EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 7, 2012

Mku wa wilaya ya Bunda amtia ndani Afisa Afya kwa kuzembea

MKUU wa Wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe amechukua maamuzi ya kumuweka rumande Ofisa Afya wa Mji mdogo wa Kibara James Manaji kwa kile alichokieleza kushindwa kusimamia shughuli za Afya katika Mji huo na kupelekea kuonekana usiofaa kwa makazi ya Binadamu.

Akizungumza na BINDA NEWS Mkuu huyo wa Wilaya alisema Afisa huyo ameshindwa kutelekeza majukumu yake ya kazi kwa kushindwa kusimamia shughuli zake na kupelekea kuonekana Mji mchafu huku akiendelea kuchukua mshahara wa Serikali pasipo kufanya kazi zilizopo mbele yake.

Alisema makazi ya Wananchi wengi katika Mji huo zinaishi bila ya kuwa na vyoo hivyo kujisaidia ovyo na kuhatarisha Afya na hivyo huenda kupelekea kuibua kwa magonjwa na mlipuko ambayo yataatarisha maisha ya Binadamu.

Mirumbe alisema Afisa huyo ameshindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo katika masuala ya Afya kwa kusema suala la choo ni muhimu katika makazi na tayari yalishatolewa maagizo muda mrefu kwa Maafisa wote wa Afya kuhakikisha kila kaya inakuwa na choo kwa ajili ya kujiepusha na magonjwa ya mlipuko.

“Ni kweli nimemuweka ndani Afisa Afya wa Mji mdogo wa Kibara kwa kushindwa kusimamia majukumu yake na suala hili ni nyeti kwa sababu hakuna jambo muhimu kama kuzingatia taratibu za Afya hususani kuwa na choo katika makazi kwa sababu tulishatoa maelekezo.

“Na hili si kwa kibara tu, nimeshatoa maelekezo katika maafisa watendaji wote wa vijiji kuhakikisha kila kaya inakuwa na choo na kuhakikisha mazingira ya usafi yanasimamiwa vizuri ili Wilaya ya Bunda ionekane ipo katika mazingira ya usafi kwa wakati wote,”alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

Alisema suala la uwajibikaji kwa watumishi wa idara zote lazima lizingatiwe na kudai kuwa ataendelea kufanya ufatiliaji bila kikomo ili kila mmoja aweze kutimiza wajibu wake wa kazi na kukomesha tabia ya kukaa ofisini na kupiga gumzo huku kazi zikiendelea kusimama.

DC Joshua Mirumbe alichukua maamuzi ya kumuweka ndani Afisa huyo wa Afya akiwa katika Mji huo wa Kibara wakati akikagua shughuli za maandalizi yakiwemo ya usafi kwa ajili ya kupokea mwenge wa Uhuru ambao unatarajiwa kuwasili Mjini Bunda agosti 18 huku miradi mbalimbali ya maendeleo ikitarajiwa kuzinduliwa.

Kwa upande wake Afisa huyo wa Afya wa Kibara James Manaji akizungumza na BINDA NEWS baada ya kutoka ndani alikokaa kwa muda wa zaidi ya masaa 24 kabla ya kuamuliwa kutoka, alisema alishangazwa na maamuzi ya Mkuu huyo wa Wilaya kumuweka ndani bila ya kufanya Takwimu juu ya uhamasisishaji wa ujenzi wa vyoo.

Alisema kazi ya uhamasishaji wa ujenzi wa vyoo inaendelea kufanyika vizuri katika vijiji vyote vinee vya Mji huo na hatua iliyochukuliwa na Mkuu huyo wa Wilaya haikuwa sahihi kwa kuwa hakufanya utafiti wowote juu ya jamabo hilo tangu ulipoanza utekelezaji wa kazi hiyo.

Alidai kuwa DC huyo amekuwa akichukua maamuzi mengine ambayo sio haki tangu alipoteuliwa kusimamia Wilaya hiyo kwa mujibu wa dhana ya utawala bora na kudai kuwa katika siku za vivi karibuni amekuwa akichukua maamuzi kama hayo bila kufanya utafiti na kuvunja haki za msingi za Binadamu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate