Asilimia 25 ya
wajawazito katika Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma bado wanajifungulia
nyumbani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutotaka kuzalishwa na
wauguzi wenye umri mdogo kuliko wao.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Dkt. Ntuli Kapologwe alisema hayo juzi mjini hapa katika mahojiano na gazeti hili (HabariLeo). Alisema kuwa wanaendelea na kampeni ya kutoa elimu ili wajawazito waone umuhimu wa kujifungulia hospitali na si majumbani kama wanavyofanya, “Wengi bado wana mila na desturi kuamua kujifungulia nyumbani kwa vile watumishi wanaowazalisha wana umri mdogo na wengi wanaona binti mdogo hawezi kumzalisha,” alisema.
Pia alibainisha kuwa mwaka 2010 kulikuwa na vifo saba vilivyotokana na uzazi na mwaka 2011 kulikuwa na vifo viwili na kwa mwaka huu mpaka sasa kuna kifo kimoja tu kilichotokana na uzazi.
Alisema hayo ni moja ya mafanikio yaliyopatikana kutokana na kuboreshwa kwa huduma za afya katika wilaya hiyo uliochangiwa kuwepo kwa mfumo mzuri wa rufaa ambapo vituo vinne vya afya vina magari ya kubebea wagonjwa. Vituo hivyo ni Bahi, Mundemu, Chipanga na Mtitaa.
Dkt. Kapologwe alisema kuwa Kituo cha Afya cha Chipanga kina huduma ya upasuaji ya uzazi wa dharura na watumishi wamekuwa wakipewa motisha ambapo watumishi wanaoishi mbali na vituo vya kazi wamepewa usafiri wa pikipiki, “Mwaka huu tutafungua zahanati mpya mbili katika Kijiji cha Mindola Kata ya Ilindi na Kijiji cha Magaga Kata ya Chifutuka,” alisema.
Dkt. Kapologwe alisema bado kwenye baadhi ya maeneo wananchi wanaamini kujitibia majumbani ndiyo njia bora kwani wengi bado wana imani za kishirikina ambapo wameendelea kurudisha nyuma juhudi za Serikali za kupambana na maradhi.
Pia alibainisha kuwa Wilaya hiyo bado haina hospitali ya Wilaya na wamekuwa wakiomba wafadhili na hata Serikali kuwezesha wilaya hiyo kuwa na hospitali ambapo mpango wa kujenga umeanza na eneo tayari limepatikana.
via HabariLeo
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Dkt. Ntuli Kapologwe alisema hayo juzi mjini hapa katika mahojiano na gazeti hili (HabariLeo). Alisema kuwa wanaendelea na kampeni ya kutoa elimu ili wajawazito waone umuhimu wa kujifungulia hospitali na si majumbani kama wanavyofanya, “Wengi bado wana mila na desturi kuamua kujifungulia nyumbani kwa vile watumishi wanaowazalisha wana umri mdogo na wengi wanaona binti mdogo hawezi kumzalisha,” alisema.
Pia alibainisha kuwa mwaka 2010 kulikuwa na vifo saba vilivyotokana na uzazi na mwaka 2011 kulikuwa na vifo viwili na kwa mwaka huu mpaka sasa kuna kifo kimoja tu kilichotokana na uzazi.
Alisema hayo ni moja ya mafanikio yaliyopatikana kutokana na kuboreshwa kwa huduma za afya katika wilaya hiyo uliochangiwa kuwepo kwa mfumo mzuri wa rufaa ambapo vituo vinne vya afya vina magari ya kubebea wagonjwa. Vituo hivyo ni Bahi, Mundemu, Chipanga na Mtitaa.
Dkt. Kapologwe alisema kuwa Kituo cha Afya cha Chipanga kina huduma ya upasuaji ya uzazi wa dharura na watumishi wamekuwa wakipewa motisha ambapo watumishi wanaoishi mbali na vituo vya kazi wamepewa usafiri wa pikipiki, “Mwaka huu tutafungua zahanati mpya mbili katika Kijiji cha Mindola Kata ya Ilindi na Kijiji cha Magaga Kata ya Chifutuka,” alisema.
Dkt. Kapologwe alisema bado kwenye baadhi ya maeneo wananchi wanaamini kujitibia majumbani ndiyo njia bora kwani wengi bado wana imani za kishirikina ambapo wameendelea kurudisha nyuma juhudi za Serikali za kupambana na maradhi.
Pia alibainisha kuwa Wilaya hiyo bado haina hospitali ya Wilaya na wamekuwa wakiomba wafadhili na hata Serikali kuwezesha wilaya hiyo kuwa na hospitali ambapo mpango wa kujenga umeanza na eneo tayari limepatikana.
via HabariLeo
No comments:
Post a Comment