EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 8, 2012

LOWASA; TUKO TAYARI KWA VITA

KAMATI ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, imesema majeshi ya Tanzania yapo tayari kiakili na kivifaa ikibidi kuingia vitani kutokana na mzozo wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi.

Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward Lowassa alipozungumza na waandishi na habari na kusisitiza Tanzania inaomba isifike katika hatua hiyo, lakini ikibidi wanajeshi wetu wapo imara kutetea mipaka ya nchi hadi tone lao la mwisho la damu.
“Jeshi letu lipo tayari, na tumeridhika na utayari wao na ‘commitment’ yao. Sisi ni moja ya jeshi lililojiandaa vizuri sana na miongoni mwa majeshi mazuri duniani. Tunajivunia vijana wa Tanzania waliopo kwenye jeshi letu. Tupo imara kiakili, vifaa vya kisasa,” alisema.

Alisema kamati hiyo inaunga mkono kauli ya serikali iliyotolewa juzi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, kwani ni sahihi inayoelezea msimamo wa Tanzania kuhusu jambo hilo.
Alisema kuwa wanategemea jambo hilo litamalizika kidiplomasia ndani kwa ndani ama ikibidi kuomba msaada wa watu wengine kusuluhisha kwa kuwa Tanzania na Malawi ni marafiki na ndugu.

“Watu waliopo mipakani ni ndugu, tusingependa kufika mahali kutokuelewana mpaka kuhusisha vyombo vya ulinzi na usalama, lakini kwa faida ya Watanzania tumepewa maelezo ya jeshi letu, tumeridhika kwamba ikibidi jeshi letu limejipanga vizuri sana.

“Watanzania wasiwe na shaka yoyote, wanajeshi wamejipanga vizuri na kwa uhakika na kama ilivyo ahadi yao, wapo tayari kulinda nchi yetu mpaka tone la mwisho la damu yao,” alisema na kuongeza kuwa kama wabunge, nao wameridhika na maandalizi ya jeshi, kwani wapo imara na timamu.
Alisema serikali haitaki kufika huko, kwani wakati wa Vita ya Uganda mwaka 1978, wananchi waliumia na kwamba kama nchi, inafahamu athari za vita kiuchumi na kwa maisha ya binadamu.

“Hatutaki kufika huko kwani si jambo jema, ndiyo maana tunasema tumalize kwa njia ya mashirikiano na kwa mazungumzo ya kidiplomasia ya mawaziri wanaohusika ikishindikana tutafute msuluhishi,” alisema.
Mwaka 1978, Tanzania iliwahi kuingia katika vita na Uganda, baada ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Iddi Amin Dada, kuvamia sehemu ya Tanzania na kudai kuwa ni yao.
Juzi, Membe alitoa tamko la serikali na kuyataka makampuni yote yanayoendelea kufanya utafiti wa mafuta katika ziwa hilo kuondoka mara moja pamoja na Serikali ya Malawi kuheshimu mazungumzo yaliyofikiwa. Alisisitiza eneo linalobishaniwa katika ziwa hilo lipo Tanzania.

Alisema pamoja na Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuzipiga marufuku ndege za utafiti za kampuni hizo, bado zilikaidi na ndege tano zilitua katika eneo la Ziwa Nyasa.
“Serikali ya Tanzania inapenda kuzionya na kuzitaka kampuni zote zinazoendelea na shughuli za utafiti katika eneo hilo zisitishe mara moja kuanzia leo Jumatatu,” alisema Membe na kuongeza kuwa, Serikali ya Tanzania iko tayari kulinda mipaka yake kwa gharama yoyote.

Alisema kwa kuzingatia nyaraka zilizotengenezwa na wakoloni wa Kiingereza mwaka 1928 na 1938, zinaonesha kuwa mpaka wa ziwa hilo upo katikati.
Alisema hoja ya Tanzania ina nguvu kulingana na sheria za kimataifa kwa vile tatizo kama hilo linafanana na mgogoro uliokuwepo kati ya Cameroon na Nigeria.
Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate