EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, November 1, 2014

NINGEKUWA MIMI PROFESA TIBAIJUKA NISINGEFUMBIA MACHO UOZO HUU KATIKA ARDHI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka.
Kwako Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka.
Najua bado hujatulia kutokana na ziara ya kushtukiza ya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee jimboni kwako, Muleba Kusini ambapo amemwaga ‘upupu’ kwa wapiga kura wako. Sijui lengo la ziara yake jimboni kwako ni nini lakini leo sitaki kuzungumzia hilo.
Pamoja na wakati mgumu ulionao kutokana na matatizo lukuki ya ardhi yanayokuhusu moja kwa moja kwa sababu wewe ndiye waziri mwenye dhamana katika masuala yote ya ardhi, nataka kukufikishia ujumbe wangu kwako.
Mimi sikuzaliwa Oktoba 12, 1950 katika Kijiji cha Kangaviyo mkoani Kagera kama wewe. Nakuapia sina CV kubwa kama wewe, sijawahi kufundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tangu mwaka 1993 hadi 1998 kama wewe.

Sijawahi kupata ‘exposure’ kubwa ya kimataifa kama wewe, sijawahi kufanya kazi katika Shirika la Umoja wa Mataifa la UN-Habitat wala sijawahi kuzunguka sehemu nyingi duniani, nikishika nyadhifa mbalimbali kama wewe.
Mimi ni mlalahoi tu, mbumbumbu nisiyejua chochote kuhusu mambo ya kimataifa wala serikali na utawala kama wewe. Hata hivyo, hilo halinizuii kukufikishia ujumbe wangu kwako.
Najua kwamba wewe ni mwanamke mchapakazi, uliyesoma na mwenye uwezo wa kuongoza ndiyo maana umeshika nyadhifa mbalimbali kwa nyakati tofauti, kuanzia Umoja wa Mataifa mpaka kwenye Serikali ya Tanzania. Naamini umepata uzoefu mkubwa wa namna ya kuongoza na kuzitatua kero mbalimbali zinazowakabili watu unaowaongoza.
Hata hivyo, mbona unashindwa kuonesha uzoefu na uwezo wako katika wizara unayoiongoza? Kuna matatizo mengi sana yanayohusu ardhi katika nchi hii, nikianza kuyaorodhesha, gazeti zima litajaa na bado hayataisha.
Ina maana huyajui matatizo haya? Hujui kero zinazowakumbwa wananchi wa Mbarali kwenye shamba la mpunga la Kapunga? Huyajui matatizo ya ardhi yanayowakabili wananchi wa Kigamboni? Vipi kuhusu mgogoro wa muda mrefu wa Chasimba na Chatembo, Kinondoni jijini Dar es Salaam?
Vipi kuhusu mapigano ya wakulima na wafugaji katika Bonde la Mto Rufiji na mkoani Morogoro? Ulianzisha mkakati kabambe wa kubomoa mahekalu ya watu waliojenga kwenye fukwe za bahari na uoto wa mikoko lakini mbona nyumba zilizobomolewa zilikuwa ni za ‘akina mwenzangu na mimi’ tu wakati mahekalu ya vigogo bado yamesimama?
Sitaki kuamini taarifa zinazoeleza kuwa unamiliki ekari zaidi ya 800 katika Kijiji cha Kyamnyorwa wilayani Muleba katika jimbo lako. Sitaki kuamini kama ni kweli na wewe unamiliki ekari za kutosha eneo la Kigamboni. Naamini wewe ni mzalendo, unawapenda Watanzania na ndiyo maana uliamua kuachia wadhifa mkubwa Umoja wa Mataifa na kurudi kuwatumikia wananchi wa Muleba.
Lakini mbona unashindwa kuyashughulikia matatizo haya yanayowakera wengi? Viwanja vya wazi karibu asilimia kubwa vimeshavamiwa na kujengwa ‘mijengo’ ya maana, kwa nini unalifumbia macho hili?
Kwa bahati mbaya mimi nitabaki kuwa mimi na sitaweza kuwa wewe lakini kama ningekuwa mimi kwenye nafasi yako, kwa hii migogoro ya ardhi inayoendelea nchi nzima, narudia tena kusema bila kumung’unya maneno kwamba nisingeifumbia macho, ningechukua hatua haraka sana.
Pengine hii ndiyo ingekuwa alama kwa wananchi wangu juu ya uaminifu wao kwangu kwa nyadhifa nyingine kubwa zaidi maana nasikia unataka kuchukua kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Wasalaam!
CREDIT: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate