EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 16, 2012

SERIKALI YAONYA VIONGOZI WA DINI , KUJIHUSISHA KISIASA UVUNJIFU WA AMANI



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo , akihutubia waumini wa dini ya Kiislam ya Jumuiya ya Ahamadia (hawapo pichani)  
SERIKALI imesema migogoro ya kisiasa na kiitikadi ya kidini, kutokuwepo kwa mgawanyo sawa wa rasimali za nchi kunaweza kuleta uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini.
  Pia imewaonya wanasiasa na viongozi wa dini wanaochanganya siasa na mambo ya kiroho, kwa kisingizio cha cha dini kuacha kufanya hivyo, kwani wanasababisha uvunjifu wa amani.
  Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo, katika mkutano wa amani uliondaliwa na Jumuiya ya Waislamu ya Ahamadiya jijini hapa, mkutano ambao ulihudhuriwa na Amiri Sheikh Mkuu wa Jumuiya hiyo nchini, Tahir Mahamood , pamoja na viogozi mbalimbali wa madhehebu ya dini ya kiislamu na kikristo jijini .
  Ndikilo alisema, wapo viongozi wa dini wanachanganya siasa na mambo ya kiroho , wanapofanya hivyo wanavuruga amani ya nchi yetu na kuingiza jamii katika machafuko, ambapo aliwataka viongozi hao na wanasiasa kuacha kuchanganya mambo hayo kwani yatasababisha amani ya nchi yetu kuvurugika.
  “Dini ni kumcha Mungu, lakini siasa ni kuchukua dola au madaraka ya nchi.Wapo baadhi ya viongozi wa dini wanachanganya siasa na mambo ya kiroho, hao wanasababisha uvunjifu wa amani.Siasa tuwachie wanasiasa kwenye majukwaa yao.Serikali inawaunga mkono kutokana na juhudi zetu za kulinda na kutunza amani tuliyo nayo,” alisema Ndikilo.
  Alidai kuwa zipo kelele za dini kutaka kuhatarisha amani ya nchi yetu, kwani jumuiya ya dini nyingine ni kuikumbusha nyingine majukumu yake ya kuhubiri amani , hili litaepusha dhahama kwa nchi yetu.
  Alisema tabia ya vitisho na kukosa uvumilivu kwa baadhi ya dini kuendesha mihadhara ya kutukanana dini zingine ni kinyume cha maadili, kwamba dini zikitumika vibaya zitasababisha umwagaji damu.
  Ndikilo alisema kuwa, serikali inawajibika kuheshimu dini hizo na kutoa uhuru wa kuabudu kwa kila raia wa nchi hii, hivyo dini ni chombo cha kuunganisha wanadamu na ikitumika vizuri itakuwa ni mhimili wa amani duniani kote na si Tanzania pekee.
  “ Wote mmekiri hapa kuwa, amani ikitoweka wote tutaathirika,bila amani hakuna mtu atafanya kazi kwa uhuru,kila mtu atatafuta pa kutokea, hivyo mchango wenu madhehebu ya dini katika kudumisha amani nchini  ni mkubwa.Mmekuwa mkihubiri amani na upendo kwa kutumia neno lenu ‘mapenzi kwa wote bila chuki kwa yeyote’ lakini pia msmamo wenu wa kufuata sheria .Hakuna serikali inataka wananchi wake wasifuate sheria,” alisema
Ndikilo alisema migogoro ya kisiasa na kiitikadi inaweza kuhatarisha amani ya nchi  kutokana na mgawanyo usio sawa wa rasilimali za nchi, kwamba ubaguzi wa rangi, kijinsia,ukabila , ukanda na udini  unaweza kuvunja amani ya nchi.
  Hata hivyo alisema ni ndoto kufikiri kuwa Usilamu ama Ukristo utatoweka kwa kupitia mihadhara au kwa kuchoma Makanisa na Misikiti, kwani yalikuwepo na yartaendelea kuwepo duniani.Kwamba kuvumiliana na kuacha kuzungumza kwa hisia kutadumisha misingi ya amani ya nchi yetu.
  Ndikilo aliwataka viongozi wote wa dini kusaidiana na serikali katika kupiga vita rushwa,mauaji ya walemavu wa ngiozi, mauaji ya vikongwe na mamambukiz ya virusi vya ukimwi kwa kluwa yote hayo hayachagui imani ya mtu.
  Pia alisema kuwa amani huanza kujengwa katika ngazi ya familia na kuitaka jamii kukemea wizi (vibaka) uvaaji wa nguo fupi za nusu uchi na kuwalea watoto katika maadili mema, kwani huo ndio mwanzo wa amani katika ngazi ya familia.
  Alisema watoto kutukana wakubwani malezi mabaya, na  baadhi ya viongozi wa kisiasa kutukana viongozi wa kitaifa kwa kisingizio cha siasa ni uvunjifu wa amani nchini, ambapo alidai ushoga ambao upo katika familia lakini unafumbiwa macho nao ni cghanzo cha kuvunjika kwa amani.
“Kila mmoja ashiriki shughuli za maendeleo akiwa ana amani, waathirika wakubwa ni watoto na akina mama, lazima tuienzi amani tuliyo nayo kwa gharama yoyote , kila mmoja akiwajibika katika eneo lake nchi yetu itakuwa salama na amani,” alisema Ndikilo
 Awali Amiri Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahamadiya, Tahir Mahamood alisema kuwa alisema Quran inaelekeza kuhusu suala la amani na jinsi ya kupeleka ujumbe unaohusiana na amani.
Alisema falsafa ya Uislamu ni amani ni zawadi (tunu) kutoka kwa Mungu,n kukumbushana na jamii kuwa tunu hiyo (amani) tuitunze,kuipoteza ni rahisi lakini kuirejesha ni gharama kubwa.
  Alidai makundi mengi yanayojihusha na mauaji yakiwemo yale ya kigaidi, yanafanya hivyo kutokana na uelewa mdogo na  kinyume na imani ya dini ya Kiislamu kwa vile haifundishi hayo.
  “Vipo vikundi vya kigaidi vinatumia dini kufanya udhalimu.Waisalmu wengi wanatumiwa kujilipua, Wailsmu walikufa kwa kutetea imani ya dini yao, lakini si wale wanaojivika mabomu na kujilipua.Kwamba mtizamo huo umepokelewa na baadhi ya mashaeikh wa dini ya Kiislamu,kinyume na mafundisho ya mtume,” alisema Amiri Sheikh Mahamood na kuongeza;
  “  Mtume hakuletwa kwa ajili ya kujilipua, au kupambana na watu, alikuja kuwafikishia ujumbe wa wazi wazi,kwa anayetaka aamini na kutoa huduma kwa watu lakini si kuwauwa..
  Alisema dini ya kiislamu inashirikiana na dini zingine na misahafu yote ya dini inafundisha hivyo, na kuwataka Waislamu kutovunja makanisa wala misikiti kwa kuwa hizo ni nyumba za ibada.
Viongoizi wa dini mbalimbali za Kiislamu,Kikristo na Kihindu walihudhuria mkutano huo wa amani, ambao ulifanyika kwenye ukumbi wa Nyerere katika hoteli ya  Gold Crest, hapa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate