EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 13, 2014

MADAI MAZITO: ROSE MUHANDO ATUNDIKWA MIMBA


 CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

Haya ni madai mazito! Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando, anadaiwa kutundikwa mimba a.k.a ujauzito unaomfanya hivi sasa kutumia muda mwingi kujificha ndani, Risasi Jumamosi limenyetishiwa.
Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando wakati akifanya yake.
Mapema wiki hii, chanzo kimoja kilipiga simu katika chumba chetu cha habari na kusimulia kuhusu habari hiyo, kwamba, Rose ambaye hana mume, amenasa na muda wowote kuanzia sasa anaweza kuitwa mama.

KUMBE
Madai ya chanzo hicho yalieleza kwamba, staa huyo amekuwa akijichimbia nyumbani kwake mkoani  Dodoma tofauti na siku za nyuma ambapo alikuwa hakauki jijini Dar.

“Kama hamsadiki ninayowaambia, najua ninyi mmebobea kwenye habari za uchunguzi ‘so’ fanyeni yenu mtaniambia,” kilidai chanzo hicho kikiomba chondechonde kisichorwe jina gazetini.
KUJIRIDHISHA
Ili kujiridhisha na habari hiyo, pasipo kwanza kuwasiliana na Rose, moja kwa moja, gazeti hili lilimpigia simu mmoja wa watu wa karibu wa nyota huyo (jina linahifadhiwa), alipopatikana, aliulizwa kuhusu ishu hiyo na haya ndiyo aliyoyaeleza:

Rose Muhando akipafomu na madansa wake.
“Yaani hadi leo mlikuwa hamjapata hii habari? Mimi siku zote nilikuwa najua labda kwenu siyo habari kwa sababu ujauzito huu ni wa siku nyingi. “Hata sasa hivi ukimuona alivyo unajua wazi kuwa kuna kichanga tumboni kwani tumbo limechomoza hatari.”
Mtu huyo wa karibu alisema anapokuwa nyumbani Dodoma mara nyingi amekuwa mtu wa kukaa ndani tu kutokana na watu kumshangaa.Alisema Rose amekuwa akijificha kwa sababu ya kuogopa macho ya watu na uchovu unaotokana na hali aliyonayo ‘kuchoka’.
NANI MHUSIKA?
Juu ya nani mhusika wa mimba hiyo, mtu huyo wa karibu, ambaye anafahamu kila kinachofanywa na nyota huyo wa Wimbo wa Facebook alisema kuwa, inadhaniwa kuwa ni ya mcheza shoo wake (jina kapuni).

Inadaiwa kwamba, Rose, mara kadhaa amekuwa akisisitiza kuwa ni lazima amzalie mtoto jamaa huyo kwa jinsi anavyompenda.“Huyo mcheza shoo ana uhusiano naye kwa muda mrefu kidogo na ameshasema kwa watu wengi tu kwamba endapo Mungu atapenda basi atafurahi kama atamzalia mtoto.
“Mimi hajaniambia mimba hasa ni ya nani, lakini naziona dalili zote kuwa ni ya huyo kijana,” alisema mtu huyo.

Rose Muhando na madansa wake wakitoa burudani.
MWENYEWE ANASEMAJE?
Baada ya kujiridhisha na maelezo ya mtu wake wa karibu, gazeti hili lilianza kumtafuta Rose, mama wa watoto watatu ambao wote amezaa na wanaume tofauti, lakini katika hali ya kushangaza, simu yake iliita hadi kukatika bila kupokelewa, hata baada ya kupigwa mara kadhaa.

Likiamini huenda alikuwa katika shughuli au mahali panapombana kuzungumza, gazeti hili lilimtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) na kumsomea mashitaka hayo ili atoe ufafanuzi, lakini pia hakuweza kujibu.
Likiamini huenda simu yake haisomeki kwa mtumishi huyo wa Mungu, gazeti hili lilitumia simu nyingine ambayo nayo iliita kwa muda mrefu hadi kukatika pasipo kupokelewa na hata pia alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu wenye maelezo kuhusu hali yake ya sasa, pia haukujibiwa hivyo jitihada zinaendelea.
NI MTOTO WA NNE
Endapo itathibitika, ujauzito wa Rose utakuwa ni wa mtoto wa nne ambapo mara kadhaa staa huyo amekuwa akisema hayupo tayari kuolewa hivyo kuwaacha baadhi ya watumishi midomo wazi wakiamini mtu wa sampuli yake haifai kuzaa nje ya ndoa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate