EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 13, 2012

Njiwa wa Diamond wazua tafrani kwa mashabiki

TUKIO la msanii Naseeb Abdul ‘Diamond’ kutinga Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam na njiwa wanne, kwenye Tamasha la Matumaini lililofanyika hivi karibuni, limezua mitazamo tofauti kwa mashabiki, huku wengine wakiingiza imani za kishirikina.

Tanzania Daima, lilishuhudia baadhi ya mashabiki wakirumbana katika gari la abiria, lililokuwa likitoka Ubungo kuelekea Mlandizi, ambako ubishi ulianza mara baada ya dereva wa gari hilo kuweka wimbo wa Diamond, unaokwenda kwa jina la ‘Mawazo’ unaotamba vilivyo hivi sasa hapa nchini.

Huku wimbo huo ukiendelea, kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la James Charles, alisema, anampenda sana Diamond, lakini kitendo alichokifanya kinaonesha ishara ya ushirikina, huku akimtaka kuwaweka wazi mashabiki juu ya maana ya kushuka uwanjani na njiwa.“Bwana wewe Diamond ni mkali na mimi binafsi namkubali, ila kitendo cha kuingia na njiwa, binafsi kimenifanya nibaki mdomo wazi, ni vema angetupa tafsiri ya njiwa wale, anaanza kufanya nimuone wa ajabu na mwenye kuamini ushirikina,” alisema Charles.

Charles alipozidi kujitwika msimamo huo, dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Aisha Rashid, alisema kuwa, naye anamuunga mkono James kwa kuwa kitendo hicho, ingawaje hakuwepo uwanjani, lakini kwa sasa kimekuwa gumzo kwa wadau mbalimbali hapa nchini.

“Tunakubali kuwa, Diamond ni mkali, lakini kama anatafuta umaarufu kwa kufanya uchawi sio ishu, mimi simsapoti hata kidogo kwa hilo, bora angefanya kama wenzake ambao walipanda bila ya kuonyesha vitu hivyo, iwapo kweli ni mchawi, basi ajue hayo yanamwisho wake,” alisema Aisha.

Akizungumzia tukio hilo, Diamond alisema, kuingia kwake Uwanja wa Taifa na njiwa wanne, ilikuwa ni sehemu ya burudani tu na ubunifu kwa ajili ya kuwafurahisha wadau na mashabiki waliokuja katika tamasha hilo kwa lengo la kuburudika.
“Kufanya kwangu hivyo, ni sehemu tu ya utashi na mbwembwe za kiburudani, si imani za kishirikina, kama ambavyo mashabiki na wapenzi wamekuwa wakifikiria,” alisema Diamond ambaye alipambana na mkali kutoka Uganda, Jose Chameleon.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate