EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 19, 2015

KAMA MKE NA MUME WANAPIGANA PICHA ZA UTUPU, WAPENZI JE?

Mapenzi ya sasa yamejaa sarakasi nyingi sana, kwa yule aliyebahatika kuingia kwenye uhusiano anatakiwa kuwa makini kuhakikisha mapenzi hayamtibulii maisha yake.Yapo mambo mengi ya kuwa nayo makini, changamoto kubwa na ya msingi ambayo wengi tunakumbana nayo ni uhakika kama kweli wanaodai wanatupenda wanamaanisha au wana zuga?Kwamba yule anayesema anakupenda ukimpasua kwenye moyo wake wewe utakuwa ndiye uliyechukua nafasi? Wengi wamebaki njia panda wanapofikiria hilo.Mbali na changamoto hiyo, pia wengi hufikiria namna ya kulinda penzi lisife. Wapo waliotokea kupendana sana lakini wakaishia njiani kwa kuachana.
Lakini pia wapo ambao mpaka leo hii wanajiuliza kama waliotokea kuwapenda wana nia njema? Kwamba anayekuambia anakupenda na anatamani siku moja uwe mwenza wake anamaanisha kweli au ana lake kichwani?
Kama ulikuwa hujui ni kwamba, wapo wanaume ambao wamejiwekea malengo ya kutembea na idadi flani ya wanawake kwa kipindi flani. Kwa hiyo wewe unayo changamoto ya kubaini kama huyo uliye naye siyo kati yao!

Achilia mbali hao wanaume, wapo wanawake pia ambao kazi yao ni kubadili wanaume kila siku, akifuatwa na mwanaume hawezi kusema ‘no’, atamkubalia.
Atakuwa naye kwa kipindi flani huku kuchuna ikiwa ni sehemu ya maisha yake kisha baada ya muda anamuacha. Ndiyo maana nikaanza kwa kusema kuwa, maisha ya kimapenzi ya sasa yamejaa changamoto nyingi sana.
Hata hivyo, kubwa ambalo leo nataka kulizungumzia linahusu hii tabia ya baadhi ya wapenzi wanapokuwa faragha kupigana picha za utupu! Hakika hili linanishangaza sana na nahisi wanaofanya hivyo hawana akili timamu.
Huwa najiuliza, mwanaume au mwanamke anapochukua simu au kamera kisha kumpiga au kumrekodi mpenzi wake akiwa kama alivyozaliwa ni ili iweje? Anazipiga kwa ajili ya matumizi gani? Ni swali ambalo hata wewe mwenye akili timamu unaweza kuwa unajiuliza.
Katika kujua kilicho nyuma ya pazia, nilijaribu kuzungumza na baadhi ya wanaume ambao ndiyo wanaotajwa sana kufanya kamchezo hako. Wapo waliosema wanafanya hivyo kwa kujifurahisha tu lakini wengine wakasema eti ni ili wanapokuwa mbali na wapenzi wao wapate kitu cha kujiliwazia.
Si wanaume tu wanaosema hivyo, hata baadhi ya wanawake nao walisema hivyohivyo. Lakini sasa cha ajabu wapo waliokuwa wawazi zaidi kwa kusema kuwa, wanawapiga picha wapenzi wao wakiwa watupu ili wakigombana wazitumie kuwakomoa. Yaani mwanaume anampiga picha mpenzi wake ili siku wakikorofishana au akitaka kuachwa, aziachie kwenye mitandao ili kumkomoa.
Sasa, ukiacha zile sababu nyingine, tusimamie hii ya kwamba wengi wanazipiga ili wakigombana na wapenzi wao wawaaibishe. Wewe ambaye una akili zako timamu unakubalije  kupozi mbele ya kamera na kumruhusu mpenzi wako akufotoe?
Hebu tuache huu ulimbukeni. Kupigana picha tukiwa watupu ni kinyume na maadili na sheria za nchi. Ukiona mpenzi wako anachukua simu yake kisha kutaka kukupiga picha, chukulia huyo hakupendi na siku hiyo iwe ndiyo mwisho wa uhusiano wenu.
Ninachokushauri msomaji wangu uliye kwenye uhusiano ni kwamba, ukiwa faragha na mpenzi wako hata kama unampenda na unamuamini sana, kuwa makini naye. Sasa hivi kwa teknolojia ilivyo watu wanapiga picha kwa siri kiasi kwamba ukizubaa utashangaa siku unaambiwa picha zako za utupu zipo, unabisha kumbe umepigwa na mpenzi wako bila wewe kujua.
Huwezi kuamini wapo watu wako kwenye ndoa lakini ukipekua simu zao wana picha za wake zao au waume zao wakiwa watupu, sasa kwa wapenzi wa kawaida hali ikoje?

Ni hayo tu kwa leo, hadi wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate