EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 18, 2014

TANZANIA INAENDA KUSHIRIKI, SI KUSHINDANA

Mshindi wa Shindano la Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanywa, Jumamosi ya wiki iliyopita, alikwea pipa kuelekea jijini London, Uingereza kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss World, yanayotarajiwa kutimua vumbi Desemba 14, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Excel London.
Mshindi wa Shindano la Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanywa.
MAANDALIZI HAFIFU
Hata hivyo, wakati Happiness akiondoka nchini, mama yake mzazi alikuwa akiendelea kunung’unika kwamba Kamati ya Miss Tanzania, ilishindwa kumfanyia mwanaye maandalizi ya kutosha kwa wakati ikiwa ni pamoja na kumcheleweshea fedha za kufanyia shopping pamoja na maandalizi mengine.
Akizungumza na kituo kimoja cha runinga, mama mzazi wa mnyange huyo, alisema wakati mwingine alilazimika kutoa fedha zake za mfukoni ili kumsapoti mwanaye, ikiwa ni pamoja na kumpa fedha kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya maandalizi ya awali ikiwemo kupiga picha zitakazotumika Miss World.


ATAFUA DAFU MBELE YA WENZAKE?
Happiness si mshiriki pekee kwenye mashindano hayo, atakuwa na kazi ya ziada ya kuchuana na wenzake 128 kutoka nchi mbalimbali duniani, kumsaka mrembo atakayerithi taji ambalo mpaka sasa linashikiliwa na mwanadada Megan Young wa Ufilipino.
Swali la kujiuliza ni je, Tanzania inategemea Happiness afanye vizuri wakati mpaka anaondoka, mwanadada huyo na mzazi wake walikuwa wakinung’unika kutokana na maandalizi hafifu aliyoyapata? Tunategemea atang’ara mbele ya wenzake ambao nchi zao zinawaandaa vya kutosha kwa kuwapa sapoti ya nguvu?
LUNDENGA APIGA KIMYA
Showbiz ilimtafuta Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga, waandaaji wa shindano hilo ili kumuuliza ukweli kuhusu madai hayo lakini hakuwa akipokea simu yake licha ya mwandishi kumpigia mara kadhaa. Hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maandishi, bado aliendelea kupiga kimya (kuuchuna).
Happiness Watimanywa.
KAMATI YA MISS TANZANIA KUNANI?
Sakata la Watimanywa kuondoka bila kuwa na maandalizi ya kutosha, linakuja siku chache baada ya kutokea tukio lingine la kihistoria ambapo aliyekuwa mshindi wa kwanza mwaka huu kwenye mashindano hayo, Sitti Mtemvu alilazimika kuvua taji lake kwa madai ya kudanganya umri, na nafasi yake kuchukuliwa na mshindi wa pili, Lilian Kamazima.
USHAURI KWA HAPPINESS
Japokuwa umeondoka katika mazingira magumu, Watanzania wengi wanakutazama kwa macho ya matumaini kwamba angalau unaweza kuwatoa kimasomaso kwenye mashindano hayo makubwa zaidi katika tasnia ya urembo duniani.
Showbiz inakutakia kila la heri Happiness, jiamini kwamba unaweza kufanya makubwa na kurudisha heshima nyumbani, kama alivyowahi kufanya Nancy Sumari kipindi hicho. Licha ya ‘magumashi’ ya Kamati ya Miss Tanzania, amini kwamba Watanzania wapo nyuma yako!- Mhariri.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate