EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 11, 2015

FAMILIA DAR YAVUNJIWA NYUMBA USIKU!

FAMILIA ya mzee Wilson Lyimo, mkazi wa maeneo ya Sinza-Makaburini, jijini Dar, imejikuta ikilala nje kwa wiki kadhaa baada ya kuvunjiwa nyumba yao usiku wa manane na watu wanaodaiwa kuwa ni mabaunsa wapatao 60.

Vitu vikiwa nje baada ya nyumba kuvunjwa.
Mabaunsa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo usiku wa kuamkia Februari 24, mwaka huu wakati wanafamilia hao pamoja na wapangaji wawili wakiwa wamelala ndani ya nyumba hiyo.
Chanzo makini kimeeleza kuwa, mabaunsa hao walipofika kwenye nyumba hiyo, waliamuru watu wote waliokuwa ndani watoke nje wakidai wamepewa maagizo ya kuvunja nyumba hiyo na jamaa mmoja (jina tunalihifadhi kwa sasa).
Mabaunsa hao walianza kubomoa kuta za nyumba hiyo bila kujali watoto na wapangaji kama wametoka nje au la ambapo hali hiyo ilisababisha usumbufu na upotevu wa baadhi ya vitu ambavyo thamani yake haikupatikana mara moja.

Kundi hilo la watu waliokuwa na nyundo na sururu waliendelea kuvunja nyumba hiyo huku wakitembeza kipigo kwa yeyote aliyejitokeza kutaka kuzima zoezi lao la kubomoa.
Kwa mujibu wa mtoto wa kwanza wa familia hiyo, Edwin Lyimo, baba yake anamiliki eneo hilo kihalali tangu mwaka 1977 kwa namba ya kiwanja Block C Namba 68, Namba ya Hati 21818 yenye jina la usajili, Wilson Fataeli Lyimo.
Edwin aliendelea kufunguka kuwa, awali familia hiyo ilikuwa na mgogoro wa muda mrefu na jamaa aliyetajwa na mabaunsa hao kuhusu kiwanja na nyumba hiyo hadi kufikishana Mahakama ya Ardhi lakini ghafla wameshangaa kuona mabaunsa hao wamekuja kuvunja nyumba hiyo.
Akizungumza na waandishi wetu, mzee Lyimo alidai kuwa nyumba hiyo ni yake na hati anazo na kuongeza kuwa anashangazwa na watu hao waliovamia na kuvunja nyumba yake na kuahidi kuwachukulia hatua ambapo amefungua jalada kituo cha polisi Mabatini lililosomeka KJN/2050/2015/KUVUNJA NA KUIBA USIKU.
Waandishi wetu walifika eneo la tukio na kukuta nyumba ya familia hiyo ikiwa imebomolewa huku wenyewe wakiweka mahema ili kujisitiri na mvua na jua huku wakiwa hawana msaada wowote.
Jitihada za kumpata jamaa aliyetajwa na mabaunsa hao ili aweze kuzungumzia sakata hilo hazikuzaa matunda kutokana na simu yake kutopatikana hewani, jitihada zinaendelea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate