EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, January 5, 2015

MUME, MCHEPUKO WAGOMBEA MTOTO

Makubwa! Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mke wa mtu aliyekuwa akiishi ukweni na mumewe wa ndoa, Bahati Ramadhani, amenusurika kuuawa na ndugu wa mumewe wakiwemo mawifi na wakwe zake baada ya kudaiwa kumgonganisha mumewe na mchepuko wake na kujikuta wakigombea mtoto.
Mwanamke, Bahati Ramadhani anayeidaiwa kumgonganisha mumewe na mchepuko.
Tukio hilo la kushangaza lililojaza kadamnasi lilijiri nyumbani kwa wakwe hao, Mtaa wa Mawenzi jirani na Soko la Matunda la Mawenzi la mjini hapa wiki iliyopita ambapo Bahati alikuwa akiishi na mumewe, ldd Yusuf.
Ilielezwa kwamba wanandoa hao walibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume (jina kapuni) ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 2.
Polisi akimbana kwa maswali mwanamke huyo kuhusu utata uliotokea.
Siku ya tukio, mama mkwe wa Bahati, Faidha Cosmas alishtukia dili baada ya kuona sms ya mwanaume ‘aliyeseviwa’ kwa jina la Saddy kwenye simu ya Bahati ikimweleza kwamba alikuwa amemtumia fedha za matumizi ya mtoto wao huyo.

Baada ya mama mkwe kuona ishu hiyo alimwambia mwanaye Idd ambapo kwa pamoja walimpigia Saddy aliyekiri kuwa anachojua mtoto huyo ni wake na amekuwa akituma fedha za matumizi.
Mama mkwe alisema kwamba walimwita Bahati na kumuuliza kama anamfahamu Saddy ambapo alikiri kuchepuka.

Mwanamke, Bahati Ramadhani akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.
Baada ya mzozo wa hapa na pale, mawifi wa Bahati waliingilia kati na kuibua bonge la mtiti wakimpa wifi yao kipigo hadi mwandishi wetu alipotonywa na kufika eneo la tukio.
Alipofika mahali hapo na kuona hali ya hatari ndipo akaita polisi wa doria ambao walifika na kutuliza ghasia.

Familia hiyo ilishuhudiwa ikiwa kwenye kikao ambapo uamuzi wa awali ulikuwa ni ldd kumuacha mara moja Bahati.
Wananchi wakishuhudia mkasa huo kwenye eneo la tukio.
Hata hivyo, katika uamuzi huo wa awali, Bahati alikubali kuondoka lakini kwa masharti ya kuondoka na mwanaye jambo ambalo liliikera familia hiyo na kumvamia wakitishia kumtoa roho.
Kabla ya mambo kuwa mabaya, polisi wakiongozwa na Afande Mwajabu waliingilia kati na kumuokoa Bahati.

Afande Mwajabu aliwahoji wahusika na baada ya maelezo, ldd alitoa uthibitisho wa kadi ya kliniki ambayo ilionesha yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.
Katikati ni mtoto anayegombewa katika utata uliojitokeza.
Mwandishi wetu pamoja na Afande Mwajabu walimpigia simu Saddy ambaye kwa sasa yuko masomoni mkoani lringa na kuweka ‘loud speaker’ ambapo alipoulizwa alisema:
“Mtoto ni wangu. Kwa sasa ana umri wa miaka 2 na kadi ya kliniki ninayo.”
Saddy alipoulizwa na mwandishi wetu kwa kipindi chote cha miaka miwili, mtoto wake alikuwa akiishi wapi alisema:

Mwanamke aliyegonganisha wanaume akichepuka akichukuliwa na mapolisi kutoka eneo la tukio.
“Nilikuwa bize na masomo lakini najua mwanangu yuko na mama yake.”
Kwa upande wake, Idd ambaye ndiye anayeishi na Bahati (huku akitokwa machozi) alisema hakutarajia kama mkewe angemsaliti kiasi hicho.
Bahati alipohojiwa, alisema kuwa siku aliyopata ujauzito alitembea na Saddy pamoja na mumewe ldd hivyo hata yeye anashindwa kujua baba halali wa mtoto wake.
Sakata hilo lilifikishwa polisi ambapo bado linatafutiwa suluhu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate