EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, January 19, 2015

KAMA SIYO MUZIKI WANGEKUWA PANYA ROAD

Msanii wa Hip Hop Bongo, Kala Jeremiah akipozi katika ndinga lake.
Makala: Chande Abdallah na Deogratius Mongela/Ijumaa Wikienda

WAKATI watu wengine wakikata tamaa na kutojibidiisha huku baadhi ya vijana wakijiingiza kwenye makundi ya uporaji kama Panya Road katika kuyatafuta mafanikio kupitia uwezo na vipaji walivyopewa na Mungu, wafuatao ni baadhi ya mastaa ambao kwa vipaji vyao wameweza kwa namna moja au nyingine kuvumilia msoto na hatimaye kutoka kimaisha:-
Kala Jeremiah
Akiwa jijini, Mwanza mwanzoni mwa mwaka 2002 alijiingiza kwenye biashara ya mitumba maeneo ya Mlango Mmoja. Mwaka 2005 aliingia ndani ya Jiji la Dar akiwa hana ndugu yeyote hali iliyomfanya awe anashinda studio za kurekodia muziki huku akidandia chakula na malazi kwa chipukizi wenzake. Kala alishawahi kujiingiza kwenye mchezo wa kamari kama njia pekee ya kujiingizia kipato, nyota yake ilianza kuonekana baada ya kuingia ndani ya mashindano ya Bongo Star Search (BSS) yaliyofanyika mwaka 2006 na baada ya hapo akawa staa.
Msanii wa mziki wa Bongo Fleva,Shilole.
Shilole
Akiwa Tabora, Igunga alishawahi kuuza genge na kufanya kazi ya mama n’tilie, katika maisha hayo alijikuta akibakwa na kupata ujauzito akiwa katika umri mdogo huku malezi ya mtoto wake yakimkabili. Miaka ya 2010 akiwa Dar, alipata nafasi ya kuonesha kipaji chake cha uigizaji na kufanikiwa kukubalika na kuwa staa mkubwa kabla ya kuingia kwenye muziki wa Bongo Fleva ambapo anaonekana kukubalika zaidi.Mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz akipozi.
Diamond
Jina lake halisi ni Nasibu Abdul, jamaa anatajwa kati ya mastaa ‘waliohustle’ mbaya ambapo akiwa anaishi maeneo ya Tandale, jijini, Dar. Aliwahi kuuza mitumba baadaye alihamia kwenye kiwanda cha kutengenezea mabegi kilichopo Mikocheni kwa mshahara mdogo ambao sawa na bure na baadaye alijishughulisha na kuuza mafuta, kabla ya kutoboa kimuziki akiwa chini ya Sharobaro Records.
Msanii wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego akipozi.
Nay wa Mitego
Jina lake kamili ni Emmanuel Elibariki. Jamaa alinukuliwa kwenye baadhi ya ‘interview’ zake kuwahi kufukuzwa nyumbani kwa wazazi wake na kuanza maisha ya kujitegemea ambapo alijiingiza kwenye kazi za saluni kama kinyozi wa deiwaka. Nay anasimulia kuwa kwa kazi hiyo aliendesha maisha yake na kulala hapohapo saluni. Baadaye akaamua kujiingiza kwenye muziki na kuanza kukubalika hatimaye kuwa staa mkubwa.

Dude
KABLA ya kuwa staa, Kulwa Kikumba ‘Dude’ Alishawahi kupitia hali ngumu ya kimaisha hadi kufikia hatua yakufanya kazi kama muhudumu wa baa kabla ya kuhamia kwenye uchomeleaji wa mageti, miaka ya 1998. Baadaye alianza harakati za sanaa na kuwika akiwa huko hadi sasa.Msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Masawe.
Wolper
Jacqueline Wolper aliingia jijini, Dar na kuanza kufanya kazi za kutembeza vyombo mitaani chini ya kampuni fulani ya mauzo. Baadaye alijiingiza kwenye masuala ya saluni. Mwaka 2009 alishawishika kujiingiza kwenye sanaa ya maigizo na kutoboa akiwa huko.

AY
kwa mujibu wa paspoti yake anaitwa Ambwene Yessaya, jamaa aliingia jijini miaka 1996 akiwa hana ndugu yeyote. Akiamini muziki utamtoa, AY anasimulia kuishi kwa kudandia nyumbani kwa rafiki yake aliyekuwa chini ya himaya ya wazazi. Baadaye aliihama nyumba hiyo baada ya wazazi wa rafiki yake kuwa na maswali mengi juu yake kuhusu wapi ametokea na wazazi wake ni akina nani! Alishawahi kulala kwenye kontena moja lililopo maeneo ya Upanga, jijini Dar na kukaa muda mrefu bila kula.
Msanii wa Bongo Fleva kitambo, 'AY' akipozi.
Pamoja na kukesha studio, alishawahi pia kutembea kwa miguu kutoka Upanga hadi Mnazi Mmoja kila siku akienda kuoga na kufua nguo zake katika vyoo vya umma vya Uwanja wa Mnazi Mmoja ambavyo enzi hizo vilikuwa bure, baadaye aliamua kujikita kwenye muziki akiwa mdogomdogo na kufanikiwa kuibukia katika Kundi la East Coast Team lililokuwa na makazi yake Upanga, jijini Dar.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate