EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 13, 2012

Madaktari wacharuka

Wataka iundwe tume huru ya kuchunguza sakata zima
CHAMA cha Madaktari Tanzania (MAT), kimepanga kufanya maandamano makubwa ya amani jijini Dar es Salaam ili kupinga dhuluma na uonevu dhidi ya taaluma muhimu ya udaktari na madaktari wenyewe.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa MAT, Dk. Rodrick Kabangila, alisema maandamano hayo yatatanguliwa na mkutano mkubwa wa madaktari wote utakaofanyika leo kujadili mustkabali na mwenendo wa taaluma ya udaktari.

Kwa mujibu wa Dk. Kabangila, MAT inasikitishwa na dhuluma hiyo kwa kuzingatia uwiano duni wa madaktari hapa nchini ambapo daktari mmoja hutibu wagonjwa 30,000 kwa mwaka chini ya viwango vya kimataifa.

Alisema jumla ya madaktari 400 walio chini ya usimamizi wa madaktari bingwa, wamesitishiwa usajili wao na wengine kusimamishwa kazi bila kujali umuhimu wao kwa mustakabali wa taifa na wananchi wake.
“Tutafanya maandamano ya amani, madaktari wote na wadau wa sekta hii wenye mapenzi mema tunawaomba washiriki… madaktari tutavaa makoti yetu meupe na watakaoshiriki nasi wavae vitambaa vyeupe.

Maandamano yataanzia nje ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, tutaishia kwenye geti la Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, tukiwa na mabango ya kulaani kitendo cha kutekwa, kupigwa na kutelekezwa kwenye msitu wa Pande alichofanyiwa Dk. Steven Ulimboka,” alisema.
Dk. Kabangila alisema kuwa wataishinikiza serikali iunde tume huru kwa ajili ya kuchunguza suala la Dk. Ulimboka itakayofanya kazi haraka na wahusika wote wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Awali, katibu huyo alieleza kushangazwa kwake na wanaojiita viongozi wa dini ambao huwakatisha tamaa kwa kuwanena mabaya bila kujali mazingira magumu wanayofanyia kazi madaktari.

Interns wanena
Kwa upande wake, mwakilishi wa madaktari wanafunzi wa mafunzo kwa vitendo (interns), Frank Kagoro, alisema kitendo cha Baraza la Madaktari kusitisha usajili wao bila kuwasikiliza ni kinyume cha matakwa ya sheria.
Dk. Frank alisema usitishwaji wa usajili huo umefanywa kimakosa kwa sababu umewagusa waliomaliza mafunzo yao na waliokuwa kwenye likizo ya uzazi jambo linalowashangaza.

Alisema kuwa kuwafukuza madaktari wanafunzi na kuwaacha madaktari bingwa ni kosa kwa sababu wanafanya kazi chini ya uangalizi wa mabingwa hao huku akisisitiza kwamba bila baraza hilo kuwa huru haki za madaktari zitaendelea kukandamizwa.
“Tunasikitishwa na utendaji wa baraza hili ndiyo maana moja ya madai yetu hata Waziri Mkuu tulimwambia tunataka baraza huru lisiwe chini ya Wizara ya Afya. Hapa tunapozungumza baadhi ya madaktari wameanza kuandika barua za kuacha kazi,” alisema.

Dk. Frank alisema wanaiomba serikali idhamirie kwa dhati kumaliza mgogoro huu vinginevyo ukandamizaji wanaofanyiwa utawakatisha tamaa hata wanaotamani kuwa madaktari siku zijazo.
Mgogoro kati ya madaktari na serikali ulianza mwaka 2005 ambapo madai ya wataalam hao ni mazingira bora ya kazi, vitendeakazi bora, mashine za kisasa na nyongeza ya posho na mishahara.
Kushindwa kumalizika kwa mgogoro huo kulisababisha Jumuiya ya Madaktari nchini, kuitisha mgomo mwanzoni mwa mwaka huu ili kuishinikiza serikali kutimiza madai yao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate