EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 20, 2012

HATIMAE MUUMIN AIHAMA RASMI TWANGA PEPETA.

HATIMAE mwimbaji maararufu wa muziki wa dansi, Mwinjuma Muumin ameihama rasmi Twanga Pepeta.
Akiongea na saluti5 usiku wa jana kuamkia leo, mwimbaji huyo alisema kwa nia njema kabisa bila ugomvi wala mgogoro wowote ameihama Twanga Pepeta na kujiunga na bendi changa ya Victoria Sound yenye maskani yake jijini Dar es Salaam.Muumin amesema kesho Jumatano atakwenda Idara ya Habari (Maelezo) kuongea na Waandishi wa habari.
Mapema jana mchana saluti5 ilimtembelea Muumin nyumbani kwao Bagamoyo (kama picha zinavyoonyesha hapo juu) ambapo licha ya kuongea mengi lakini alikataa kuzungumzia uvumi uliozagaa kuhusu kuhama kwake Twanga Pepeta.
“Mimi hadi muda huu bado ni mwanamuziki wa Twanga ila baadae nitakuja town (Dar es Salaam), tutafutane usiku pengine nitakuwa na kitu tofauti cha kukueleza” alisema Muumin katika maongezi yake na saluti 5 jana mchana.
Hatimae saluti5 ikakutana tena na Muumin saa 6:45 jana usiku jijini Dar es Salaam na ndipo alipoweka mambo hadharini kuwa ameihama rasmi bendi aipendayo sana ya Twanga Pepeta.
“Ni uamuzi mgumu sana, naipenda Twanga Pepeta, nilipata malezi mazuri kuanzia kwa uongozi, wanamuziki, maseneta hadi mashabiki.
“Kibinaadamu najua ziko sehemu kadhaa ambazo tulikwazana lakini sitapenda mazuri mengi niliyoyapata pale yafunikwe na mabaya machache, itakuwa ni ukosefu wa fadhila, naomba wote watakaoumizwa na kuhama kwangu wanisamehe na tulindiane heshima.
“Haitakuwa jambo jema mimi au Twanga Pepeta tukaanza kupita huku na kule na kuchafuana, bado naichukulia Twanga na Aset kwa ujumla kama nyumbani kwangu” alisema Muumin.
Alipoulizwa ni kwanini ameihama Twanga wakati aliahidi kumalizia muziki wake kundini hapo, Muumin alisema amezingatia vitu viwili.
Kwanza ni dau alilopewa Victoria Sound, pili ni uchanga wa bendi aliyojiunga nayo. “Naiona Victoria kama bendi changa ambayo haitaweza kuwa bendi shindani kwa Twanga Pepeta, kamwe nisingethubutu kujiunga na bendi yeyote shindani kwa Twanga” alisema Muumin aliyetunga wimbo Penzi la shemeji katika albam ya Dunia Daraja.
Aidha, Muumin aliongeza kuwa anaamini kuwa kuondoka kwake Twanga Pepeta hakutaacha pengo lolote kwa vile ina mkusanyiko wa wanamuziki wenye vipaji vya hali ya juu.
Muumin amesema changamoto aliyonayo sasa ni ya kutengeneza nyimbo nzuri kwa bendi yake mpya ili kuitoa katika hatua moja kwenda hatua nyingine.
Kuondoka kwa Muumin Twanga Pepeta kunahitimisha wingu zito lililokuwa limetanda kufuatia kutoonekana kwake jukwaani wiki nzima iliyopita.
                         CHANZO CHA HABARI SALUTI5

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate