EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 7, 2015

MTOTO MIAKA 5 ATEKWA DAR, ABAKWA HADI KUFA

NIkweli dunia imekwisha! Ni vigumu kuamini mtoto mdogo ambaye anahitaji uangalizi na ulinzi kutoka kwa jamii anageuzwa mwanamke na kuingiliwa kwa nguvu hadi mauti. Huu ni unyama na ukatili wa hali ya juu.
Mtoto Ester Banzi enzi za uhai wake.
Tukio hilo la kutisha lilitokea katikati ya wiki iliyopita, Tabata Msimbazi jijini Dar ambapo mtoto Ester Banzi ,5, (pichani) alikutwa na mauti baada ya kuingiliwa kimwili na mwanaume ambaye inadaiwa alimteka kwanza.
Akizungumza na Gazeti la Uwazi kwenye msiba huo, mama mdogo wa marehemu Ester aliyejitambulisha kwa jina la Watende Hamis huku akitokwa machozi mfululizo, alisema:
“Siku ya tukio, ilikuwa saa 5:30 asubuhi tukiwa nyumbani, dada (mama wa marehemu aitwaye Rebeka) alikuwa ameinjika sufuria ya ugali jikoni kwa ajili ya chakula cha mchana.
“Akamtuma Ester dukani akanunue unga. Alimpa shilingi 1,200. Si mara ya kwanza Ester kutumwa dukani kwa vile ni jirani tu.

“Tulimsubiri Ester arudi na unga lakini alichukua muda mrefu. Ikabidi tumfuate dukani, hatukumuona. Tuliwauliza watoto wenzake ambao anapenda kucheza nao, wakasema walimuona amebeba mfuko cha Rambo huku akiongozana na baba mmoja.

Jeneza lililobeba mwili wa marehemu likiwa tayari kwa ajili ya kuagwa.
“Basi, tuliendelea kumtafuta bila mafanikio. Ikabidi tutoe taarifa kwa baba yake ambaye akaingiwa na wasiwasi, akaenda kutoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Tabata Shule.“Ndani ya masaa matatu baba yake akatupigia simu kwamba mwili wa Ester umeokotwa huku ukionekana alibakwa na kuharibiwa vibaya.”
Naye kijana anayeuza duka ambalo marehemu alitumwa kununua unga, bila kutaja jina lake alikiri Ester kufika dukani hapo na kupimiwa unga kisha akaondoka.
Baadhi ya wananchi majirani na maeneo hayo waliohojiwa na waandishi wetu kuhusiana na tukio hilo walisema kwamba wao walimuona mtoto huyo akifuatana na mwanamume mmoja, lakini hawakumtilia mashaka kutokana kwamba walifikiri ni ndugu yao.
Mtu mmoja ambaye mwili wa marehemu ulikutwa jirani na nyumba yake, naye alizungumzia tukio hilo:
“Sisi tulisikia sauti ya mtoto akiomba msaada. Tulipata hofu ikabidi tukaangalie eneo lile ndipo tulipouona mwili wa mtoto huyo. Tulipomchunguza tukagundua alibakwa kwani nguo yake ya ndani ilikuwa pembeni.
“Inaonekana huyo mtu hakuchukua muda mrefu kufanya kitendo hicho. Tulimpigia simu Mkuu wa Kituo cha Polisi Tabata Shule, Afande Kobelo akaja na timu yake. Hili tukio nahisi lina ushirikina ndani yake.”
Mmoja wa askari aliyefika katika eneo la tukio ambaye hakutaka kutaja jina lake kwa vile siyo msemaji mkuu wa jeshi hilo alisema mwili wa mtoto huyo ulionekana kuingiliwa kimwili, marehemu alivunjwa shingo na kutobolewa upande wa kushoto kichwani.Marehemu Ester alizikwa wiki iliyopita mkoani Morogoro. Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu. Amina.
CHANZO: GAZETI LA UWAZI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate