EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 6, 2015

PANYA ROAD 510 MBARONI


Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akionyesha picha za viongozi wa Panya Road kwa wanahabari.
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashikilia watu 510 wakiwemo viongozi watatu wa kundi linalojihusisha na uhalifu la ‘Panya Road’ .
Watu hao wamekamatwa katika operesheni inayoendeshwa na jeshi hilo, kupambana na uhalifu.
Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Suleiman Kova alisema jana kuwa watuhumiwa hao, ni pamoja na watuhumiwa 36 waliokamatwa juzi, kufuatia vurugu iliyotokea Ijumaa iliyopita.
Alisema chimbuko la Operesheni hiyo, inayoendeshwa na wakuu wa Polisi wa Mikoa ya Kipolisi ya Temeke, Kinondoni na Ilala, wapelelezi na askari wa kiintelijensia ni matukio yaliyowahusisha vijana hao na kusababisha tafrani kwa wananchi mbalimbali wa jiji la Dar es Salaam.
Baadhi ya Panya Road waliokamatwa.
Alitaja viongozi wa kundi hilo wanaoshikiliwa kuwa ni Khalfani Said (24) na Said Mohammed (22), wakazi wa Tandale Sokoni katika Manispaa ya Kinondoni na Mohammed Nangula (19), mkazi wa Mburahati kwa Jongo, pia Kinondoni.
Alisema kwamba kazi yao kubwa ni kuwaunganisha na kuratibu uporaji katika maeneo mbalimbali.
Alisema mbali na ‘Panya Road’, operesheni hiyo ambayo itakuwa ya kudumu kuanzia sasa, imewakamata wapigadebe, wacheza kamari na watuhumiwa wengine waliokamatwa katika vijiwe na katika msako wa nyumba kwa nyumba.

“Imegundulika kwamba kila inapotokea kijana ameuawa, wakati wa maziko viongozi hawa wanakuwepo na kuwachochea vijana wenzao kufanya vurugu, kama ilivyotokea Januari 2 katika eneo la Magomeni Kagera ambapo vijana walipambana na polisi baada ya maziko ya kijana mwenzao aliyefariki kutokana na matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi Januari Mosi eneo la Mwananyamala.
“Tunashukuru kwa kuwa baadhi ya wananchi waliweza kutupa ushirikiano wa moja kwa moja kuwabaini wahalifu tunaowashikilia, ni ukweli usiopingika kuwa vijana hawa wanaojihusisha na vitendo viovu wanafahamika kwa wananchi hivyo ni jukumu la wazazi, walezi katika mitaa yote ya Dar es Salaam kujihusisha kikamilifu katika kuwabaini vijana hao ili tuweze kukomesha maovu yao ambayo pia ni kero kwa wananchi,” alisema Kamanda Kova.
Aidha, alisema katika operesheni hiyo, pia watuhumiwa hao walikamatwa na vilevi mbalimbali zikiwemo bangi, lita 150 ya pombe kali aina ya gongo na mabunda matatu ya dawa za kulevya aina ya mirungi.
Alisema katika kuhakikisha msako huo unazaa matunda, jeshi hilo limeweka mpango maalumu wa kuwahusisha moja kwa moja watendaji kuanzia ngazi ya Mitaa, Kata na Tarafa ili waweze kushirikiana na polisi kuweza kuwabaini wahalifu au makundi ya uhalifu wa aina hiyo.
Alisema mpango huo utafanikiwa kutokana na semina elekezi iliyotoa mafunzo hayo, iliyofanyika hivi karibuni kwa watendaji hao katika kukabiliana na matukio hayo.
Aliwataka vijana ambao hawana kazi za kufanya, kutafuta njia nyingine za kuendesha maisha yao na siyo kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya na kufanya makosa ya jinai, yanayowafanya baadhi kujiingiza katika makundi hayo.
(CHANZO: HABARI LEO)

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate