EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 13, 2015

CCM HAIJAWAHI KUTOKEA!

Mwandishi Wetu
NIJohn Pombe Joseph Magufuli ambaye amepita kwa kishindo na ‘usimpimie’ kuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan, lakini yaliyojiri katika mchakato wa kumpata mgombea huyo, hayajawahi kutokea, Ijumaa Wikienda limechimba na kuchimbua.
Mh.John Pombe Joseph Magufuli akiwashukuru wajumbe baada ya kumteua kuwa mgombea wa CCM.
Sarakasi zilikuwa ni nyingi lakini katika kukiokoa chama kisizame mjini Dodoma, ilibidi kutumia akili nyingi na nguvu ya ziada kumpata mtu clean (safi) ambaye ni Magufuli.
Uchunguzi wa kina uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba, tangu uhuru wa Tanzania (1961) hakujawahi kuwa na mvutano mkubwa, ikiwemo wajumbe kuonesha upinzani dhahiri mbele ya mwanyekiti wao wakati wa mikutano ya chama hicho katika kumchagua mgombea achilia mbali idadi kubwa ya waliojitokeza.
Baadhi ya wapiga kura waliozungumza na gazeti hili walisema, mwaka huu uchaguzi ndani ya CCM umekuwa mgumu kiasi kwamba, hakuna rekodi yoyote inayofanana nayo hapo miaka ya nyuma.
Akitoa neno baada ya kuteuliwa.
“Mimi nimekuwepo tangu uhuru, sijawahi kuona ugumu wa uchaguzi ndani ya chama, tangu Tanu (Tanganyika African  National Union) mpaka sasa CCM. Hii ni hali ya hatari.“Kwanza hata wajumbe wenyewe walikosa adabu hata kwa mwenyekiti wao,” alisema mzee Bakar Masoud, mkazi wa Msasani, Dar.
“Watu wanabebana bwana! Mimi sijawahi kuona, safari hii sijui haya mambo yametokea wapi?” alisikika mwanachama mmoja wa chama hicho akisema kutokea mkoani Dodoma.

AWALI, UTARATIBU ULIVYOKUWA
Katika ratiba iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Julai 9, 2015, Kamati Kuu ya CCM (CC) inakaa kupitia majina yote ya wanachama 38 waliojitokeza kugombea na kuyakata ili kubakisha majina matano yenye sifa kwa mujibu wa mtazamo wa kamati hiyo.
Yalipatikana majina hayo ambayo ni January Yusuf Makamba, Bernard Camillus Membe, Asha–Rose Mtengeti Migiro na Balozi Amina Salum Ali.Julai 10, 2015, Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) kukaa kwa lengo la kupokea hayo majina matano kutoka CC na kuyapigia kura ili yapatikane majina matatu.
Majina matatu yalipatikana ambayo ni John Magufuli (kura 2104 sawa na 87.1%), Asha-Rose Migiro (kura 59 sawa na 2.4%) na Amina Salum Ali (kura 253 sawa na 10.5%).
Akiwa na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan.
Julai 11, 2015, Mkutano Mkuu wa CCM kukaa kwa ajili ya kuyapigia kura majina matatu ili kupata jina moja kwa ajili ya kupeperusha bendera ya chama hicho dhidi ya wagombea wa upinzani kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa urais utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
RATIBA YAPANGUKA
Hata hivyo, katika hali isiyokuwa ya kawaida, ratiba zote hizo hazikwenda sawa baada ya kutokea kwa ugumu uliokuwa nje ya uwezo wa chama. Hadi Julai 11 siku ya Mkutano Mkuu, Nec walikuwa hawajamaliza kikao chao hivyo kuingilia ratiba ambayo si yake.
Matokeo yake, Julai 11 kukawa na vikao viwili, Nec iliyoanza saa nne asubuhi wakiwa wamelala na kiporo walichopewa na CC waliomaliza kikao saa saba usiku na Mkutano Mkuu ambao ulianza saa mbili usiku.
Mabadiliko mengine yaliyojitokeza ni baada ya matokeo ya kumpata mgombea mmoja kushindwa kupatikana hadi jana saa 6:30 usiku ambapo mwenyekiti wa chama hicho aliahirisha kikao mpaka asubuhi ya saa 4:00 tofauti na miaka mingine ya uchaguzi ndani ya chama hicho.
UPINZANI DHAHIRI
Katika hali ambayo haikutarajiwa, kwenye mkutano wa Nec, wakati viongozi wa chama kitaifa wakiingia kwenye Ukumbi wa Dodoma Convention, wajumbe walisimama na kuimba wimbo wa chama huku sehemu ya kumtaja mwenyekiti (Jakaya Kikwete) wao walichomekea jina la Lowassa (Edward) ambaye alikuwa miongoni mwa waliojitokeza kugombea lakini jina lake likakatwa mapema huku kukiwa na malalamiko kwamba, mgombea huyo alionewa.
“Tuna imaaaniii na Lowaaaassa, oyaa! Oyaa! Oyaaa!” baadhi ya wajumbe walisikika wakiimba hivyo.
Baadhi ya wananchi waliokuwa wakifuatilia runingani mkutano huo walisema kulitaja jina la Lowassa kwa wakati huo ilhali alishakatwa ni uasi na upinzani, kwani uwepo wa mwenyekiti ulitaka staha zaidi.
WAJUMBE WA CC KUPINGA
Tukio lingine ambalo lilionesha halijawahi kutokea ni kitendo cha wajumbe watatu kutoka CC kujitokeza hadharani kupinga uamuzi wa wajumbe wengine.
Wajumbe hao ni Emmanuel Nchimbi aliyekuwa msemaji wa wenzake, Sophia Simba na Adam Kimbisa ambao walidai kuwa, katika kikao cha kukata majina matano, kanuni ya chama ya mgombea anayekubalika na wengi ndiye apite, haikuzingatiwa.
Hata hivyo, Nchimbi hakumtaja mgombea anayependwa na wengi japokuwa wengi walimsemea kuwa alimaanisha Edward Lowassa.
LOWASSA GUMZO
Licha ya jina la Lowassa kukatwa mapema katika hatua ya kushindwa kuingia ‘Top 5’, jina lake limeendelea kuwa gumzo kila kona ya nchi, baadhi ya watu wakimzungumzia kwa namna yoyote ile tofauti na wagombea wengine.
Kwenye mitandao ya kijamii, ishu ni Lowassa hadi gazeti hili linakwenda mitamboni. Baadhi ya watu walitupia hivi:
“Hivi kweli Lowassa wamemkata?! Jamani, kweli CC ni kiboko. Hivi sasa itakuaje?
“Hivi ni kwa nini Lowassa amekatwa? Si walisema ndiye atapita kwenye Tano Bora, nini kimetokea? Siasa bwana ni ngumu sana.“Lowassa out! Daa! Kweli CCM ina wenyewe. Lakini naamini hata waliopita wanaweza, mfano Magufuli, anakubalika pia.”
Kwa upande wake Kikwete alisema kuwa kazi aliyopewa na chama chake ya kumpata mgombea anayefaa, ameifanikisha na kinachosubiriwa ni ushindi wa kishindo dhidi ya wapinzani.  

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate