EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 4, 2015

Mkuu wa Mkoa Dar aonya watakaoleta vurugu



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki, amesema kwamba serikali ina taarifa kwamba kuna kundi la vijana ambalo litafanya vurugu wakati huu wa kampeni za uchaguzi na siku ya uchaguzi.
 
Hata hivyo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limesema halina taarifa zozote kuhusu vurugu hizo.
 
Sadiki alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, katika viwanja vya Mbagala Charambe jimbo la Mbagala.
 
Kada huyo wa CCM ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam, alipanda jukwaani na kuwahutubia wananchi waliokusanyika kumsikiliza Samia ikiwa siku ya kwanza ya kampeni za chama hicho katika Mkoa wa Dar es Salaam.
 
Hata hivyo, Sadiki hakufafanua vijana hao wameandaliwa na nani wala maeneo waliyoko. Pia hakueleza kama ni kutoka vikundi vya uhalifu wala vyama vya siasa zaidi ya kusema kuwa wameandaliwa kufanya fujo. 
 
POLISI WASEMA HAWANA TAARIFA
Alipotafutwa  Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, kuzungumzia suala hilo alisema hawezi kulizungumzia kwa kuwa bado hajapatiwa taarifa na kuahidi kuwa atakapopatiwa taarifa, atalitolea ufafanuzi.
 
“Sijaisikia hilo suala, siwezi kulizungumzia mpaka nitakapopata taarifa nitaliongelea,” alisema Kamanda Kova.
 
Kamanda Kova alisema ni vyema atafutwe Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke ili alitolee ufafanuzi.
 
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida, alisema wanawake na vijana wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo ukosefu wa ajira.
 
Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgombea mwenza,  alisema CCM inajua changamoto hizo na kwamba mgombea mwenza akiingia Ikulu atazitatua akishirikiana na mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli.
 
SAMIA AMWAGA AHADI MBAGALA
Akizungumza na wananchi wa jimbo la Mbagala, Samia alisema Mbagala siyo kituo cha utalii ambacho wanasiasa wanaweza kwenda na kupiga picha.
 
Alisema atahakikisha anatatua kero ya foleni ya magari ikiwamo kujenga barabara ya Mbagala hadi Kongowe.
 
Pia, aliahidi kujenga soko katika eneo la Temeke pamoja na Kijichi ili kutoa nafasi 5,000 kwa wafanyabiashara kufanya biashara.
 
Kuhusu usumbufu kwa wafanyabiashara  ndogo ndogo jijini Dar es Salaam, alisema hakuna mtu atakayebughudhiwa ikiwamo kulipishwa kodi zinazoleta usumbufu.
 
Aliahidi kuwaunganisha wafanyabishara katika benki mbalimbali ili wapatiwe mikopo ya kuanzisha na kuendeleza biashara.
 
Akizungumzia tatizo la ukoesfu wa maji, Samia alisema katika Jiji la Dar es Salaam kero hiyo itamalizika haraka watakapoingia Ikulu.
 
Samia alisema asilimia 30 ya tenda zote za halmashauri watahakikisha zinatolewa kwa wananchi wa kawaida ambao wananishi katika eneo husika.
 
Akizungumzia msongamano, Samia alisema tatizo hilo litaisha haraka watakapoingia Ikulu kwa kuwa watajenga barabara za juu pamoja na kusimamia usafiri wa reli.
 
MGOMBEA UBUNGE
Akizungumza katika mkutano huo, mgombea wa ubunge wa Jimbo la Mbagala (CCM), Issa Mangungu, alisema jimbo hilo linakabiliwa na uhaba wa vifaa vya ujenzi ukiwamo mchanga.
 
Kuhusu tatizo la barabara, Mangungu aliomba kujengwa njia mbili kutoka Mbagala hadi Kongowe ili kumaliza kero hiyo.
 
MGOMBE UDIWANI
Mgombea udiwani katika Kata ya Kilungule, Said Fela maarufu kama mkubwa Fela, alisema anajua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.
 
Fela ni mmmiliki wa bendi maarufu ya Yamoto ambayo imepata umaarufu kwa makundi yote wakiwamo wanawake na vijana.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate