EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 7, 2012

MKE WA SLAA ATEGEWA FUMANIZI



Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
KUNA taarifa kwamba mke wa Dk. Wilbroad Slaa (pichani), Josephine Mushumbusi ametengenezewa mtego ili afumaniwe na mume wa mtu.
Vyanzo vyetu vya habari vimesema kuwa mpango huo wa fumanizi umeandaliwa na chama kimoja cha siasa (jina tunalihifadhi) ili kumharibia Josephine na mumewe ambaye ni katibu mkuu wa Chadema katika medani ya siasa.
 
Mtoa habari wetu alibainisha kuwa maandalizi ya mpango huo yanafanyika Dodoma ambako kumekuwa na mikutano kadhaa ya wahusika ambapo mikakati inapangwa ya jinsi ya kumfumania na mume wa mtu ambaye tayari ameandaliwa na kuahidiwa kitita kikubwa cha fedha.
Habari zinasema kundi hilo limetengewa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya operesheni hiyo maalum inayoongozwa na kada wa chama kimoja ambaye jina lake linaanzia na herufi M.
Imeelezwa kuwa mume wa mtu aliyepatikana ameanza kazi kwa kumtumia Josephine ujumbe wa kimapenzi katika simu huku akimuahidi kitita kikubwa cha fedha.
 
“Huu ni mkakati wa kisiasa nia ikiwa ni kuwamaliza Dk. Slaa na mkewe katika ulingo wa siasa kwani Josephine akinasa basi umaarufu wa mumewe utakuwa umekwisha. Lakini habari hii siyo siri tena na waliopanga mpango huu wana hali tete baada ya kujua kuwa njama zao zimegundulika,” alisema mtoa habari wetu.
Gazeti hili lilipopata taarifa hizi liliwasiliana kwa njia ya simu na Josephine na alipoulizwa kama anajua chochote kuhusu mpango huo alikiri kufahamu.
 
“Ni kweli mpango huo upo na nimekuwa nikipokea SMS nyingi za kimapenzi na nimemuonesha Dk Slaa,” amesema Josephine juzi Jumapili.
Hivi karibu wakili maarufu nchini, Mabere Marando aliwahi kulalamika akidai kuna mtambo wa mawasiliano ambao umeingizwa nchini kinyemela ambapo mtu unaweza kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno kwa kutumia kifaa hicho, hali ambayo imesababisha watu mbalimbali waliozungumza na gazeti hili kudai kuwa inawezekana ndiyo unaotumika kumsumbua Josephine.
 
Nalo jeshi la polisi nchini, lilipoulizwa na gazeti hili kuhusu madai hayo, limesema linaendesha uchunguzi wa madai ya Marando.
Msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso alisema baada ya madai hayo kutolewa, jeshi hilo, kupitia Kitengo cha Simu na Ufuatiliaji, limeanza kazi ya kuchunguza ukweli wa mashine hiyo na kama kweli kuna anayefanya kitendo hicho, hatua kali sana zitachukuliwa.
 
“Taarifa za kuwapo na mtambo wa kuingilia mawasiliano ya simu ya mtu mwingine zimetufikia, tunachunguza kwa ukaribu, tunajua suala hili lilianzia bungeni na sasa lipo ndani ya jamii. Kuingilia mawasiliano ya mtu mwingine bila ridhaa yake ni kosa la jinai, sasa tusianze kuhukumu kitu ambacho hatuna uhakika nacho, tusubiri kazi ya uchunguzi ikamilike,” alisema Senso.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate