EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 21, 2012

Waziri Membe atema cheche kuhusu ndoa za jinsia moja

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amewataka marafiki na mashabiki wa nchi zinazoshabikia ndoa za jinsia moja waache kuitania Tanzania.

Membe alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Konde, (CUF) Khatib Said Haji, aliyeitaka serikali kuzieleza nchi hizo kuwa ni kheri kuondoa misaada yao kuliko ndoa za jinsia moja.
                    Bernard Membe,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,

Akijibu swali hilo, Membe alisema suala hilo ni la kisiasa pia na ni vyema marafiki na mashabiki wanaozungumza na mataifa hayo kuwaaambia kuwa waache kuwatania Watanzania.


Katika swali la msingi mbunge huyo, alisema kumekuwa na msimamo mkali wa kimkakati wa nchi za Magharibi wa kuzitaka nchi rafiki ya zile zinazopokea misaada kutoka kwao kuhalalisha ndoa hizo.


Alihoji Tanzania ikiwa ni moja kati ya nchi hizo zinazopata misaada mbalimbali kutoka kwa mataifa hayo imejianda vipi kukabiliana na janga hilo hasa pale nchi hizo wahisaani zitakapokatisha misaada kwa Tanzania.


Akijibu swali hilo, Membe, alisema itakapotokea wahisani wakasitisha misaada kwa sababu ya msimamo wa Watanzania, nchi iko tayari kujifunga mikanda na kujibeba wenyewe badala ya kukubali kudhalilisha utu na utamaduni.


Alisema sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kipengele cha 9(a) tafsiri ya ndoa imeelezwa kuwa ni “Muungano wa hiari kati ya mwanaume na mwanamke wenye lengo la kudumu katika maisha ya wawili hawa”.


Alisema kulingana na sheria hiyo, suala la msingi ni kulingana na matakwa ya sheria ya Tanzania ili kuwepo na ndoa inayotambulika kisheria na ni lazima kuwepo pande mbili za jinsia tofauti yaani mwanamume na mwanamke.


“Nchi marafiki duniani zikiwemo za magharibi, zimeendelea kutuheshimu kutokana na msimamo wetu huo thabiti na usioteteleka kwa kuendelea kutoa misaada ya ushirikiano wa kiuchumi kwa serikali ya Tanzania,” alisema na kuongeza kuwa Tanzania itaendelea kupokea misaada ambayo haina masharti ya kubadili sera, utamaduni wa sheria za nchi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate