EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, October 21, 2012

Serikali yapiga marufuku mihadhara nchi nzima.

SERIKALI imepiga marufuku mihadhara ya kidini nchi nzima kwa siku 30 ikiwa ni moja ya hatua ya kukabiliana na machafuko ya kidini yanayolinyemelea taifa.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi alitangaza hatua hiyo ya Serikali jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Waziri Nchimbi alisisitiza  kuwa Serikali pia inafanya uchunguzi ili kubaini kama vurugu hizo zina mkono wa makundi ya nje ya nchi.
Alisema kuwa, Serikali sasa haitawabembeleza watu wanaoeneza chuki za kidini kwa sababu ni wajibu wake kulinda amani kwa wananchi wake.

Waziri huyo alieleza kusikitishwa na vurugu zilizotokea juzi Ijumaa maeneo mbalimbali jijini baada ya baadhi ya Waislamu kujiandaa  kuandamana  kwenda Ikulu kushinikiza kutolewa rumande kwa kiongozi wao, Sheikh Issa Ponda.
Waandamanaji hao pia walipinga tukio la kukojolewa kwa kitabu kitakatifu cha Kurani na mtoto lililotokea mwanzoni mwa wiki eneo la Mbagala.

“Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ametangaza juzi kusitisha mihadhara ya nje kwa siku 30. Na mimi natumia fursa hii kutangaza kusitisha mihadhara hiyo kwa nchi nzima kwa siku 30, hadi tutakapoona hali imetulia,” alisema Nchimbi.
Waziri Nchimbi alikiri pia kwamba, Serikali imekuwa ikikosea kuwakamata watu wanaofanya vurugu wakati wa maandamano na kuwaacha wanaoshawishi na kuwezesha maandamano hayo.
“Huo ndiyo uamuzi mpya wa Serikali. Anayeshawishi, anayefanikisha na anayewezesha, wote watakamatwa. Tumegundua kwamba, tulikuwa hatufuati sheria kwa kuwakamata tu wanaotenda. Ndiyo maana baada ya upelelezi tukaona kuwa wasaidizi wake (Ponda), waliwashawishi watu waandamane kwenda Ikulu ,au gerezani ili wamtoe (Ponda) rumande,” alisema Dk Nchimbi.

Alipongeza Mwananchi
Katika hatua nyingine, Waziri Nchimbi alilimwagia sifa gazeti la Mwananchi kwa tahariri zake zinazohimiza kudumishwa kwa amani, hasa baada ya matukio ya uvunjifu wa amani, ikiwamo kuchomwa moto na kuibwa kwa mali za makanisa hivi karibuni.
Katika tahariri yake ya jana iliyochapishwa ukurasa wa mbele ikiwa na kichwa cha habari  ‘Chonde chonde tunaomba amani’, gazeti hili lilionya juu ya uwezekano wa kuvunjika kwa amani na likataka pande zinazohusika kujiepusha na matukio yanayoweza kulitumbukiza taifa katika machafuko.

Waziri Nchimbi alisisitiza kuwa Serikali inafuata utawala wa sheria, hivyo haitaruhusu watu kufanya maandamano kwenda popote ili kushinikiza kumtoa mahakamani mtu aliyetuhumiwa hadi mahakama itakapotoa uamuzi wake.
“Mahakama peke yake ndiyo yenye mamlaka ya kutoa hati ya mtu, hivyo kujaribu kumtoa mtu aliyefikishwa mahakamani ni kosa kisheria,” alisisitiza.
Huku akitaja mifano wa baadhi ya nchi duniani ambazo zimewahi kukumbwa na machafuko ya kidini, Dk Nchimbi alisema kuwa Serikali haitavumilia mtu au kikundi chochote kitakachoonekana kikieneza chuki za kidini.

“Staili yetu ya kucheka na wavunja amani inatuharibia. Kwetu sisi amani ni muhimu mno….Wote mnajua jinsi chokochoko za kidini zilivyoleta madhara nchini Nigeria, hakuna anayetaka kwenda tena huko, watu zaidi ya  milioni mbili waliuawa. Migogoro ya dini iliwahi kuzikumba nchi za Ulaya miaka 400 iliyopita na kusabanisha vifo vya watu milioni nne,” alisema na kuongeza:
“Huko Lebanon, Waislamu wa madhehebu ya Sunni walikuwa wakigombana na Wakristo. Hadi wanakuja kutafuta suluhisho tayari watu 250,000 walikuwa wameuawa… Hivi kweli Watanzania na sisi tutasubiri hadi watu milioni tisa wafariki, mali ziharibiwe halafu ndiyo tujadiliane?”
Dk Nchimbi amewaonya wanasiasa kutochukulia vurugu hizo kwa masilahi ya kisiasa, huku akiwataka wananchi na vyombo vya habari kutoshabikia uvunjifu wa amani.
Kuhusu vyombo vya habari vya kidini vinavyoeneza chuki alisema Serikali itaiwajibisha Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na taasisi nyingine za Serikali zinazosimamia, endapo kutakuwa na redio au televisheni na magazeti yanayoeneza maneno ya chuki za kidini.
Akizungumzia suala la kuonekana kwa kiongozi wa kundi la Uamsho la Zanzibar Sheikh Farid Hadd, Dk Nchimbi alisema kuwa baada ya kuonekana huko jeshi la polisi limemkamata na linamhoji ili kujua alikokuwa na kwa nini alipotea na kusababisha wafuasi wake wafanye vurugu iliyosababisha pia kuuawa kwa askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia.Chanzo cha habari na Mwananchi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate