EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, November 2, 2014

MPENZI WA MEYIWA AZUIWA MAZISHINI

Johannesburg, Afrika Kusini. Familia ya nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini ‘Bafana Bafana’, Senzo Meyiwa imemzuia mpenzi wa mwanasoka huyo na mama wa mtoto wake, Kelly Khumalo, kuhudhuria mazishi yake mjini Durban, kwa mujibu wa New Age.



“Mazishi haya yapo wazi kwa kila mtu kuhudhuria na kutoa heshima zake za mwisho kwa Senzo, lakini yule msichana (Kelly Khumalo) haruhusiwi. Asifikirie kabisa kuhusu hilo,” alinukuliwa baba wa Meyiwa, Samuel.


Ofisa Upelelezi wa Gauteng, Meja Jeneali Norman Taioe aliwaambia waandishi wa habari mjini Johannesburg jana kwamba Meyiwa alipigwa risasi kifuani alipokuwa amekwenda kumtembelea mpenzi wake, ambaye ni mwanamuziki na msanii, Kelly 
Khumalo, katika mji wa Vosloorus, Ekurhuleni Jumapili usiku.


Wanaume wawili waliingia katika nyumba hiyo wakati kipa huyo mwenye miaka 27 wa timu ya taifa na klabu ya Orlando Pirates akijiandaa kutoka na mpenzi wake. Mmoja kati ya wauaji hao alikuwa nje.


“Senzo na rafiki yake walikuwa wanatoka wakati watu wawili wakiingia ndani ya nyumba hiyo. Mmoja wa watu hao alimdhibiti mmoja wa marafiki wa Senzo,” Taioe alisema Jumatatu.


Risasi moja ilipigwa ndani ya nyumba na mbili nyingine zilipigwa ovyo nje. Watu hao walifanya tukio hilo na kuiba simu.


Zawadi nono ya Rand 250,000 imetangazwa kutolewa kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa wahusika.

Polisi ilitoa michoro ya sura za watu wawili wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo wakiwa na rasta kichwani na mmoja ana jino la dhahabu. Meyiwa anatarajiwa kuzikwa mjini Durban kesho.


Wakati huo huo; kunatarajiwa kuwa na maziko ya nyota watatu wa Afrika Kusini Jumamosi, Mbulaeni Mulaudzi, Senzo Meyiwa na Phindile Mwelase, ambao wataagwa kwenye ukumbi wa Standard Bank mjini Johannesburg.


Nahodha wa Bafana Bafana na Orlando Pirates, Meyiwa aliuawa kwa kupigwa risasi mjini Vosloorus Jumapili, wakati mshindi wa dunia wa zamani wa mbio za mita 800, Mulaudzi alipoteza maisha katika ajali ya barabarani, Ijumaa iliyopita.

Bondia wa kike, Mwelase alifariki dunia baada ya kushindwa kuamka tangu alipoanguka na kupoteza fahamu wiki mbili zilizopita.


Awali, familia ya Meyiwa iliombwa na klabu ya Orlando Pirates kumzika kipa huyo Jumapili kutokana na wingi wa maziko ya watu maarufu siku hiyo.
 Lakini, baba yake, Samwel Meyiwa alikataa ombi hilo na kusisitiza kuwa mtoto wake atazikwa Jumamosi kama walivyopanga awali.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate