kwa mujibu wa mlinzi wa getini hapo mzee huyo alikuwa akiomba kumuona Wema ili amuulize sababu ya kumwacha Diamond ambaye walikuwa na mapenzi kama ya njiwa.Baada ya kumkosa mzee huyo alisema anaendelea kumsaka hadi atakapompata ili wazungumzie ishu hiyo kiundani.
WAZO LA KWENDA KWA DIAMOND
Baada ya kuondoka nyumbani hapo kwa Wema, mzee huyo alisema huenda yupo kwa Diamond na hata kama hatakuwepo itabidi azungumze naye juu ya ishu hiyo ya kuachwa na Wema.
Ilisemekana kwamba mzee huyo anafanya jitihada zote hizo kwani kwa upande wake Wema ndiye mwanamke pekee anayemkubali.
Ilielezwa kwamba baba Diamond anataka kuwasikiliza kila mmoja na kuhakikisha anawaunganisha upya ili waendelee na safari yao ya kimapenzi hadi watakapooana.
Akigonga getini kwa mwanaye.
TUJIUNGE NYUMBANI KWA DIAMOND
Huku wanahabari wetu wakipeana ishara kuwa wawahi getini kwa Diamond au Dangote, walipofika mahali hapo, dakika chache baadaye mzee huyo alinaswa getini kwa mwanaye maeneo ya Sinza-Mori, Dar akigonga mlango.
GETI LAFUNGULIWA
Baada ya kugonga kwa muda mrefu huku akiwa amefura, alitokea msichana ambaye alimfungulia mlango mdogo wa getini ambapo alikuwa akizungumza naye akiomba kuonana na Diamond bila mafanikio.
MAMA DIAMOND KWA MBALI
Wakati mzee huyo akiomba kuingia ndani, kwa mbali alionekana mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ kwa mbali akiwa amekaa barazani bila kutambua sauti ya baba Diamond aliyekuwa akizungumza nje ya geti.

Staa wa muziki Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
MADANSA WA DIAMOND
Hata hivyo, baadhi ya madansa wa Diamond walikuwa wakiingia na kutoka bila kumjali mzee huyo huku mmojawao akimfananisha bila kuwa na uhakika.Baba Diamond alipoona imeshindikana kumuona mwanaye huku mlango ukifungwa, aliondoka kwa huzuni akiamini ipo siku atawakutanisha Wema na Diamond ili kumaliza tofauti zao.
Gazeti hili liliwatafuta zilipendwa hao kwa nyakati tofauti lakini hawakupatikana hivyo jitihada za kuwafikia zinaendelea au hata wao wenyewe wakisoma habari hii watatupigia simu zetu kwani wanazo namba.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautful Onyinye’.
TULIKOTOKA
Huko nyuma, Diamond aliwahi kudai kwamba baba yake alimtelekeza yeye na mama yake ambapo waliishi maisha ya tabu na kushindwa kusoma kwa kukosa ada lakini hivi karibuni alitangaza kumsamehe.
Wakati Diamond akifanya kufuru kila kukicha na kugawa magari, baba yake anaishi peke yake,  maeneo ya Magomeni-Kagera, Dar.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate