EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 17, 2012

CRDB YASHINDA TENDA YA KUCHAPISHA TIKETI KWA ELEKTRONIKI


DAR ES SALAAM, Tanzania
 Benki ya CRDB PLC imeibuka mshindi wa tenda ya kutengeneza tiketi za elektroniki za kuingilia uwanjani iliyotangazwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ofisa Habari wa TFF Boniface Wambura ameithitibishia Habari Mseto.
 
Kampuni saba zilijitokeza katika hatua ya awali ya kuonesha nia (Expression of Interest) kwa ajili ya tenda hiyo ambapo Aprili 19 mwaka huu Kamati ya Mipango na Fedha ya TFF ambayo ndiyo Bodi ya Tenda ya shirikisho ilipitia maombi hayo na kupitisha nne kati ya hizo.
 
Baadaye kampuni hizo nne; CRDB Bank PLC, Prime Time Promotions, Punchlines (T) Limited na SKIDATA People Access Inc. zilitakiwa kuwasilisha rasmi tenda zao zikionesha jinsi zitakavyofanya shughuli hiyo pamoja na gharama ya utengenezaji kwa tiketi moja.
 
Bodi ya Tenda ya TFF ilikutana Julai 13 mwaka huu kwa ajili ya kupitia tenda hizo ambapo kampuni zote nne zilifanya uwasilishaji (presentation) wa jinsi zitakavyofanya shughuli hiyo, na baadaye kuipa kazi hiyo benki ya CRDB.
 
Uamuzi huo wa Bodi ya Tenda uliwasilishwa mbele ya Kamati ya Utendaji ya TFF. Kamati ya Utendaji ya TFF katika kikao chake kilichofanyika Julai 14 mwaka huu iliridhia uteuzi huo wa benki ya CRDB.
 
Baadhi ya vigezo ambavyo Bodi ya Tenda ya TFF iliangalia na kuipa CRDB tenda ni, uwezo wa kufanya kazi hiyo (Capacity), hadhi yake mbele ya jamii (Credibility) katika shughuli inazofanya na teknolojia ya kisasa itakayotumika kutengeneza tiketi hizo.
 
Uamuzi wa TFF kutangaza tenda hizo ulilenga kuimarisha udhibiti wa mapato ya milangoni na kurahisisha mtiririko mzima wa washabiki kupata tiketi na kuingia viwanjani.
 
Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema: “Hatua hii ni muhimu sana, kwani tulikuwa tukiisubiri kwa muda mrefu. Si tu itaimarisha udhibiti wa mapato, bali pia itaondoa matatizo ya tiketi na kuendelea kujenga Credibility (kuaminika) ya TFF. Mafanikio haya si kwa TFF pekee bali mpira wa miguu kwa ujumla.”
   
Kwa mujibu wa Wambura, CRDB imeanza mara moja mchakato wa shughuli hiyo, ambapo tiketi hizo zinatarajia kuanza kutumika rasmi katika kipindi cha kati ya miezi miwili na mitatu ijayo kuanzia sasa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate