EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, December 15, 2014

MISS TZ AFARIKI GHAFLA

KWELI kifo hakina huruma jamani! Mshiriki wa Miss Tanzania 2013 akitokea Miss Ilala, Martha Gewe, mkazi wa Tabata Segerea, Dar amefariki dunia baada ya kuugua ghafla, Ijumaa Wikienda linakupa zaidi.
Marafiki wa aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2013 akitokea Miss Ilala, Martha Gewe wakiwa na huzuni.
Martha amekutwa na mauti katika Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana jijini Dar es Salaam, Ijumaa iliyopita ambako alikimbizwa baada ya kuugua na madaktari walibaini kwamba, malaria ilipanda kichwani.

AFYA YAKE SIKU ZA NYUMA
Habari zaidi zinasema kuwa mrembo huyo hakuwa akisumbuliwa na ugonjwa wowote huko nyuma na alionekana mwenye afya njema huku mipango yake ikiwa imelenga jinsi atakavyoisherehekea Sikukuu ya Krismasi.
“Lakini Jumatano iliyopita alianza kuumwa, alisema anahisi homa ambayo baadaye ikabainika ni malaria.
Mwili wa marehemu Martha Gewe ukiwa kwenye jeneza.
“Tulimpeleka Amana, akalazwa kwa siku tatu tu, leo (Ijumaa) akafariki dunia. Madaktari wamesema ile malaria kukimbilia kichwani ndiyo tatizo,” alisema ndugu mmoja wa marehemu huyo kwa sharti la kutochorwa jina gazetini kwa kuwa siyo msemaji wa familia ya mzee Gewe.
WALICHOSEMA MADAKTARI
Ijumaa Wikienda lilifanikiwa kuzungumza na madaktari wawili wa Hospitali ya Amana jijini Dar kuhusu ugonjwa wa malaria kupanda kichwani.
Na hii ndio safari ya mwisho ya marehemu Miss Martha Gewe.
“Mpaka sasa bado malaria ni tishio, inaua watu wengi sana. Kwa malaria kupanda kichwani ni hatari zaidi kwani mgonjwa anaweza kupoteza maisha ndani ya muda mfupi sana.
“Kikubwa watu wazingatie kuwa mbali na mazingira hatarishi kwa ugonjwa huo na wajichunge kuumwa na mbu ambao ndiyo wana-oeneza ugonjwa huo,” alisema daktari mmoja.
MAMISI WENZAKE NI MACHOZI
Kufuatia taarifa za kifo hicho, mamisi wenzake walipigwa na mshangao, wengine wakiuliza nini kilimpata mwenzao huyo!
Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa.
“Kwa kweli nilipopata taarifa za kifo cha Martha sikuamini mara moja kwa vile sijawahi kusikia akiumwa au hata kwamba alilazwa kwa muda mrefu.
“Kifo chake kimeniumiza sana, sijui hata nisemeje jamani, kweli kifo hakina huruma,” alisema Miss Ilala 2013, Dorice Mollel huku akilia.
Mrembo mmoja ambaye hakutaja jina lake alisikika akisema: “Yaani Happiness (Watimanywa) yuko Uingereza kusaka taji mwenzake anapoteza maisha ghafla hapa nyumbani Tanzania! Inauma sana kwa kweli.”
Warembo wengine walioshiriki msiba wa Martha nyumbani kwao, Tabata, Dar walishindwa kujizuia na kujikuta wakibubujikwa machozi muda wote kiasi cha kushindwa kuongea na mwandishi wa gazeti hili.
Hashim Lundenga ‘Anko’.
HISTORIA YA MARTHA KATIKA UMISI
Mwaka jana, Martha alishiriki shindano la kumsaka Redd’s Miss Ukonga lililofanyika katika Ukumbi wa Wenge Garden, Ukonga Mombasa jijini Dar.
Katika kinyang’anyiro hicho, Martha aliibuka kidedea kwa kuvalishwa taji hivyo kupata tiketi ya kwenda kushiriki Miss Ilala 2013 kwenye Ukumbi wa Golden Jubilee Tower, Dar ambapo mshindi alikuwa Dorice.
Marehemu alipata nafasi ya kuvuka Miss Ilala na kushiriki Redd’s Miss Tanzania 2013 chini ya Hashim Lundenga ‘Anko’ na kufanikiwa kuwa miongoni mwa Kumi Bora huku Happiness Watimanywa akiibuka mshindi.
Marehemu Martha Gewe enzi za uhai wake.
Watimanywa usiku wa kuamkia leo, kule jijini London, Uingereza  alifurukuta kugombea Taji la Miss World!
MAZISHI YA MARTHA 
Marehemu Martha alizikwa Jumamosi iliyopita kwenye makaburi ya nyumbani kwao, Tabata Segerea jijini Dar es Salaam huku msiba huo ukihudhuriwa pia na warembo mbalimbali ambao wamewahi kuvaa mataji nchini.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate