EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 21, 2012

Madaktari: Mgomo pale pale

Ni dhahiri mgomo sasa hauepukiki keshokutwa, baada ya kile kinachodaiwa kushindwa kwa serikali kutoa majibu ya utekelezaji wa madai mbalimbali ya madaktari nchini. 
Hali hiyo imedhihirika kufuatia madaktari katika hospitali mbalimbali nchini kujitokeza hadharani na kutangaza azma yao ya kugoma keshokutwa kuishinikiza serikali kutekeleza madai yao.
Wasiwasi wa kufanyika mgomo huo unakolezwa na kimya cha serikali ambayo licha ya madaktari hao kutangaza azma yao ya kugoma, hadi kufikia jana serikali ilikuwa bado haijatoa taarifa yoyote kuhusiana na hatima ya utekelezaji wa madai ya madaktari.
Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, alisema kufikia jana walikuwa hawajapokea taaraifa yoyote kutoka serikalini kuhusiana na madai yao.
                                                            Dk. Ulimboka
Dk. Ulimboka alisema kuwa leo wanatarajia kutoa tamko kuhusiana na suala hilo.
Wakati madaktari wakijianda kugoma, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi, amesema kuwa serikali inasubiri maamuzi ya Tume ya Usuluhishi kwa kuwa suala hilo liko katika mkondo wa sheria.

Akizungumza na NIPASHE jana jioni, Dk. Mwinyi alisema serikali haiwezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa inasubiri sheria ifuate mkondo wake.
Alisema wakati wa mgomo wa kwanza, suala hilo lilifikishwa mahakamani na mahakama kuamua liende katika Tume ya Usuluhishi ambayo ilitoa muda kwa serikali na madaktari kujadiliana ili kufikia mwafaka.

Alisema juzi Tume hiyo ilitakiwa kufuatilia makubaliano, lakini madaktari walikwenda katika Tume na kusema kuwa hawajakubaliana na serikali.
Hata hivyo, alisema kati ya madai 10 ya madaktari, matano yamekelezwa. Moja ya madai hayo alisema ni kuongezwa kwa posho ya kuitwa kazini kutoka Sh. 10,000 hadi Sh. 25,000.

Posho nyingine ni posho ya uchunguzi wa maiti kutoka Sh. 10,000 hadi Sh. 100,000 kwa daktari bingwa na wasaidizi wake Sh. 50,000. Nyingine ni kupewa kadi ya kijani kwa ajili ya huduma za afya na kupewa chanjo ya kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.
Dk. Mwinyi alisema dai lingine la kutaka uongozi wa wizara kubadilishwa limeshatekelezwa.
Hivi karibuni, madaktari waliipa serikali wiki mbili kuhakikisha inatekeleza madai yao, vinginevyo watagoma tena kama mgomo wa Januari na Fenruari mwaka huu uliotikisa sekta ya afya na kusababisha madhara makubwa kwa wagonjwa katika hospitali nyingi za umma.

Pia hawakukubaliana na maelezo ya ripoti ya kamati ya serikali iliyopewa kazi ya kushughulikia madai ya madaktari.
Walisema ripoti hiyo imeshindwa kueleza jinsi madai yao yatakavyoshughulikiwa, likiwamo la nyongeza ya mshahara, ambapo walitaka kima cha chini kiwe Sh. milion 3.5.
Walidai wamegundua katika ripoti hiyo kuwa serikali haina nia ya kutekeleza madai yao na kwamba kila wanapokutana katika kikao, wamekuwa wakijibiwa majibu yasiyoridhisha.
Walisema kuna madai yao, ambayo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyatolea maamuzi walipokutana katika mkutano uliowakutanisha madaktari wote katika Hospitali ya Taifa ya 

Muhimbili (MNH), ambayo kamati hiyo imeyaondoa wakati yalishafanyiwa kazi.
Walisema Pinda aliwaambia katika kipindi cha bajeti ijayo kuhusiana na posho ya madaktari kwa wale wanaoitwa kuendelea na kazi wakati wanapokuwa katika mapunziko walijulishwa kuwa daktari bingwa atapatiwa Sh. 50,000 na kwa daktari wa kawaida atapatiwa Sh. 40,000. Hata hivyo, walisema suala hilo limeondolewa.
Madaktari hao walisema katika suala hilo kamati imeamua kuondoa utekelezaji huo na kubakiza Sh. 20,000 na Sh. 25,000 kwa daktari bingwa, wakati Waziri Mkuu aliziongeza kwa kiwango hicho na kuwaahidi kuwa katika bajeti ya mwaka 2012/2013 wataongezewa kiwango hicho.

Mbali na hayo, pia walisema kuna mambo mbalimbali ambayo kamati hiyo imeshindwa kuwatekelezea licha ya kwamba waliahidiwa kuwa yangefanyiwa kazi na serikali.
Kutokana na hilo, madaktari waliipa serikali siku 14 kuhakikisha inatekeleza madai yao na kwamba kama haitafanya hivyo wanajianda kufanya mgomo wa madaktari wote nchini.
Pamoja na hilo pia walitangaza mgogoro baina yao na serikali.
KCMC WATANGAZA MGOMO
Wakati Ulimboka akisema hivyo, madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro jana walitangaza kujiunga na mgomo huo iwapo serikali itashindwa kutoa majibu ya madai yao.
Mwenyekiti wa madaktari hao, Dk. Rosemary Mrina, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Juni 15, mwaka huu, walikutana na kujadili kwa kina taarifa ya serikali ya kamati ya majadiliano baina ya serikali na madaktari iliyoundwa wakati wa mgomo wa awali.
Dk. Mrina alisema hawajaridhishwa na majibu ya serikali kwani yameshindwa kuwa na jibu la kutatua kero zao.
Kero hizo ni upungufu wa vifaa tiba na dawa, mazingira magumu ya kufanyia kazi, maslahi yao ikiwemo posho mbalimbali ambazo ni stahili zao.

Daktari Mugisha Nkoronko ambaye ni mjumbe wa kamati ya kitaifa ya kushughulikia madai ya madaktari alisema tayari Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kimetangaza mgogoro wa wiki mbili kati yake na serikali, hivyo ni wazi kuwa watakaoathirika ni wananchi.
“Hatupendi ile hali ya wakati ule ijirudie, lakini serikali inatulazimu kufika huko kutokana na majibu mapesi yaliyotolewa, tumepeleka madai ya kurasa 50 wamejibu kwenye karatasi moja, moja ya maadui watatu tunaopigana nao tangu nchi ipate uhuru ni maradhi, lakini serikali imeshindwa kutatua kero zetu ili nasi tufanye kazi katika mazingira mazuri,” alisema.

Alisema madai ya madaktari yamebebwa na hoja nzuri na za msingi, lakini majibu ya serikali ni mepesi sana na ambayo huwezi kuyatarajia na kuwa mgogoro huo ulishafika kwa rais ambaye aliingilia kati na kuahidi kuutatua, lakini hakuna lililofanyika.
Dk. Anette Kessy alisema serikali imewapuuza wakati mgogoro uliopita Rais Jakaya Kikwete aliahidi kuupatia suluhu, lakini hadi sasa hakuna majibu waliyoyapata.
 Juzi madaktari katika Hospitali ya Rufani ya Bugando jijini Mwanza walitangaza kuunga mkono mgomo huo.
                                       CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate