EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 6, 2014

BILA UKAWA CCM HAING’OKI – ZITTO

Bila UKAWA CCM haing’oki - Zitto  
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema kuwa mwanasiasa yeyote makini kutoka vyama vya upinzani mwenye dhamira ya kuiondosha madarakani Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hawezi kukwepa kufanya kazi na muungano wa vyama vinavyounda kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Zitto anasema kuwa hata vyama vichanga vinavyokua kama ACT-Tanzania na vingine, vina nafasi ya kuingia katika umoja huo ili kuzidisha nguvu ya upinzani kuing’oa CCM kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Mwanasiasa huyo, alitoa kauli hiyo katika mahojiano maalum na gazeti hili, yaliyofanyika juzi nyumbani kwake jijini Dar es Salaam juu ya masuala mbali mbali ya kijamii na kisiasa, huku akieleza namna UKAWA wanavyoweza kufanikisha ushindi wa kuing’oa CCM.

Zitto alisema kuwa, uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Disemba 14 mwaka huu, uchukuliwe kama sehemu ya kujifunza makosa yatakayofanyiwa kazi kuelekea katika ushindi wa mwaka 2015.

“Nimefurahi kukutana na wenzangu wa CHADEMA wakati wa mashauriano juu ya maazimio ya kamati ya PAC, nimekulia CHADEMA…nimefanya kazi CHADEMA, wapo niliowalea kisiasa, wapo niliowapokea kina Silinde, Lyimo na wengine, hivyo kukutana nao kwa pamoja baada ya mtafuruku ulioanza Disemba 22 mwaka jana, kumenipa faraja sana na sioni shida kufanya kazi na UKAWA kwa maslahi ya nchi,”alisema Zitto.

Alisema tofauti yake na chama chake haiwezi kumzuia kufanya kazi na UKAWA na kwamba hata kukutana kwao katika kujadili maazimio ya kamati ya Bunge kwa ajili ya kuwachukulia hatua watuhumiwa wa kashfa ya Escrow, ulikuwa mpango wa Mungu.
Kwa mujibu wa Zitto, ili UKAWA waweze kushinda katika uchaguzi ujao ni vema viongozi pasipo kujali maslahi binafsi, wakajiwekea malengo ya idadi ya viti vya ubunge watakavyopigania kwa nguvu zote wakiwa katika mgawanyo watakaokubaliana.

“Katika hili la ushindi kwa upinzani ndani ya muunagano ni dhahiri hauna mjadala, cha muhimu ni kukubaliana kwa mfano kuwa wanataka wabunge wangapi watakaowapigania kwa pamoja na hapa wasipungue 150 kwa mgawanyo utakaokubalika; mfano Zanzibar, CUF wasimamishe wagombea katika majimbo yote na bara wapate katika baadhi ya maeneo wanayokubalika,” alisema na kuongeza;
“CHADEMA NCCR-Mageuzi na ACT-Tanzania waweke wagombea kwa upande wa bara katika maeneo wanayokubalika na kila mgombea apiganiwe kwa nguvu zote katika eneo analokubalika dhidi ya mgombea wa CCM,”alisema Zitto.

Alisema vyama hivyo kwa umoja wao vikiwa na uhakika wa kupata wabunge 150, wasiokuwa na ushindani kutoka CCM, wanaweza kugombania majimbo mengine kwa ajili ya kuongeza idadi ya wabunge kwa lengo la kupata serikali yenye nguvu zaidi.
Kuhusu kutafuta maridhiano ndani ya CHADEMA, Zitto alisema maridhiano ya aina yoyote yatakayofanywa yanapaswa kuwashirikisha watu wote walioumizwa na shutuma alizopewa.

“Nimesamehe kila aina ya matusi niliyofanyiwa lakini mambo mawili sitoweza kuyaacha, moja ni kutaka shutuma kuwa ninatumiwa na CCM kwa ajili ya usaliti ithibitishwe na kama haupo waliotunga uongo huo wawajibishwe kwa kuwa hii pasipo kuthibitishwa kwa tuhuma hizo za usaliti, kutamuathiri hata mwanangu na kizazi change,”alisema Zitto.
Alisema yupo tayari kuwajibika kwa yale atakayoyafanya kuliko kuvumilia baadhi ya mambo yasiyokuwa na maslahi kwa Umma.
CHANZO: TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate