EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 6, 2015

MMEACHANA? HAKUNA SABABU YA KUCHUKIANA!

Mpenzi msomaji wa XXLove karibu kwenye Jumatatu nyingine mwanana katika ulimwengu wa uhusiano wa kimapenzi.Katika mada yetu tajwa hapo juu, nitazungumza na wale rakifi zangu walioachana au kuachwa na kuanza kumchukia mwenza wake.
Ni kweli kuachwa kunaumiza sana moyo. Kimsingi usiombe kukumbwa na maumivu ya kuachwa. Lakini kama hilo limekwishatokea, kwa nini uendelee kuumia na kumchukia aliyekuwa mpenzi wako?
Kitendo cha kukuacha wewe, kinaweza kumtokea hata yeye na kujikuta akilia na kuhuzunika kama wewe. Kama ndivyo basi mapenzi ndivyo yalivyo. Leo kwako, kesho kwake.
Hakuna sababu ya kuchukiana na kuwekeana visasi kwa sababu kama tutafanya hivyo, kwa dunia ya sasa iliyojaa uchepukaji, itakuwa dunia ya visasi kila kukicha.

Ifahamike kwamba, mapenzi hayana fomula, inawezekana mwenza wako akawa amerubuniwa na kuna siku atarejea kwako na kutulia kama unavyotaka.
Siwatetei wenye tabia ya kuacha, wala siyo tabia nzuri kubadilisha wapenzi, lakini pengine ni ujana ndiyo unamsumbua au ni tabia asili ya mwenza wako, tabia ambayo haipaswi kuigwa na ni hatari kiimani, kimaadili na hata kiafya.
Ninavyofahamu mapenzi ni kitu cha ajabu sana, inawezekana mkawa mmeachana kwa muda kwa maana ya kupumzishana au kuna mtu kaingilia kati penzi lenu au mmeachana moja kwa moja.
Haijalishi ni aina ipi ya kuachana ila ninachozungumzia ni kuachana au kuachwa na kujenga chuki, hakuna sababu kwa namna mapenzi yalivyo kwa sababu utachukia wangapi? Hivi kwa mfano, ukiachwa au kuachana na wapenzi watano na wote ukawachukia, si utakuwa umetengeneza bomu la hatari katika maisha yako? Kwa sababu utakuwa ukiwaona moyo wako unaumia na kuwaza mabaya juu yao.
Kama mlikuwa mnajua mtakuja kugombana, hamkuwa na sababu ya  kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na kama mlilazimishana, kupendana hakuna sababu ya kuchukiana. Naamini hamkujua kama mtakuja kugombana ndiyo maana mliamua kupendana na ‘kushea’ baadhi ya vitu vyenu.
Sidhani kama mliamua kuwa wapenzi ili mje kupeana stress (msongo), mgombane, mchukiane, muharibiane maisha na mambo mengine.
Kama umeachwa kwa sababu za msingi, kubaliana na ukweli ili maisha yasonge kuliko kuendelea kufikiria na kutengeneza chuki na uhasama na mtu aliyekuacha au kuachana, haisaidii kitu, kama wewe unavyohisi kutendwa na yeye huko alikokwenda anaweza kutendwa vilevile. Mapenzi ni mchezo usiokuwa na bingwa.
Angalizo; kwa wale wenye tabia ya kuacha hovyo, haipendezi kwani kuna mambo mengi ambayo unaweza kuyatengeneza bila kujua.
Wanawake huamini kwamba unapomuacha, huwa umemchezea kwa maana ya kutimiza haja zako na unapopata mtu mwingine ‘unamshiti’ bila kujua kuwa uhusiano wa mapenzi ni kama kitabu ambacho kinapaswa kifunuliwe kurasa zake. Inawezekana anayekifunua, akafunua kurasa moja na kukutana na andiko alilokusudia au kufunua kurasa zaidi na zaidi.
Tukutane wiki ijayo katika mada nyingine tamu na nzuri.

CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate