EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 20, 2012

CCM yajipima kwa CHADEMA vigogo wapya, mawaziri kuanza ziara mikoani.

KATIKA mikakati yake ya kupambana na nguvu za operesheni za CHADEMA mikoani, Chama cha Mapinduzi (CCM), kimelazimika kuwatumia viongozi wake wapya wakiongozana na mawaziri ili kwenda mikoani kufafanua kwa wananchi jinsi serikali ilivyotekeleza ilani yake.

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa chama hicho kujaribu kukabiliana na upinzani wa CHADEMA mikoani, ambapo mwaka jana baada ya mkutano wao wa maazimio ya kujivua gamba, walijitahidi kuzunguka baadhi ya mikoa bila kufua dafu.
Operesheni zinazofanywa na CHADEMA za Sangara na sasa Vuguguvu la Mabadiliko (M4C), zimeitikisa CCM na hivyo wajumbe wake kutumia muda mwingi kwenye mkutano mkuu wao uliomalizika mjini Dodoma, kujitapa kuwa lazima wafanye mashambulizi ya kuwasambaratisha.

Akitangaza mkakati huo mpya jana kwa waandishi wa habari wa kuchanja mbunga kwa kutumia anga kwa helikopta kama CHADEMA, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema wameanda ziara ya siku nne katika mikoa minne.
Alisema ziara hiyo itaongozwa na sekretarieti mpya chini ya Katibu wake Mkuu, Abdullahman Kinana, na kuwashirikisha baadhi ya mawaziri.
Nape alisema kuwa ziara hiyo ni ya chama na sio ya kiserikali na kwamba itaanza kesho hadi Novemba 24 katika mikoa ya Mtwara, Arusha, Geita na Rukwa.

Akifafanua zaidi alisema Kinana ataanzia Mtwara ambako atakuwa na mawaziri husika wanaoshughulikia masuala ya kilimo ili kuzungumzia zao la korosho na waziri wa uchukuzi atakayezungumzia bandari na miundombinu.
Nape aliongeza kuwa wakiwa Sumbawanga watazungumzia miundombinu na kwa Geita watafuatilia migogoro ya migodi na kumalizia Arusha kwa kuangalia harakati za kufufua viwanda kwani vinaathiri ajira.

Nape alisema kuwa lengo la kuongozana na baadhi ya mawaziri ni kutoa maelezo ya papo hapo hasa kwa mambo yanayosuasua ikiwemo kuwawajibisha bila kusubiri Bunge kufanya hivyo.
“Lengo tunasukuma spidi ya utekelezaji wa maendeleo na ilani ya uchaguzi na tunajikita kwa baadhi ya mambo na kuendeleza mageuzi ndani ya chama na ndio azimio tuliloondoka nalo katika mkutano mkuu wa nane,” alisema.

Akizungumzia kung’atuka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, Nape alisema kiongozi huyo ameondoka ili akasimamie uanzishwaji wa chuo cha uongozi cha CCM, ambacho kitasaidia makada kuwa na nidhamu na uwajibikaji.
Akijibu hoja za CHADEMA zinazodai CCM imetekeleza ilani ya chama hicho hususan katika suala la elimu na kupunguzwa kwa bei za vifaa vya ujenzi, Nape alisema kuwa suala la elimu bure ni la CCM.
“Suala hilo lilianza wakati wa TANU chini ya Mwalimu Julius Nyerere na hata hao kina Dk. Slaa wamesomeshwa bure na TANU,” alisema.

CHADEMA wajiimarisha
Wakati CCM ikianza ziara mikoani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeanza kujiimarisha kwa kuendesha mafunzo ya darasani na vitendo, kwa lengo la kuwajengea uwezo wenyeviti na makatibu wa mikoa 32 ya kichama.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni wa CHADEMA, Benson Kigaila, alisema kuwa mafunzo hayo yatafanyika Novemba 22 hadi 23, mwaka huu, wilayani Karagwe, mkoa wa Kagera.
Kigaila alisema baada ya mafunzo hayo wataingia kwenye vitendo ambapo makatibu na wenyeviti hao watasambaa kushambulia vitongoji na vijiji vyote vya wilaya ya Karagwe, kwa kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo hayo.

Alibainisha kuwa mafunzo hayo ya vitendo ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya ujenzi na uimarishaji wa chama, hususan operesheni ya M4C ambayo imesaidia viongozi kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya ndani na hadhara.
Kuhusu M4C, Kagaila alisema wakati viongozi hao waliopata mafunzo wakiendelea, chama kitatoa ratiba ya operesheni hiyo kubwa itakayoendelea kufanyika kwa nchi nzima.
Habari hii imeandaliwa na Happiness Mnale na Shehe Semtawa

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate