Na Mwandishi Wetu
YAPO madai kwamba, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeshikilia makombora mazito ya kashfa ya Waziri Mkuu aliyestaafu, Mheshimiwa Edward Lowassa na kwamba chama hicho cha siasa kinamtegea jambo kiongozi huyo wa zamani wa serikali.
YAPO madai kwamba, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeshikilia makombora mazito ya kashfa ya Waziri Mkuu aliyestaafu, Mheshimiwa Edward Lowassa na kwamba chama hicho cha siasa kinamtegea jambo kiongozi huyo wa zamani wa serikali.

Waziri Mkuu aliyestaafu, Mheshimiwa Edward Lowassa.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba, Chadema kimekuwa
kikimchimba kwa siri Lowassa kwa kukusanya tuhuma zake nzito
watakazozilipua pindi CCM itakapompitisha mheshimiwa huyo kuwa mgombea
urais.Hata hivyo, licha ya Chadema kutega walichotega, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli hata mara moja hajawahi kutamka hadharani kwamba atagombea urais kupitia CCM mwaka huo.
Habari za uchunguzi zinadai kwamba tayari Chadema kina mabomu kadhaa ambayo hawataki kuyafyatua dhidi ya Lowassa na ndiyo maana hakuna hata siku moja ambayo viongozi wa chama hicho wamemshukia Lowassa kama wanavyofanya kwa viongozi wengine wa CCM.
Mwenyekiti wa Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe.
Uchunguzi ukazidi kudai kuwa Chadema ambayo ipo chini ya mwenyekiti
wake, Freeman Mbowe, imekuwa ikiomba kila kukicha chama tawala
kimpitishe Lowassa ikiamini kwako atakuwa kibonde kwenye uchaguzi huo.“Sisi Chadema tumekuwa kimya kuhusu Lowassa kwa muda mrefu siyo kwamba tunamuogopa au tunataka aje katika chama chetu, ukweli ni kwamba mabomu yake tunayo, tunasubiri uchaguzi mkuu. Tukifanya hivyo sasa, wakati ukifika tutapigana vipi?” alisema kiongozi mmoja wa Chadema ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini.
Wakati hali Chadema ikiwa hivyo, kuna habari kwamba, Lowassa naye ana makombora ya viongozi wa chama hicho akisubiri wakati wa kuyalipua.
Hata hivyo, hakuna kiongozi hata mmoja wa Chadema ambaye alikuwa tayari kusema bomu japo moja la Lowassa ambaye wachunguzi wa mambo wanasema kama ataamua kugombea atapeta katika Halmashauri Kuu ya CCM kwa kuwa ana wafuasi wengi wanaomkubali.
CHANZO CHA HABARI NA GLOBAL PUBLISHERS.
No comments:
Post a Comment