EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 20, 2012

Haikubaliki kwa mjamzito kupoteza maisha akijifungua – Rais Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa ni jambo lisilokubalika kwa mwanamke kupoteza maisha wakati akijifungua kwa sababu uja uzito siyo ugonjwa.

Aidha, rais Kikwete amesema kuwa pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali katika kupunguza vifo vya akinamama wakati wa uzazi na mipango mingine ya uzazi bora, bado tatizo linabakia kubwa na zinahitajika juhudi zaidi ili kuondokana na tatizo la vifo wakati wa uzazi.

Rais Kikwete ameyasema hayo, Alhamisi, Julai 19, 2012, wakati alipokutana na kuzungumza na Mtendaji Mkuu wa shirika la kimataifa lisilokuwa la kiserikali la Pathfinder International, Dkt. Purnima Mane, Ikulu, Dar es Salaam.

Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo lisilokubalika kabisa kwa mwanamke kupoteza maisha wakati akijifungua. “Uzazi siyo ugonjwa na kwa hakika ni jambo lisilokubalika kwa mwanamke kupoteza maisha wakati akijaribu kutoa maisha kwa binadamu mwingine. Hili ni jambo ambalo Serikali itaendelea kupambana nalo hadi kulifikisha mahali pazuri zaidi.”

Rais Kikwete amesema kuwa ni kweli kuwa Serikali yake imekuwa inafanya juhudi kubwa katika eneo hili lakini bado tatizo ni kubwa na zinahitaji jitihada za ziada. “Tumefanya jitihada kubwa na kupata mafanikio ya kujivunia lakini bado kazi ni kubwa.”

Takwimu za sasa zinaonyesha kuwa akinamama 578 kati ya 100,000 hupoteza maisha wakati wa uzazi, idadi ambayo imeshuka kutoka miaka minne iliyopita wakati takwimu zilionyesha kuwa akinamama 790 kati ya laki moja walikuwa wanapoteza maisha wakati wa kujifungua.

Miongoni mwa maamuzi ambayo Serikali imechukua kukabiliana na tatizo hilo ni pamoja uamuzi wa kupunguza umbali wa kufikia huduma za afya kwa kujenga zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata na hivyo kuhakikisha kuwa huduma hizo zinapatikana katika umbali usiozidi kilomita tano.

Serikali pia imeamua kuwa kila zahanati ama kituo cha afya lazima kiwe na huduma za kuhudumia wazazi na waja wazito.

Serikali pia imechukua hatua za kukabiliana na ugonjwa wa ukimwi ambao ni moja ya chimbuko kubwa la vifo vya akinamama waja wazito.

Dkt. Mane ambaye anatembelea Tanzania kwa mara ya kwanza amemsifu Rais Kikwete kwa uongozi wake katika masuala ya afya na masuala mengine. “Uongozi wako katika suala hili ni jambo linalojulikana duniani pote. Tunakushukuru sana kwa sababu wewe ni bingwa wetu na msemaji wetu mkubwa katika mapambano ya usalama wa akinamama waja wazito.”

Pathfinder International ni shirika la kimataifa lisilokuwa la kiserikali ambalo malengo yake makuu ni kushughulikia afya za akinamama na kuboresha uzazi. Katika Tanzania, Pathfinder International linaendesha miradi tisa kwa sasa katika maeneo ya ukimwi, masuala ya uzazi na uzazi wa mpango.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.

Dar es Salaam.

19 Julai, 2012

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate